BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

TANZANIA YAPATA SHUJAA MPYA

Written By Koka Albert on Monday, October 15, 2012 | 1:30 AM


 Mh Peter Kallaghe akiwa katika picha ya pamoja na timu nzima ya TWENDE PAMOJA. Kutoka kushoto Lee Patterson, Mike Knox (Director) Wilfred Moshi, Mary Iannarelli, Fiona Macpherson na Veronica Avinou
 Mike Knox mwanzilishi wa Twende Pamoja akifanya mazungumzo na Urban Pulse
 Mwanzilishi wa Twende Pamoja Mike Knox akila pozi na Frank Eyembe wa Urban Pulse Edinburgh, Scotland
 Wilfred Moshi akipeperusha bendera ya Tanzania kileleni Mlima Everest
Wilfred Moshi safarini kuelekea kileleni.Picha zote hisani ya Wilfred Moshi na Urban Pulse
Imeandikwa na Freddy Macha kwa ushirikiano na Urban Pulse

 Kwa mara ya kwanza kabisa katika historia ya nchi yetu kijana Wilfred Moshi, Mbongo wa kawaida tu (anayefanya kazi ya upagazi kuwahudumia watalii wanaopanda mlima Kilimanjaro), ameweka rekodi mpya ya kuwa Mtanzania wa kwanza kupanda Everest - mlima mrefu kushinda yote duniani.
 Hivi karibuni, Moshi,   alialikwa majuma matano nchini Uingereza kutembelea shule mbalimbali za Scotland akakutana na takribani wanafunzi 5,000 .
 
Wanafunzi walitaka kufahamu namna alivyopanda mlima Everest wenye mita 8,848 (futi 29, 029). Mlima huu mgumu kuukwea kuliko yote ulimwenguni umewahi kupandwa na na watu 4,000 toka ulipoanza kufikiwa kileleni na Edmund Hillary na Sherpa Tenzig Norgay mwaka 1953. Kati ya hao 200 walifariki. Mwaka huu wanne wameshafariki wakiijaribu shughuli hii inayochukua  miezi miwili na kugharimu Dola 100,000 (Shilingi milion 157,500,000) Linganisha na mlima Kilimanjaro unaodai  siku tano na gharama (ikiwepo vifaa husika) Dola 2,000 (Shilingi milioni 3, 161).
Wilfred Moshi ni Mtanzania wa kwanza na Mwafrika wa tatu kufikia kilele cha kitendawili hiki Mei 19 2012 (kilichoitwa “Chomolungma” na wenyeji kabla ya kubatizwa jina la Everest na Waingereza enzi za ukoloni)  
Wilfred aliyezaliwa mwaka 1979 na kumaliza kidato cha sita shule ya Kilimanjaro Boys, amekuwa akipanda mlima Kilimanjaro tangu angali bado shuleni na miaka 19.
Mara baada ya kuwasili Edinburgh, Scotland alikaribishwa bungeni akakutana na Waziri wa Sheria mheshimiwa Kenneth MacAskill na viongozi wengine. Safari ilikirimiwa na shirika la “Twende Pamoja” lililoanzishwa na Mike Knox miaka 30 iliyopita. “Twende Pamoja” imejenga ushirikiano kati ya wanafunzi wa Scotland na shule 34  za Kitanzania. Ni moja  ya mashirika, watu binafsi  na wafadhili mbalimbali ulimwenguni waliochangia fedha za kumwezesha Moshi kupanda mlima Everest.
Balozi wetu Uingereza, Mheshimiwa Peter Kallaghe vile vile alisafiri toka London kumtembelea Wilfred Moshi na kumpa heko. Umbali wa London had Scotland ni kama Dar es Salaam hadi Kigoma!
Kwanini Moshi anahusudu kupanda milima?
Ukweli sisi bado hatuoni umaana (au umuhimu) wa kupanda milima. Anasema lengo lake lilikuwa kutimiza ndoto ya Mtanzania wa kwanza kupanda Everest. Pili, upandaji milima ni moja ya njia zinazoweza kusaidia kujenga jamii kwa misaada na fadhila za mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO). Tujiulize vipi alisaidiwa na watu wengi namna hiyo kuchangia fedha takikana? Tatu, Moshi amethibitisha ukiwa na moyo na jitihada unaweza kufanya lolote. Ushujaa na ushupavu wake utasaidia kuwahamasisha Watanzania kuwa ukitaka kufanya jambo lolote lile unaweza ili mradi uwe na moyo na nidhamu.
Mpanda milima mashuhuri, Mike Hamill, aliyeshakwea milima yote  mikubwa saba duniani anasema katika kitabu chake kipya (“Climbing Seven Summits”) wapanda milima ni watu wenye moyo wa kufikia malengo na kufanikiwa katika maisha yao.
 Akiwa Uingereza Moshi alipanda mlima wa Ben Nevis  mrefu kuzidi  nchi hii-  wenye mita 1,344 (futi  4, 409). Baada ya kuimudu milima mitatu sasa , Wilfred Moshi ameazimia kupanda milima  katika mabara yote 7 duniani. Anasema amebakisha milima mitano: Aconcagua ( Marekani ya Kusini ), Kosciuszko (Australia), Vinson Massif ( Antarctica) McKinley(Alaska) na  Elbrus(Urusi).
Mungu ambariki Mtanzania huyu mwenye jazba na hamasa anayetuletea sifa.

RAIS JAKAYA KIKWETE AZIMA MWENGE MKOANI SHINYANGA



Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi cheti na kikombe Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Ms Margareth Nyalile ambaye Manispaa yake ilishinda nafasi ya kwanza katika kufanikisha mbio za mwenge mwaka huu. Sherehe za kuzima mwenge zilifanyika mjini Shinyanga tarehe 14.10.2012
Rais Jakaya Kikwete akipokea mwenge kutoka kwa kiongozi wa mbio za mwenge wa mwaka 2012 Captain Honest Mwanossa wakati wa sherehe za kuzima mwenge zilizofanyika katika uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga tarehe 14.10.2012. wa pili kutoka kushoto ni Waziri wa habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mkukangara.

Kocha Yanga ataka wabadilike

Written By Koka Albert on Friday, October 12, 2012 | 2:42 AM

KOCHA wa Yanga, Enerst Brandts amewataka wachezaji wake Nurdin Bakari na Juma Seif kubadilika huku akifunga milango kwa beki Shadrack Nsajigwa.

Brandts alisema haridhishwi na kiwango cha Nurdin na Seif Kijiko kwa sasa na kuweka bayana kwamba Nsajigwa hana nafasi kwenye kikosi chake.
Wanatakiwa kubadili uchezaji wao ili wapate nafasi  kwenye kikosi cha kwanza,รฎalisema kocha huyo.

Kuhusu hatma ya beki Nsajigwa รซFusoรญ aliachwa kwenye safari ya Kanda ya Ziwa, Brandts alisema sijaona kiwango chake, sijaona umuhimu wa  yeye kuja huku, hapa nipo na wachezaji 20.

Tangu kuanza msimu huu Nsajigwa ameshindwa kupata namba ya kudumu kwenye kikosi cha Yanga baada ya kuwajiliwa kwa Mbuyu Twite na Juma Abdul.

Hivi karibuni Nsajigwa alikaririwa na vyombo vya habari akisema Yanga imesajili vijana wengi wazuri ndio maana amekosa namba kwenye kikosi hicho.
Nimewapisha vijana waweze kucheza kwani wanaonyesha uwezo mzuri, naamini kwa kikosi tulichonacho tutafanya vizuri zaidi kwenye ligi,รฎ alisema  Nsajigwa.

Mambo ya Denilson akiwa na sao paulo

JOB OPPORTUNITIES FOR RECENT GRADUANTS: ACCESS BANK EXCITING CAREER OPPORTUNITIES IN MWANZA

Written By Koka Albert on Tuesday, September 18, 2012 | 1:25 AM

AccessBank Tanzania is a full commercial bank providing micro, small and medium sized enterprises (MSMEs) with a broad range of appropriate financial services. Established in 2007, the bank is owned by a multinational shareholder group and member of an emerging global network of commercial microfinance banks (The "Access Group") with headquarters in Berlin/Germany.
As one of the fastest-growing bank in Tanzania, Accessbank is now opening soon a branch in Mwanza City, we offer excellent long-term career development opportunities for recent and fresh graduates and young professionals. In order to support our dynamic expansion process, we are looking forward to recruit a number of self-motivated and enthusiastic individuals to join our teams in our new branches in Mwanza.
FIELD OFFICERS
       Responsibilities:
  • Marketing and attracting potential business loan clients
  • Conducting on-site and risk assessment of loan applicants
  • Loan monitoring and recovery
Interested candidates must be ready to work extensively outside the office. If you prefer desk-based job, please look out for other vacancies advertised by the Bank from time to time.
       Qualifications and Experience:
  • Education: Graduate or Diploma holder
  • Experience: No prior work experience required
CLIENT ADVISOR
       Responsibilities:
  • Marketing and attracting potential clients for banking accounts and saving products
  • Opening closing, and maintaining different types of customers accounts
  • Dealing with cheques and money transfers
       Qualifications and Experince:
  • Education: Graduate or Diploma holder
  • Experince: No prior work experience required
CASHIERS:
       Responsibilities:
  • Cash deposit and withdrawal transactions (local and foraign currency)
  • Management and full responsibility of the daily cash box
       Qualifications and Experience:
  • Education: Diploma Holder or good form Six
  • Experince: No prior work experience required
Please send your CV ONLY by email to career@accessbank.co.tz DO NOT send CV more than once. Please refrain from sending any attachment via the website. Certificates and other relevant documents will only be required during the interview. The deadline for sending CVs is 1st October, 2012.

Waziri Nchimbi atimuliwa na waandishi wa habari

Written By Koka Albert on Tuesday, September 11, 2012 | 6:52 AM

WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi, amekumbana na fadhaa ambayo haikutarajia wakati alipotimuliwa katika maandamano ya waandishi wa habari ya kupinga mauaji ya mwandishi mwenzao wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, David Mwangosi, wakati alipozuka bila mwaliko.

Huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe tofauti, waandishi waliandamana kuanzia kwenye ofisi za Channel Ten katikati ya jiji la Dar es Salaam na kutembea hadi katika viwanja vya Jangawani lakini walipofika mwisho wa maandamano yao walipigwa na butwaa baada ya kumkuta Waziri Nchimbi akiwa wa kwanza kufika katika eneo hilo tayari kupokea maandamano.

Wakati Nchimbi akijiandaa kuanza kuzungumza mbele ya wanahabari, upinzani mkali ukazuka kwa waandishi dhidi ya kiongozi huyo wa serikali wakitaka aondoke mahala hapo kwani maandamano hayo yalikuwa hayamuhusu.

"Atokee.... aondokee.... hatumtakiiii.... nani kamleta hapa?" yalikuwa ni baadhi ya maneo yaliyokuwa wakitolewa kwa sauti kubwa kupinga uwapo wa waziri Nchimbi mahala hapo.

Huku akizomewa, Waziri Nchimbi alijaribu kuvumilia aibu hiyo kwa takriban dakika tano huku pengine akitumai kwamba watamruhusu kuzungumza kilichompeleka mahala hapo.

Mwandishi wa habari mkongwe, ambaye pia ni mwanasheria, Nyaronyo Kicheere, alisogea mbele ya umati wa waandishi na kusimama jirani na alipokuwapo waziri Nchimbi na kusema: "Tumeambiwa tunakuja hapa kwa ajili ya mkutano wa waandishi wa habari na utapokewa na jukwaa la wahariri, inakuwaje tupokewe na mtu mwingine. Hatumhitaji mtu mwingine hapa, aondoke."

Baada ya kauli hiyo, waziri Nchimbi aliondoka mahala hapo na kuzua shangwe kubwa kwa waandishi ambao pia walimsindikiza kwa kumzomea mpaka alipoingia katika gari lake la wizara. Hakuja na gari lake la waziri.

Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari walizungumza na kukemea mauaji hayo na bila ya kuuma-uma maneno walisema kwamba Mwangosi aliuawa kwa kulipuliwa na polisi na kwamba waliohusika wote wachukuliwe hatua za kisheria.

"Waandishi na wafanyakazi wengine wanalipa kodi ilipolisi wapate magwanda, wapate bunduki, wapate mabuti na wanalipwa ili walinde raia na sio kuua raia, vitendo kama hivi havikubaliki," alisema Jesse Kwayu, mhariri mkuu wa gazeti la NIPASHE.

Mwandishi mkongwe, Masoud Sanani, aliongeza: "Waarabu wanasema 'wal kiswaswa haq' yaani 'kisasi ni haki', lakini sisi kwa busara tunasema kwamba hatuna kisasi ila tunataka mambo haya yawe mwisho, waandishi waachwe wafanye kazi zao kama askari wanavyoachwa wafanye kazi zao."

"Tumeshasikia askari akitingishwa kidogo, mtu anashitakiwa kwa kumzuia askari kufanya kazi yake, tunataka waandishi nao waachwe wafanye kazi yao," alisema.

Waandishi walitaka familia ya marehemu Mwangosi ilelewe na watoto wasomeshwe mpaka watakapofikia.

Miongoni mwa mabango yaliyokuwapo katika maandamano hayo yalisomeka: "Bunduki na mabomu hayatazuia kalamu zetu kuandika ukweli," "Hatuogopi vitu vizito wala vitu vya

IBADA YA MAZISHI YA MAREHEMU DAUDI MWANGOSI YAFANYIKA ITETE, TUKUYU MKOANI MBEYA

Written By Koka Albert on Tuesday, September 4, 2012 | 5:59 PM

 
Mke wa Marehemu Daudi Mwangosi akilia kwa uchungu.
 
Maelfu ya  watu wakiongezeka kuja katika Mazishi ya mwandishi wa habari wa Channel 10 Daudi Mwangosi muda huu.
  
Mheshimiwa Mark Mwandosya ambaye ni Waziri ofisi ya Rais na pia Mbunge wa Rungwe Mashariki akitoa salamu kwa niaba ya Serikali.
 
Watu wakiwa wengi na wenye utulivu wakisikiliza watu mbalimbali wakitoa salam zao kwa ndugu wa Marehemu.
 Mjane wa Marehemu Daudi Mwangosi aliyejishika, akiwa na uchungu muda huu.
Ibada ikiwa inakaribia kuanza.
 Ibada ya mazishi ndio imeanza muda huu.
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa wenye majonzi makubwa.
Waandishi wa Habari wakiwa katika msiba wa kwanza kutoka kulia ni Ndugu Joseph Mwaisango ambaye ni mwandishi mkuu wa Mbeya yetu Blog, Rais wa UTPC Keny Simabaya, pamoja na Felix Mwakyembe .

R.I.P MWANGOSI
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger