BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

Dk Slaa, Mnyika, Lema matatani

Written By Koka Albert on Tuesday, July 10, 2012 | 5:56 AM

POLISI KUWAHOJI KWA MATAMSHI KWAMBA WANATISHIWA MAISHA, DK NCHIMBI ASEMA WANASABABISHA CHUKI
Neville Meena na Florence Majani, Dodoma
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Godbless Lema huenda wakajikuta matatani kutokana na madai waliyoyatoa juzi kwamba wanatishiwa kuuawa na kigogo mmoja wa Idara ya Usalama wa Taifa.Kutokana na matamshi hayo, jana Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi ameliagiza Jeshi la Polisi kuwahoji viongozi hao ambao walidai kuwa mauaji hayo yamepangwa kufanywa kwa kuwekewa sumu kwenye chakula au kwa kutumiwa makundi ya ujambazi.

Akizungumza na waandishi wa mjini hapa jana, Dk Nchimbi alisema licha ya kudai kwamba wanatishiwa, ameshangazwa na msimamo wa viongozi hao kukataa kupeleka suala hilo polisi kwa madai ya kuhofia suala hilo halitafanyiwa kazi.

Alisema watawahoji viongozi hao kwa sababu suala la usalama wa Mtanzania yeyote si la hiari, bali ni la kikatiba na la kisheria hivyo, ni lazima polisi watimize wajibu wao.

“Ni lazima tuwahoji ili tujue ni nani amewatisha na kwa sababu zipi. Hatutamuomba mtu ruhusa ya kumlinda kwa sababu huo ni wajibu na kazi yetu kuwalinda raia, hilo halina mjadala. Hatua zitachukuliwa endapo itabainika kuwa madai yao yana ukweli,” alisema Dk Nchimbi.

Aliwataka viongozi  wote wa kisiasa wakiwamo wa Chadema wanapohisi kutishiwa usalama wao, watoe taarifa polisi ili vyombo vya dola viyafanyie uchunguzi malalamiko yao ili utaratibu ufanyike kuhusu usalama wao kama sheria inavyotaka.

Alionya tabia ya viongozi kuzungumza nje ya utaratibu akisema haikubaliki kwani inaweza kuwa ni mbinu za kujitafutia umaarufu wa kisiasa.

Dk Nchimbi alisema jambo hilo si jema kwani linajenga hofu miongoni mwa Watanzania na kuwafanya wasiviamini vyombo vyao vinavyowalinda kwa mujibu wa sheria.
“Ni kweli kuwa kila mwanasiasa anataka kukubalika na umma lakini, akubalike katika taratibu zinazokubalika,” alisema Dk Nchimbi na kuongeza:

“Ingekuwa Serikali inataka kukubali umaarufu kama huo, basi ingetumia mwanya wa haohao Chadema wakati mitandao ya kijamii iliposambaza taarifa kuwa Chadema ilihusika na kifo cha marehemu, Chacha Wangwe.”

Alisema Serikali haikukurupuka na kuwakamata, badala yake ilifanya uchunguzi kwanza na matokeo yake alikamatwa  dereva wake ambaye ameshachukuliwa hatua.
Alisema kama Serikali ingekuwa inatafuta umaarufu, ilikuwa ni fursa nzuri kwake kujipatia umaarufu na kukivuruga chama hicho kwa kuwakamata viongozi wa Chadema hasa baada ya kuwapo kwa uvumi kwamba wamemuua kiongozi huyo.

“Viongozi wetu wa kisiasa ni lazima wafanye mambo ambayo kesho na keshokutwa watakiri mchango wao, ama katika ujenzi au uharibifu wa nchi yetu. Kila siku wakilalamika kuwa wanataka kuuawa basi ni lazima watu watawashangaa kwani badala ya kutatua matatizo ya wananchi wanabaki wakilalama wanataka kuuawa. Watu kama hawa wanafanya hivi kwa masilahi yao, wanaweza kuwagombanisha wananchi.”

Waziri Nchimbi aliwataka wananchi na viongozi wa kisiasa kuondoa hofu kwani Serikali ina wajibu wa kuwalinda na hakuna mtu atakayenufaika kwa mauaji ya wanasiasa hao.

Kuhusu madai kwamba polisi wamekuwa wakipuuza malalamiko ya wapinzani, Dk Nchimbi alikiri kuwapo kwa baadhi ya polisi wenye kasoro katika utendaji wao lakini akasema wengi ni waadilifu.
Alisema ikiwa kuna mtu haridhishwi na utendaji wa polisi kwa kutopata huduma kama inavyostahili, ana uhuru wa kutoa taarifa katika ngazi za juu hata ikiwa ni kwake.

Ikulu nayo yatoa tamko

Katika hatua nyingine, Ikulu imesema hakuna mpango wowote unaoratibiwa na Idara ya Usalama wa Taifa kwa lengo la kuwaua viongozi hao wa Chadema.
Jana, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alihoji sababu za Serikali kutaka kuwaua viongozi hao wakati si tishio lolote kwa nchi.

Balozi Sefue alisema Idara ya Usalama wa Taifa haiko kwa ajili ya kuua raia au viongozi, bali kulinda masilahi ya taifa na kuhoji: “Sasa kwa nini wauawe? Wana nini hasa hadi Idara ya Usalama ifanye hivyo?”

Alisema ni vyema wakati mwingine kukawa na umakini kwa kuangalia namna siasa zinavyoweza kufanya kazi... “Hii inaweza kuwa siasa tu. Sisi serikalini hatuna mambo ya vyama, tunafanya kazi kwa ajili ya watu wote.”

Alisema Idara ya Usalama wa Taifa na Serikali hazifanyi kazi kisiasa, bali kwa kuangalia masilahi ya Watanzania wote: “Huku serikalini sisi hatuna ugomvi na wanasiasa. Tunafanya kazi na watu wote.”
Alisema wanaoweza kufikiria kuwa kuna siasa katika Serikali na vyombo vyake wao ndiyo wanaweza wakawa wanafanya siasa.

Tuhuma za Chadema
Kauli hizo za Serikali zinatokana na tuhuma za Chadema kwamba kimebaini njama za kuwaua viongozi wake hao waandamizi ambazo zinaratibiwa na kigogo mmoja wa Idara ya Usalama wa Taifa na kwamba nyendo zao zimekuwa zikifuatiliwa kwa saa 24.

Tuhuma hizo za Chadema zilitolewa juzi na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni akisema: “Sisi Chadema hatuna mambo ya siri tunayotaka kufanya katika nchi hii. Matatizo ya Watanzania yapo wazi na yanajulikana na kila mmoja, Serikali ya CCM itekeleze sera na ahadi zao kwa wananchi na si vitisho.”

Mapokezi ya kocha mpya ya Yanga

Written By Koka Albert on Wednesday, July 4, 2012 | 7:41 AM

 
Kocha mpya wa Yanga, Mbelgiji Thom Saintfiet amewasili mida hii Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam na kulakiwa na mamia ya wapenzi wa klabu hiyo. Tazama mapokezi yake tangu anatokea ndani ya Uwanja wa Ndege, hadi akiwa ndani ya gari tayari kwa safari ya Jangwani.










GRAND LAUNCH NEW MAISHA CLUB DODOMA

Sakata la Ulimboka latikisa Bunge

Written By Koka Albert on Tuesday, July 3, 2012 | 7:15 AM

MBILINYI AFANANISHA WALIOMTEKA NA JANJAWEED, WAZIRI NAGU AINGILIA KATI
Waandishi Wetu
KITENDO cha kutekwa nyara, kuteswa na kisha kuumizwa mwili mzima, kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka jana kilitikisa Bunge huku wabunge wa CCM na Chadema wakitupiana mpira kuhusu nani waliohusika na tukio hilo.

Msuguano huo ulianza baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi kudai kuwa waliofanya kitendo hicho ni sawa na wanamgambo hatari wa Janjaweed wa Sudan.  

Kauli hiyo ya Mbilinyi maarufu kwa jina Sugu, ilizusha tafrani ndani ya Bunge kwani Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji), Dk Mary Nagu aliomba mwongozo wa Mwenyekiti wa Bunge, Sylivester Mabumba aliyekuwa akiendesha Bunge jana jioni akihusisha matamshi hayo na kuituhumu Serikali kutumia watu kama Janjaweed katika kumteka Dk Ulimboka jambo ambalo alisema siyo la kweli.

Akichangia Hotuba ya Ofisi ya Rais, (Utumishi, Utawala Bora, Ikulu na Mipango) Mbilinyi alisema kitendo alichofanyiwa Dk Ulimboka ni cha kinyama na baadhi ya watu wanaamini kwamba Serikali ilihusika, hatua ambayo ilimfanya Dk Nagu kusema Mbilinyi alikuwa akizungumzia jambo ambalo hana uhakika nalo na kutaka aamriwe kuthibitisha.

Mwenyekiti Mabumba alimtaka Mbilinyi athibitishe kauli yake au aifute. Wakati Mabumba akimtaka Mbilinyi kuthibitisha au kufuta kauli yake, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu alitaka kuingilia kati suala hilo na hata kuwasha kinasa sauti, lakini Mabumba alimwamuru akae chini.
Mbilinyi alipopewa nafasi alisisitiza: “Waliomteka Dk Ulimboka walikuwa na silaha kama siyo askari, basi hawana tofauti na kikundi cha Janjaweed ambacho kilifanya mauaji makubwa na kumfanya Rais wa Sudan, Omar Al Bashir ambaye sasa anatakiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai kuhusu kufanya uhalifu dhidi ya binadamu.”

Alifafanua kwamba, hakusema kama Serikali inatumia Janjaweed, bali alizungumzia namna Al Bashir alivyotumia wapiganaji hao kufanya uhalifu badala ya jeshi.
Hali hiyo ilizidi kuzua mvutano kati ya kiti cha Spika na Mbilinyi uliodumu kwa dakika tatu, huku Lissu naye akitaka apewe nafasi atoe hoja yake.

Baadaye Mabumba alitumia busara na kuamua kumalizia suala hilo kwa kumtaka Mbilinyi aendelee kuchangia na mbunge huyo wa Mbeya akiendelea kuzungumzia zaidi hilo, alitaka Bunge liunde tume ya uchunguzi kwa sababu hana imani na Serikali kuunda tume kuchunguza ukatili huo.

Baada ya Mbilinyi kumaliza, Mabumba alimtaka Lissu atoe dukuduku lake na aliposimama alimpinga Mwenyekiti huyo wa Bunge kwa maelezo kwamba alitumia kifungu kisicho sahihi kumwamuru Mbilinyi atoe maelezo ya kuthibitisha au kufuta kauli. Hata hivyo, alimtaka akae chini akisema: “Usitafute umaarufu hapa.”

Baadaye alisimama Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Stella Manyanya ambaye alikituhumu Chadema kwa kuchochea mgomo huku akidai kwamba kilihusika kumteka na kumjeruhi Dk Ulimboka.

Mbunge wa Ubungo (Chadema),  alikuja juu baada ya kauli hiyo akimtaka Mwenyekiti amtake Manyanya kuthibitisha au kufuta kauli yake. Badala yake, Mabumba alimtaka Mnyika kuthibitisha kwamba chama hicho hakihusiki.

Mnyika alisema Chadema hakihusiki na suala hilo na kueleza kwamba ripoti ya Kamati ya Bunge iliyoundwa kuchunguza mgogoro wa madaktari na Serikali inathibitisha hivyo, akitaka iwasilishwe bungeni na isomwe.

Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba alisema Chadema kinaunga mkono mgomo wa madaktari akirejea hotuba ya upinzani bungeni iliyotolewa jana ikisema inawaomba wananchi kwa kushirikiana na madaktari kuiunga mkono Chadema kuishinikiza Serikali hadi wapate haki zao.

Manyanya alisimama tena na kudai kwamba hata waliomteka daktari huyo walikuwa wamevaa magwanda ambayo yanatumiwa na makada wa Chadema kauli ambayo iliibua mzozo huku wabunge wengi wa Chadema wakisimama kutaka kuzungumza.

Mwenyekiti Mabumba alilazimika kutumia dakika kadhaa kuwataka wabunge watulie na wakae chini lakini Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali alikataa kutii amri hiyo akitaka kuzungumza hali ambayo ilimfanya Mabumba kuamuru atolewe nje ya eneo la Bunge na kumtaka Manyanya aendelee kuzungumza.

Muhimbili utata mtupu
Wakati uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ukisema huduma katika hospitali hiyo zimerejea katika hali ya kawaida baada ya madaktari kurejea kazini jana, madaktari bingwa wa hospitali hiyo nao wametangaza kuanza mgomo.

Taarifa iliyotolewa jana na msemaji wa uongozi wa Muhimbili, Aminiel  Aligaesha imesema wagonjwa wote waliolazwa wodini jana walihudumiwa na baadhi ya kliniki za huduma ya upasuaji zilifanyika na kuongeza: “Hata hivyo, upasuaji haukufanyika kwani hakukuwa na orodha ya wagonjwa waliopangwa kufanyiwa upasuaji.”

Lakini wakati uongozi wa Muhimbili ukisema hivyo, madaktari bingwa walikutana jana katika hospitali hiyo na kutangaza kuanza mgomo. Akizungumza muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkutano wao uliofanyika katika hospitali hiyo, msemaji wao Dk Catherine Mng’ongo alisema:
“Sisi madaktari bingwa kufanya kazi bila Interns haiwezekani. Tungeanza kufukuzwa sisi kwanza. Kuanzia sasa hatutafanya kazi hadi hapo Serikali itakapokubali kuwarejesha wote kazini na kufungua meza ya majadiliano yenye nia ya dhati ya kumaliza mgogoro.”
Dk Mng'ong'o alisema zaidi ya madaktari 200, waliokuwa kwenye mafunzo ya vitendo Muhimbili na Taasisi ya Mifupa (Moi) wamepatiwa barua za kufukuzwa kazi na idadi yao nchi nzima inafikia 300.

Tamko la Rais Kikwete

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania , Dk Godbles Charles ameeleza kushangazwa na kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwa Serikali haihusiki katika sakata hilo na akidai ameingilia kazi ya tume iliyoundwa na Polisi kuchunguza tukio hilo.
“Je, ni sahihi kwa Rais kutamka waziwazi kuwa Serikali yake haihusiki kwa namna yoyote ile hata kabla ya ripoti ya uchunguzi?” alihoji Dk Charles.
Habari zilizopatikana jana zilieleza kuwa hali ya Dk Ulimboka inaendelea vizuri anakotibiwa Afrika ya Kusini.
Hospitali nyingine
Madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC wamekubaliana na kuendelea na mgomo wakisubiri uamuzi wa mkutano mkubwa wa madaktari utakaofanyika leo.
Jumamosi iliyopita, uongozi wa KCMC uliwatimua madaktari zaidi ya 80 walioko kwenye mafunzo kwa vitendo na kuwataka wasionekane katika eneo la hospitali wala kukusanyika hapo.

Uongozi wa Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru, umelazimika kuitisha kikao cha pamoja na madaktari wa hospitali hiyo kwa lengo la kuwasihi waachane na mgomo.

Vyanzo vya habari hospitalini hapo, vilidai ya kwamba katika kikao hicho uongozi wa hospitali hiyo chini ya Mganga Mkuu Mfawidhi, ulilazimika kuitisha kikao siku moja baada ya tukio la Dk Ulimboka na kuwaangukia madaktari hao waachane na mgomo.

Huko Mbeya, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Mbeya, Dk Eliuter Samky amesema utoaji huduma kwa wagonjwa siyo wa kuridhisha  kutokana na kuathirika kwa kiasi kikubwa kwa baadhi ya sekta muhimu.

Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, Samky alisema mgomo huo umesababisha kuzorota kwa huduma kwa wagonjwa licha ya kusitisha huduma nyingine za kawaida na kubaki kuendelea kutoa huduma za dharura.

Habari hii imeandikwa na Leon Bahati, Geofrey Nyang’oro Aidan Mhando,Victoria Mhagama, Godfrey Kahango, Mbeya, Daniel Mjema, Moses Mashalla, Arusha.

Bolt beaten again! Jamaican rival Blake stuns Usain for second time in three days

Written By Koka Albert on Monday, July 2, 2012 | 1:02 PM

Usain Bolt was beaten for the second time in three days by training partner Yohan Blake, this time surrendering his supremacy in the 200metres.

The Jamaican world record holder and Olympic champion was edged out by his rival in their nation's trials for this summer's Games in London. Blake came home in 19.80, 0.03seconds ahead of Bolt. 

In a result that can no longer be considered a surprise, Blake started edging into the lead near the turn, then burst past Bolt for the narrow victory.
Come back here: Usain Bolt congratulates Yohan Blake after his 200m triumph
Come back here: Usain Bolt congratulates Yohan Blake after his 200m triumph at the Jamaican Olympic Trials

The win came two days after Blake, the reigning world 100 champion, beat Bolt in the 100 by running a 9.75. 

If everything goes to form, their next meeting will be at the London Olympics. 
'I can never be discouraged,' Bolt said. 'I'm never worried until my coach gets worried, and my coach isn't worried, so I'm OK.'
Flat out: Bolt received treatment on the track after the 200m final
Flat out: Bolt had time to reflect on his defeat as he received treatment on the track after the 200m final

Glen Mills, who coaches both runners, said: 'Usain, he has the experience, the ability, he has been there already. He might be a little off at the moment, but I'm sure when the time of delivery comes around, he'll be on top of his game.'

When asked if he was carrying an injury or was holding back, Bolt said: 'I don't want to get into that.
'I was just working (the leg) around for a few moments to get myself back together. I'm not far off. I can get it done.'
Bolt added: 'I was very sad with my turn, it was awful, but I've been working more on the 100 meters.
'I can't blame it on that, though. Just have to get my things together and get it done.'
Showdown: Yohan Blake (right) and Usain Bolt (left)
Treat in store: Blake (right) and Bolt (left) will renew their rivalry at the London Olympics in under a month
Dip for the line: Bolt tries to edge in front but is beaten by his rival
Dip for the line: World record holder Bolt desperately tries to edge in front but is beaten by his rival
Blake will be making his first trip to the Olympics, which can be a daunting prospect. After these pair of benchmark victories, he sounded ready for more work, not a celebration. 

'It leaves me to get back into training,' Blake said. 'It's not over. I still have the Olympics to go.'
Like a racecar driver catching a glimpse of something lurking in his rearview mirror, Blake could see Bolt making up ground out of the corner of his eye. The best ones know how to close things out. 
'I felt him on my right-hand side. No need to panic,' Blake said. 'I just stayed focused.'

In the women's 200, Shelly-Ann Fraser-Pryce ran a personal best 22.10 seconds to also complete the 100-200 sweep. She'll be joined by Sherone Simpson and two-time defending Olympic champion Veronica Campbell-Brown.

Who's the daddy now, Mario? After suffering heartache in Euro 2012 final, Balotelli is due to become father

It has been a rollercoaster week even by the standards of Mario Balotelli.
First he scored two stunning goals in the Euro 2012 semi-final against Germany. Then it was heartache in the final against Spain on Sunday.
But now Balotelli has received perhaps the biggest news of all - that he is to become a father.
Down and out: Mario Balotelli reacted angrily to Italy's Euro 2012 defeat
Down and out: Mario Balotelli reacted angrily to Italy's Euro 2012 defeat
The 21-year-old has been told by his pregnant former girlfriend Raffaella Fico that it is his child.
He was told on the eve of the match against Germany when he grabbed a brace to book his country's place in the final. He reportedly told her: 'You gave me the best news of the world.'

And Italian model Raffaella has claimed that the pair are patching up their relationship.
She said: 'Mario and I are rebuilding our relationship. He never stopped loving me. Those who think I've wanted to trap the rich and famous footballer will have to think again. 

'Last Christmas, he told me: "Let's get married and make a son" and I accepted. Now I'm waiting for Mario to discover the sex of the child, although he would prefer a boy, and to choose the name.'
Meanwhile, AC and Inter Milan have been warned that Balotelli is worth £200million following his star showing at Euro 2012.
Balotelli's? The Italian model, who split up with the striker two months ago, was at a charity event when she showed off her bump and has reportedly said it is Mario's
Baby bump: Mario Balotelli's ex-girlfriend Raffaella Fico has sparked rumours she's pregnant with his child after showing off her baby bump
 Baby bump: Mario Balotelli's ex-girlfriend Raffaella Fico sparked rumours after showing off her baby bump
As they were: Mario and Raffaella dated for a year until they broke up two months ago
As they were: Mario and Raffaella dated for a year until they broke up two months ago
Balotelli, 21, a self-confessed Milan fan, is a target for the Italian giants but will set any prospective suitor back the eye-watering figure, according to his agent.

The striker could not prevent Italy crashing to a 4-0 Euro 2012 final defeat to Spain on Sunday night but stole the limelight by scoring two superb goals in his national team's 2-1 triumph over Germany in the semi-finals of the tournament in Poland and Ukraine.

'I have always said that Mario Balotelli is one player that could become the strongest in the world,' Balotelli's agent Mino Raiola told Sky Italia. 'He is probably amongst the strongest in Europe.
'How much is he worth? He is worth what the market says, he is one that can make a difference.
'In the actual market I don't think there is a value for him but if I had to give a price I would say he is worth 250million (euros).
Down and out: Mario Balotelli reacted angrily to Italy's Euro 2012 defeat
Down and out: Mario Balotelli reacted angrily to Italy's Euro 2012 defeat
'I say this to give a figure but you would have to ask the City owner (Sheikh Mansour) how much he is worth.'

Raiola added that he could see no immediate return to Italy for Balotelli. 'I'm 200 per cent certain that Mario will not return to Italy at least while I'm his agent.' Balotelli is under contract at the Etihad Stadium until June 2015.

The volatile front-man was reduced to tears in the wake of the Euro 2012 final. He endured a frustrating evening as Spain romped to a historic third successive major international tournament victory.
Firing blanks: Balotelli was unable to prevent Spain from running away with the trophy
Firing blanks: Balotelli was unable to prevent Spain from running away with the trophy
And unfortunately after the match the ugly side of his game came to the fore once more after the striker clashed with members of Italy's backroom staff.

Balotelli had had a splendid tournament until that point, most notably when he blasted Italy into Sunday's showpiece with a stunning double to down Germany.

However at the full-time whistle in Kiev, the Manchester City man made a beeline for the dressing room. He came up against resistance from senior figures and appeared to push one. 

After several minutes, Balotelli could then be seen on his haunches in the centre of the pitch. He later collected his medal but broke down in tears as soon as he returned to the pitch.

Italy coach Cesare Prandelli says his player will emerge stronger from the shattering experience.
'I told Mario that these are experiences you have to deal with and have to accept,' said Prandelli. 'You have to hold your hands up and say the opponents were better, accept defeat.

'But you also have to make sure this helps you going forward and you can grow from the experience. This has happened to a number of players, and will happen again, but this is what sport is all about.'
I'm outta here: Mario stormed off at full-time
                                           I'm outta here: Mario stormed off at full-time
.
Words of sympathy: Italy coach Cesare Prandelli comforted his striker
                Words of sympathy: Italy coach Cesare Prandelli comforted his striker

JK: Hatuhusiki unyama aliofanyiwa Ulimboka

SEMA MADAKTARI WASIOKUBALI MSHAHARA WA SERIKALI WAFUNGASHE VIRAGO
Boniface Meena
WAKATI Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka akiendelea na matibabu Afrika Kusini, Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali haihusiki na kilichomtokea daktari huyo kwa kuwa alikuwa kiungo muhimu katika majadiliano baina ya pande hizo mbili.

Rais Kikwete alisema hayo jana katika hotuba yake ya kila mwezi, ambapo mbali na suala hilo, pia alizungumzia sababu za mgomo wa madaktari na usafirishaji wa wahamiaji haramu.

Dk Ulimboka ambaye alikuwa anaratibu mgomo wa madaktari unaoendelea nchi nzima kutokana na Serikali kushindwa kutimiza madai yao mbalimbali, anatibiwa figo na majereha aliyoyapata katika sehemu mbalimbali za mwili, baada ya kutekwa na watu wasiojulikana, kisha kupigwa, kung'olewa kucha, meno mawili na kutupwa katika Msitu wa Pande, usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita.

Tangu kutokea kwa unyama huo uliofanywa na watu wasiojulikana, baadhi ya wananchi na wanaharakati wamekuwa wakiilaumu Serikali kuwa inahusika na utekaji huo na wengine wakienda mbali zaidi, kuwa watekaji walikuwa wanamlazimisha kueleza nani yuko nyuma ya mgomo wa madaktari.

Rais Kikwete, kama awali alivyosema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, walisema wanatambua kuwa, Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka kuhusu kilichomtokea Dk Ulimboka, lakini yeye ameshangazwa na hisia hizo, kwani haoni sababu ya Serikali kufanya hivyo.

"Dk Ulimboka alikuwa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na madaktari. Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya.  Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam madaktari wanamwamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali," alisema Rais Kikwete.

Alisema Serikali haina sababu ya kumdhuru Dk Ulimboka kwa sababu suala la mgomo, Mahakama Kuu imekwishatoa amri ya kuusitisha, hivyo anayekaidi amri hiyo atakuwa ananunua ugomvi na mhimili huo wa dola, ambao wenyewe una mamlaka ya kumtia adabu.

"Hivi baada ya kufika hapo Serikali iwe na ugomvi na Dk Steven Ulimboka kwa sababu ipi na jambo lipi hata iamue kumdhuru?" alihoji na kuongeza:

"Kama kuna mtu wa Serikali kafanya, itakuwa kwa sababu zake binafsi na siyo za Serikali au kwa kutumwa na Serikali," alisema Rais Kikwete.

Alisema alichofanyiwa Dk Ulimboka kimemsikitisha na kumhuzunisha kwa kuwa ni kitendo cha kinyama na kinyume kabisa na mila na desturi za Tanzania.

Alisema Watanzania hawajazoea mambo hayo na kwamba ameelekeza vyombo vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi wa kina ili ukweli ujulikane.

"Nimesema kuwa ningependa ukweli huo ujulikane mapema ili tuondoe wingu baya la kutiliana shaka na kulaumiana kunakoendelea hivi sasa," alisema.

Alisema anatoa mkono wa pole kwa Dk Ulimboka na kumwombea apone haraka ili aungane na familia yake na Watanzania wenzake katika ujenzi wa taifa.

Rais Kikwete pia alimpongeza Juma Mgaza ambaye alimsaidia Dk Ulimboka kumtoa katika pori alikotupwa na kumpeleka kituo cha polisi kwa moyo wake wa huruma.

Kuhusu mgomo
Kuhusu mgomo unaoendelea Rais Kikwete alisema, kiwango cha mshahara cha Sh3.5 milioni wanachokitaka madaktari Serikali haina uwezo wa kukitoa, hivyo daktari anayeona kuwa hawezi kufanya kazi serikalini bila ya kulipwa mshahara huo, awe huru kuacha kazi na kwenda kwa mwajiri anayeweza kumlipa kiasi hicho.

Rais Kikwete alisema, kwa sasa Serikali haiwezi kuwaahidi kuwa inao uwezo wa kuwalipa mshahara wa kuanzia wa Sh3.5 milioni na posho zote zile, kwani ikifanya hivyo malipo ya daktari anayeanza kazi yatakuwa Sh7.7 milioni kwa mwezi, kitu ambacho haitakiweza.

"Si vyema kutoa ahadi hewa kwa watu tunaowaheshimu na kuwathamini kama walivyo madaktari. Kutokana na ukweli huo basi kama daktari anayeona kuwa hawezi kufanya kazi serikalini bila ya kulipwa mshahara huo awe huru kuacha. Nasi tutamtakia kila la heri,"alisema Rais Kikwete.

Rais Kikwete alisema, madaktari hawana sababu ya kugoma ili washinikize kulipwa mshahara huo kwani uwezo haupo.

"Kwa nini upate usumbufu wa kuachishwa kazi na kutakiwa kuondoka kwenye nyumba ya Serikali ndani ya saa 24. Jiepushe na yote hayo kwa kujiondoa mwenyewe," alisema.

Alisema mamlaka za ajira zimeanza kuchukua hatua hizo kwa wale wanaokwenda kinyume na sheria za kazi na wataendelea kufanya hivyo kwa wote wanaoendelea kugoma.

Alisema anajua baada ya hatua hizo kuchukuliwa kuna manun’guniko ya kuonewa yatajitokeza, lakini ni bora kufanya hivyo ili ijulikane Serikali haina daktari.

"Mlitegemea mwajiri afanyeje? Ni bora kufanya hivyo ili ajue hana daktari aweze kufanya utaratibu wa kuziba hilo pengo na huyo anayekuja awe na mahali pa kuishi."

Kutokana na hali hiyo amewasihi madaktari kuacha mgomo na kurejea kazini, kwani Watanzania wanateseka na kupoteza maisha.

Sababu za mgomo
Rais Kikwete alisema kwamba, kuna masuala matatu ambayo yamekuwa na mwafaka kwa kiasi fulani na kutoafikiana kwa baadhi ya mambo kati ya madaktari na Serikali.

Alisema suala la kwanza ni suala la kufanya kazi katika mazingira hatarishi ambalo Serikali imekubali hoja ya kuchukua hatua ya kuwalinda madaktari wanaofanya kazi katika mazingira hatarishi.

Pia alisema Serikali imeeleza dhamira ya kurudisha posho ya mazingira hatarishi kwa watumishi wa umma wanaostahili na utekelezaji wake utafanyika baada ya uchambuzi wa kina wa kubainisha mazingira hatarishi ni yapi, viwango stahiki viwe vipi na nani hasa wahusike.

Rais Kikwete alisema kuwa, madaktari wamekataa suala hilo la kufanya uchambuzi, wanataka kiwango kiwe kama wanavyotaka wao, yaani asilimia 30 ya mshahara na kianze mara moja.

Alisema suala la pili ambalo wamekubaliana nusu nusu ni kuhusu nyumba za kuishi ambalo Serikali imekiri wajibu wake wa kuwapatia nyumba za kuishi.

Rais Kikwete aliongeza kwamba, kwa maeneo ambayo madaktari wanalipwa posho ya pango, Serikali imesema waajiri wataendelea kufanya hivyo kwa mujibu wa taratibu zilizopo kwa watumishi wa umma wenye stahili ya kupewa nyumba.

Alisema jambo hilo limekataliwa na madaktari na kutaka lazima walipwe asilimia 30 ya mshahara kama posho ya nyumba.

Rais Kikwete alisisitiza kwamba, Serikali kwa upande wake imeona vigumu kufanya hivyo na kuwasihi wakubali wanayotendewa kama wafanyakazi wengine wote wa umma.

Alisema suala lingine ambalo lilikuwa na makubaliano ya nusu nusu ni kuhusu posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu na pande zote mbili ziliafikiana kuwa yapo baadhi ya maeneo nchini yanayo mazingira magumu kwa watumishi wa umma, hivyo hatua zichukuliwe kuwasaidia watumishi hao.

Kuhusu posho, alisema Serikali imekubali kuwapo posho ya aina hiyo ila itatekelezwa baada ya kufanya uchambuzi wa kuainisha mazingira husika, kutambua watumishi waliopo na gharama zake.

Alisema madaktari hawajakubali kusubiri zoezi la uchambuzi lifanyike, wanataka Serikali ilipe posho hiyo sasa.

"Tofauti hapa si posho hiyo kuwapo, bali ni rai ya Serikali ya kubaini maeneo yenyewe na kupanga aina ya hatua na viwango vya posho kulingana na mazingira halisi ya maeneo. Madaktari hawaoni haja ya kufanya hayo," alisema.

Alisema kuna mambo mawili ambayo hayakuwa na mwafaka kabisa kati ya pande hizo mbili na la kwanza ni posho ya kuitwa kazini (on call allowance).

Rais Kikwete alisema, Serikali ilishaongeza posho hizo tangu Februari, 2012 posho iliongezwa kutoka Sh10,000 hadi Sh25,000 kwa daktari bingwa, Sh20,000 kwa dakari mwenye usajili wa kudumu na Sh15,000 kwa madaktari waliohitimu ambao wapo katika kipindi cha mafunzo kazini (Interns).

Alisema hata hivyo, madaktari kwa upande wao hawakukubali uamuzi huo wa Serikali na kusisitiza walipwe asilimia 10 ya mshahara.

Rais Kikwete alisema ugumu wa kukubali pendekezo la madakari ni kuwa sharti la malipo haya ni mtu kuitwa kazini na kwamba ukitaka ilipwe kiwango cha mshahara ina maana kuwa hata kama daktari hakupangwa kuitwa au alipangwa na hakutokea aendelee kulipwa.

Alisema jambo la pili ambalo mwafaka haukufikiwa baina ya Serikali na madaktari ni kuhusu mshahara wa kuanzia kazi wa daktari ambao madaktari wanataka uwe Sh3.5 milioni wakati Serikali inasema kiasi hicho hatukiwezi.

Alisema Serikali imeeleza utayari wake wa kuongeza mshahara kwa kati ya asilimia 15 mpaka 20 kama ambavyo itafanya kwa watumishi wote wa umma katika mwaka huu wa fedha.

Rais Kikwete alisema, kwa kiwango cha sasa cha mshahara wao, daktari ataanzia kati ya Sh1.1 milioni na Sh1.2 milioni kutegemea kiwango kipi hatimaye kitaamuliwa.

"Madaktari wamekataa katakata na wameng’ang’ania Sh3.5 milioni," alisema.

Alisema ni muhimu madaktari wakatambua kuwa wagonjwa wanateseka na wengine kupoteza maisha kwa mgomo usiokuwa halali kisheria ambao pia haustahili kuwapo hata kwa mujibu wa maadili ya udaktari.

Alisema viongozi wa MAT na wenzao wanawaingiza madaktari katika mgogoro na mahakama na waajiri wao isivyostahili.

Rais Kikwete alisema ni vyema viongozi wa madaktari na madaktari wakatambua kuwa wanashiriki katika mgomo usiokuwa halali ambao pia kiongozi wao mkuu amekana mahakamani kuwa hahusiki nao.

Rais Kikwete alisema madaktari lazima watambue pia kwamba ajira zao wanaziweka hatarini kwani mfanyakazi hana kinga ya kutofukuzwa kazi na mwajiri kwa kushiriki mgomo unaokubalika kisheria.

"Huu siyo. Watapoteza ajira, hawana pa kukimbilia, hawana cha kuwalinda. Kwa madaktari interns, wanahatarisha maisha yao, kwani hawatapata cheti cha kudumu wakishiriki mgomo usiokuwa halali. Lazima watafakari kwa hayo wafanyayo," alisema.

Hoja za madaktari
Rais Kikwete alisema katika mambo 12 ambayo madaktari waliyawasilisha pande zote mbili zilifikia mwafaka na kukubaliana kwa pamoja kwa mambo saba.

Alitaja la kwanza ni kuhusu usafiri wa kwenda na kurudi kazini ambalo limeshashughulikiwa.

Alisema jambo la pili, ni madaktari kupatiwa Green Card za Bima ya Afya ambalo Serikali na Wizara ya Afya zimechukua hatua za utekelezaji wake.

Jambo la tatu, alilitaja Rais Kikwete kuwa ni hatua za kinidhamu kuchukuliwa dhidi ya Watendaji Wakuu wa Wizara ya Afya ambalo tayari Serikali imechukua hatua.

"Uongozi wa juu wa wizara umebadilishwa na sasa kuna uongozi mpya. Lakini, jambo la kustaajabisha hata Waziri mpya wa Afya alipowataka waonane kuzungumzia hoja walikataa kumuona.  Kwanza walisema hawaoni sababu kwa vile wameyazungumza na kamati yake kwa miezi mitatu bila ya mafanikio," alisema.

Rais Kikwete alisema kuwa, jambo la nne walilokubaliana ni viongozi kuwalazimisha kupewa rufaa ya kutibiwa nje suala ambalo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amewaeleza madaktari wazingatie maadili ya kazi zao na kukataa kutoa rufaa kwa mtu asiyestahili awe kiongozi au asiwe kiongozi.

Alisema jambo la tano ambalo pande zote mbili zilikubaliana ni kuhusu madaktari waliofukuzwa.

"Hawa ni wale Interns waliokuwa wamerudishwa wizarani kutoka Muhimbili na kupangiwa hospitali za Temeke, Ilala, Mwananyamala na Lugalo. Hili ni jambo ambalo lilikuwa limemalizika kitambo na wote walikuwa wamerudi Muhimbili," alisema.

Rais Kikwete alisema jambo la sita ni kuhusu mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa na madaktari kuhusu kuboresha huduma ya afya ambalo Serikali imeliafiki.

Rais Kikwete alisema jambo la saba, ambalo pande zote walilokubaliana ni kuhusu kuongeza posho ya uchunguzi wa maiti.

Alisema jambo hilo jipya halikuwepo mwazoni, hata hivyo, Serikali imelikubali na posho hiyo imeongezwa kutoka Sh 10,000 hadi kufikia Sh100,000 kwa daktari na Sh50,000 kwa wasaidizi wake,” alisema.
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger