BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

Ufafanuzi wa NECTA haukubaliki

Written By Koka Albert on Wednesday, March 21, 2012 | 7:16 AM

Dk. Joyce Ndalichako

KATIBU Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk. Joyce Ndalichako, kwa mara nyingine ametetea uamuzi wa baraza lake kuwafutia matokeo ya mtihani wa kidato cha IV baadhi ya wanafunzi. Nimesikia kwa umakini utetezi alioutoa.

Kimsingi Dk. Ndalichako ameeleza mambo matatu makubwa kuhalalisha kile alichoita, “kukithiri kwa vitendo vya udanganyifu katika vyumba vya mitihani.”

Kwanza, Dk. Ndalichako amesema baraza lake limelazimika kuchukua hatua hiyo ngumu baada ya baadhi ya walimu na wasimamizi wa mitihani kushiriki katika “uchafuzi wa mitihani.”

Pili, amasema baadhi ya wanafunzi walikutwa na majibu ya mitihani kupitia simu zao za mkononi.
Tatu, amesema wasimamizi walikamata vikaratasi ambavyo wanafunzi walikuwa wanavitumia “kupasiana” majibu.

Lakini kabla ya Necta kubebesha tuhuma wasimamizi wa mitihani sharti ieleze kama katika mtihani huu, ilibadilisha mfumo wake wa kuteua wasimamizi waaminifu kama wanavyofanya siku zote.
Hii ni kwa sababu, wengi wa wasimamizi ni wale wale waliowahi kutaka kutunikiwa tuzo kutokana na kulipatia sifa nzuri ya “usimamizi wenye tija,” baraza lake.

http://www.mwanahalisi.co.tz/ufafanuzi_wa_necta_haukubaliki

Wizi wa kutisha Chuo Kikuu Huria

CHUO Kikuu Huria Tanzania (OUT) kimeingia katika kashfa nzito ya wizi wa mamilioni ya shilingi, imefahamika

Fedha zinazotajwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha ni zaidi ya Sh. 800 milioni. Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa kati ya kiasi hicho, Sh. 500 milioni ziliibwa katika idara ya malipo ya mishahara iliyokuwa ikiongozwa na Angelus Mlekaria.

Fedha kiasi kingine zaidi ya Sh. 300 milioni imeelezwa kuwa zimepotea mikononi mwa James Rweikiza, aliyekuwa mhasibu na mkuu wa kitego cha mikopo ya wanafunzi wanaojiunga na chuo hicho.

In Pictures: Mourinho, Guardiola, Wenger & the 10 managers leading football's rich list

Written By Koka Albert on Tuesday, March 20, 2012 | 6:52 AM

The latest round of football rich lists have been published, with a number of familiar faces from the world game topping the charts for financial rewards.

France Football have highlighted the managers who have made the most over the last year in combined wages and sponsorship deals, with two Spanish-based managers and another plying his trade in France making up the top three.


The following list, which sees every boss surpass the £5m mark for their earnings in the last 12 months, includes a few surprise inclusions - but do you think the lucky 10 are deserving of their astronomical loots?

If not, let us know which managers are more worthy of the biggest bucks that the game has to offer in our comments section below.

1. Jose Mourinho, Real Madrid | £12.3m


2. Carlo Ancelotti, PSG | £11.2m


3. Pep Guardiola, Barcelona | £8m


4. Arsene Wenger, Arsenal | £7.5m


=5. Fabio Capello, Ex-England | £7.1m


=5. Guus Hiddink, Anzhi | £7.1m


7. Sir Alex Ferguson, Manchester United | £6.7m


8. Dick Advocaat, Russia | £5.8m


9. Jose Camacho, China | £5.1m


10. Roberto Mancini, Man City | £5m

In Pictures: Lionel Messi, Cristiano Ronaldo & the 10 players leading football's rich list

The following list, which sees every player comfortably beat the £10m barrier for their earnings in the last 12 months, includes a few surprise inclusions along with some heavyweights of the game both on and off the pitch.




1. Lionel Messi, Barcelona | £27.5m

2. David Beckham | £26.2m

3. Cristiano Ronaldo, Real Madrid | £24.3m

4. Samuel Eto'o, Anzhi | £19.4m

5. Wayne Rooney, Man Utd | £17.2m


6. Sergio Aguero, Man City | £15.7m


7. Yaya Toure, Man City | £14.7m


8. Fernando Torres, Chelsea | £13.9m

9. Kaka, Real Madrid | £12.9m

10. Philipp Lahm, Bayern Munich | £11.9m



HAVE YOUR SAY
What do you make of the highest-earning players and the money they have made over the last 12 months? Do you think the lucky 10 are deserving of their astronomical loots? If not, let us know which players are more worthy of the biggest bucks that the game has to offer in our comments section below.

**************WELCOME TO AN OPEN DEBATE***************

Who do you think should become the PFA player of the year,,,in English Barclays Premier League?

GetInformedTz is keen to find out what is your response dear viewers

Proposed Names

  1. Wayne Rooney
  2. Robin Van Persie\
  3. David Silva
  4. Vicent Company
  5. Joe Hart
  6. Mario Ballotel
  7. Alexander Song
  8. Wojciech Szczensy
  9. Laurent Koscielny
  10. Peter Odimwingie
Your All Welcome!!!!!!!!!!!!

Kampuni zasambaza dawa bandia

Mustapha Kapalata,Nzega
WANANCHI wa Kata ya Shigamba wilayani Nzega, mkoani Tabora wameilalamikia kampuni ya Biosustain (T) LTD kwa kuwapatia dawa bandia za kupulizia pamba tofauti na makubaliano ya awali.

BIOSUSTAIN ni kampuni inayojihusisha na kilimo cha pamba cha mkataba wilayani hapa yenye makao makuu yake mkoani Singida
Wananchi hao kwa nyakati tofauti walisema dawa hiyo aina ya Zetabestox,  haina uwezo wa kuangamiza wadudu na kwamba wadudu wanaendelea kushambulia mazao.

Kampuni hiyo imesambaza chupa za dawa bandia zaidi ya 1,017 huku kila chupa ikiuzwa Sh1,500 na kampuni hiyo ina hudumia Kata 34 wilayani hapa.

Daudi Nhonge Diwani wa kata hiyo alisema kuwa kampuni hiyo imesababisha hasara kubwa kwa wananchi hasa katika msimu huu wa kupulizia dawa kwenye zao la pamba.

Diwani huyo alishauri taratibu zifuatwe kama mkataba unavyoeleza kwamba endapo  mkulima au kampuni atakaye sababisha hasara anapaswa kuchukuliwa  hatua za kisheria.

‘’Kampuni ya Biosastain imewapa hasara kubwa wananchi hasa kwa kuwapatia dawa bandia, tunaiomba serikali ichukue hatua kali dhidi ya ubadhilifu huo,’’ alisema diwani huyo.

Zaidi ya fekati 2,500 za pamba zimeliwa na wananchi hao kutokana na kampeni kubwa iliofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Florence Holombe.

Ofisa Kilimo na Mifugo, Willam Mafwele akizungumza kwa njia ya simu yake ya mkononi alisema amepokea  malalamiko ya wananchi kuhusu dawa hiyo na kufafanua kwamba tayari ameitaarifu bodi ya pamba.

 Naye Yohana Basanda Msimamizi wa kampuni hiyo akizungumuza kuhusu malalamiko hayo alikiri kwamba dawa hiyo haiui wadudu na alisisitiza kuwa wanafanya jitihada za kupata dawa nyingine.

Basanda aliwaomba wakulima waendelee kusubiri kwa kuwa tatizo linatafutiwa ufumbuzi haraka.Alisema kampuni iliwauzia dawa bandia na tayari wamepeleka taarifa kwa kampuni hiyo kwamba wamepokea malalamiko kutoka kwa wananchi dawa hiyo haifanyi kazi

Asilimia 35 ya wangonjwa wa kansa ni wa sigara’

Tausi Ally                                
UVUTAJI sigara au wanaopokea moshi wa sigara wametajwa kulazwa wengi kwa kansa nchini.Habari ziolisema asilimia 35 ya watu wanaougua ugonjwa wa kansa waliolazwa Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam, wamepata ugonjwa huo  baada ya  matumizi ya sigara (tumbaku) au kupokea moshi wa sigara kutoka kwa wavutaji.

Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Hospitali ya IMTU, Dk  Ali Mzige wakati akichangia mada kwenye mkutano wa Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) wa kuzuia matumizi ya sigara, tumbaku, ugoro, kuberi na bangi.

Dk Mzige alisema matumizi ya vilevi  hivyo kwenye jamii katika mikusanyiko ya watu hususani kwenye vituo vya afya,  yanasababisha madhara kwa wavutaji na kwa wale wasiovuta, lakini wanapokea moshi kutoka kwa wavutaji. "Asilimia 85 ya kansa wanazoumwa wanaume duniani vyanzo vyake vinahusishwa na  matumizi ya tumbaku, sigara, ugoro, kuberi  na kwa wale wasiotumia kupokea moshi kutoka kwa watumiaji hao,"alisisitiza Dk Mzige.

Alisema watumiaji wa sigara na tumbaku wapo katika hatari ya kupata madhara  ya nywele  kunyonyoka,  mtoto wa jicho, kukunjamana kwa ngozi, kutosikia vizuri na saratani ya ngozi.

 Madhara mengine wanavyoweza kuyapata watumiaji hao ni  meno kuoza, mapafu  kushindwa  kufanya kazi vizuri,  ulaini wa mifupa, magonjwa ya moyo, vidonda vya tumbo,  vidole kubadilika rangi, kansa ya kizazi, kuharibika kwa mimba,  kupunguza nguvu za kiume, ukurutu, kuziba kwa mishipa midogo ya damu  pamoja na kansa ya mapafu na viungo vingine.

 “Madhara yanayotokana na matumizi ya sigara na tumbaku ni makubwa, tushirikiane kuzuia matumizi ya vitu hivi kwenye mikusanyiko ya watu na hata kwenye vituo vya afya  kwa sababu, takwimu zinatisha na wanaothirika zaidi ni wale wasiotumia vilevi hivyo bali wanapokea moshi tu,” alisisitiza kusema Dk Mzige.

 Alibainisha kuwa watu wengi wanaojihusisha na matukio ya kujiua, ukifuatia undani wao walikuwa ni wavuta sigara ambapo kwa upande wa bangi Dk Mzige alisema inasababisha ungonjwa wa kansa na  kuharibu ubongo kwakuwa ina kemikali 400.
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger