BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

Mgomo wa madaktari waanza rasmi

Written By Koka Albert on Sunday, June 24, 2012 | 1:03 AM

Mgonjwa akihamishwa kutoka Wodi ya Kibasila katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), iliyopo Dar es Salaam jana, ili kupelekwa katika hospitali nyinyine kutokana na tihsio la kuwepo kwa mgomo wa madaktari, katika hospitali hiyo na nyingine za serikali sehemu mbali mbali nchini wanaodai stahiki zao mbali mbali, kwa madai ya serikali kushindwa kuzitekeleza. Picha na Emmanuel Herman
HUDUMA ZA KAWAIDA ZAZOROTA
Waandishi Wetu, Dar na Mikoani       
 MADAKTARI nchini wameanza mgomo katika baadhi ya hospitali nchini baada ya Serikali kushindwa kutekeleza madai yao waliyowasilisha katika Kamati ya Majadiliano iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.  Mgomo huo umetangazwa na Jumuiya ya Madaktari nchini huku ikifafanua kwamba kati ya madai kumi waliyotaka yatekelezwe na Serikali, hakuna hata moja lililofanyiwa kazi.  Hata hivyo,  jana madaktari hao ambao walikaa vikao vya majadiliano na Serikali kwa siku 90 baada ya kusitisha mgomo wao wa pili, wamesema katika madai yao kumi, hakuna hata moja lililotekelezwa na Serikali.  Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Dk Stephen Ulimboka jana aliwaeleza waandishi wa habari kwamba ili warejee kazini, Serikali inatakiwa kutekeleza madai yao yote na kusisitiza kwamba dai lao la kwanza ni kuitaka Serikali kuboresha huduma za msingi kwa wagonjwa.   
“Mgomo umeanza leo na hauna kikomo, lengo ni kuishinikiza Serikali kutekeleza madai yetu, hata zile huduma za dharura nazo kuanzia kesho (leo) zinaweza kusitishwa,” alisema Dk Ulimboka.  Wakati Ulimboka akieleza hayo, huduma katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na Taasisi ya Mifupa (Moi) ilikuwa ikitolewa kwa kusuasua huku baadhi ya wafanyakazi wakisisitiza kuwa mgomo huo upo. 

Licha ya wafanyakazi hao kukiri kuwa siku za mwisho wa wiki idadi ya wagonjwa katika hospitali hizo huwa ndogo, lakini walisisitiza kuwapo kwa mgomo huo na kufafanua kuwa kwa mtu mgeni katika eneo hilo si rahisi kutambua hali hiyo.  Mwananchi Jumapili lilifika katika hospitali hiyo na kukuta huduma zikitolewa ‘kiaina’ huku baadhi ya wagonjwa wakieleza kwamba zimezorota, sio kama siku zilizopita.  

Tamko la Jumuiya      Akieleza kwa kina sababu za mgomo huo, Dk Ulimboka alisema katika madai waliyoyawasilisha, hakuna hata moja lililotekelezwa na kufafanua kwamba Serikali imeongeza dai ambalo wao hawakuliwasilisha.  Madai hayo ni pamoja na kupandishwa kwa ongezeko la mishahara, posho ya kuitwa kazini, posho za kufanya kazi katika mazingira magumu, bima ya afya, nyumba za kuishi, kukopeshwa magari kwa ajili ya usafiri, kuboreshwa kwa mazingira ya kufanyia kazi kwa kupeleka vifaa vya kazi, dawa na kuboresha miundombinu.  

“Serikali imesema imerekebisha viwango vinavyotumika kulipa posho ya uchunguzi wa maiti  kwa Sh 100,000 kwa uchunguzi wa madaktari na Sh50,000 kwa watumishi wengine, lakini hili halikuwa dai letu!” alisema Dk Ulimboka.   Naye Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi aliwatahadharisha madaktari hao kuacha mgomo, akieleza kuwa ni batili na ni kinyume cha viapo vyao vya kazi.  Dk Mwinyi aliainisha mambo 10 ambayo madaktari walikuwa wamepanga kutekelezewa na kusema kuwa kwa sehemu, yametekelezwa na baadhi ya mambo yaliyobakia wanaweza kuyazungumza.

Mwanza
Madaktari zaidi ya 200 waliopo katika Hosptali ya Rufaa ya Bugando jana walianza mgomo rasmi baada ya Serikali kushindwa kutoa majibu ya kuridhisha kuhusu madai yao mbalimbali yaliyosababisha madaktari hao kugoma mapema mwaka huu.  Akizungumza na Mwananchi Jumapili, Mwakilishi wa Kamati ndogo ya kufuatilia madai madaktari hao, Dk Richard Kirita alisema kwamba madaktari wa kada zote katika hospitali hiyo wapo kwenye mgomo isipokuwa baadhi ya madaktari bingwa pamoja na wakuu wa idara.

 “Kwa kuwa leo sio siku ya kazi unaweza kudhani hakuna mgomo, lakini njoo Jumatatu (kesho) ndo utapata picha halisi ya mgomo kwa sababu wagonjwa watakuwa wengi, lakini hakutakuwa na huduma,”alisema 
Moshi

Hali ya utendaji wa madaktari mkoani Kilimanjaro imeonekana ya kusuasua huku baadhi ya madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC wakisema hawaingii kazini na wengine wakisema bado wanasikilizia.

Katika Hospitali ya Mkoa ya Mawenzi, madaktari waliokuwa zamu walisema kwa leo huwezi kujua aliyeko kwenye mgomo na ambaye hayupo, kwani wengi hawako kazini leo hadi kesho.  

 Baadhi ya wagonjwa waliolazwa Hospitali ya KCMC katika wodi ya wanawake, walisema kuwa walitangaziwa kuwa kutakuwa na mgomo wa madaktari na kila mmoja aangalie cha kufanya na kuwa walifika wodini hapo asubuhi na hawakuzungumza na mgonjwa na kutoka.   Wagonjwa hao wamesema Ijumaa jioni wagonjwa wengi waliruhusiwa kuondoka hata kama hali zao hazijatengemaa ambapo walisema wanahofia afya zao kama madaktari watatekeleza msimamo wao.   Mbeya   Katika Hospitali ya Rufaa Mbeya madaktari 10  kati ya 80  ndiyo waliokubali jana kuendelea na  huduma ya kutibu wagonjwa ambapo wengine wameanza mgomo rasmi. 

Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Mbeya, Dk Eliuter Samky amethibitisha kuwapo na hali ya mgomo na kwamba ana uhakika wa madaktari 10 waliopo zamu kuendelea kazi.     

Awali Mwandishi wa gazeti hili alipofika  katika hospitali hiyo hakukuta daktari yeyote na ofisi za utawala zikiwa zimefungwa huku katika eneo la mapokezi likiwa na wagonjwa ambao wamekaa wakisubiria kupata huduma.  Katika kitengo cha wazazi Meta wanawake wanaokwenda kupata huduma  wamesema wameingiwa na hofu kubwa kwa kukosa huduma hiyo baada ya kuona matangazo yanayosema hakuna mgojwa atakayepatiwa matibabu.  

Wakizungumza hospitalini hapo wanawake hao ambao hawakutaka kuandikwa majina yao, walisema kuwa mbali na kuona tangazo hilo lakini pia waliambiwa na baadhi ya madaktari kuwa ni bora wakaenda sehemu nyingine kwa ajili ya matibabu kwa kile kilichoelezwa kuwa kuwa na wao wapo katika mgomo huo hivyo hakuta kuwa na huduma yeyote kwa mgonjwa.

Furious Nasri swears at journalist following France's Euro 2012 exit

Temper, temper: Nasri (right)
France midfielder Samir Nasri was involved in a row with a French reporter after his team were knocked out of Euro 2012 in the quarter-finals 2-0 by Spain.

Nasri, who came in as a second-half substitute, went through the mixed zone without a word for text reporters after the match.

Asked by a reporter for a quote, he answered: 'You are looking for s***, you are looking for trouble.'

The reporter replied: 'Get lost.'

Nasri then turned back and said 'f*** you' followed by a stream of further abuse, inviting the reporter to have a conversation with him man-to-man.

Nasri had already been involved in a row with the media at the tournament when he muttered 'shut up' after scoring the equaliser in France's 1-1 draw against England in their opening game.

Euro 2012 yaua shabiki China

Written By Koka Albert on Saturday, June 23, 2012 | 8:23 AM

Beijing, China
SHABIKI wa soka nchini China, Jiang Xiaoshan amefariki baada kukaa siku 11 bila kulala akiashuhudia kwenye televisheni mechi zote za michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya inayoendelea Poland na Ukraine.

Shabiki huyo anadaiwa kuziunga mkono England na Ufaransa kwenye michuano hiyo, alifariki kutokana kutokana na mwili kuchoka Jumanne wiki hii.

Kwa sababu ya muda tofauti wa kurushwa kwa mechi hizo, Xiaoshan hakuwahi kulala kwa muda wote huo na badala yake alikesha kuangalia mechi hizo na kisha siku iliyofuata kwenda kazini.
 
Kwa mujibu wa mtandao wa sina.com, shabiki huyo alishuhudia kwenye televisheni mchezo kati ya  Ireland na Italia ambapo alirejea nyumbani saa 11 alfajiri na alipoamua kulala hakuamka tena.

Taarifa zaidi zilidai kuwa matumizi ya tumbaku na na pombe na kuchoka kulikotokana na kushindwa kulala, kunaelezwa kuwa chanzo cha sababu.

Mechi zote alizoangalia Xiaoshan ni sawa na dakika 1890, ambapo aliweza kushuhudia mabao 51 kabla ya kufariki kwake.

Yondani awashusha joto mashabiki Yanga

Sweetbert Lukonge
BEKI Kelvin Yondani ambaye amekuwa kiini cha habari katika kurasa za michezo kwa zaidi ya wiki mbili sasa, hatimaye ameanza rasmi mazoezi na klabu yake, Yanga ya jijini Dar es Salaam aliyojiunga katika uhamisho ulioleta utata toka mabingwa wa soka nchini, Simba nayo ya jijini.
Awali, Yondani alitarajia kujiunga na mazoezi ya vijana hao wa jezi za Kijani na Njano juzi, lakini hakutokea na hivyo kuleta presha kwa mashabiki wa Yanga waliojitokeza kumshuhudia kwa mara ya kwanza.

Mamia ya mashabiki wa Yanga hawakuamini macho yao walipomuaona Yondani akiwasili Makao Makuu ya klabu hiyo mtaa wa Jangwani akiwa na baadhi ya wachezaji wengine.

Kilichofuata kwa mashabiki hao baada ya kumuon Yondani, ni furaha na shangwe kutoka, ikiwa ni kielelezo tosha ya kumkubali kuja Jangwani akitoka mahasimu wao wakubwa Simba.
Shangwe za kumpokea Yondani zilikwenda sambamba nyimbo za kebei toka kwa mashabiki wa Yanga dhidi ya Mwenyekiti wa Simba, Adeni Rage ambaye wakati fulani aliwahi kusema: "Yondani kamwe hawezi kwenda Yanga."

Ni wazi Yondani atakuwa na mzigo mkubwa wa kuisaidia Yanga kupata mafanikio baada ya msimu huu kumaliza ligi nafasi ya tatu ikiwa ni mara ya kwanza zaidi ya miaka 20.

Yondani alivaa jezi namba tano ambayo pia alikuwa akiivaa wakati akicheza Simba, na muda wote wa mazoezi kwenye Uwanja wa Kaunda alikuwa akishangiliwa na mashabiki.

Lakini hiyo haikuwa mara ya kwanza kwa Yondani kushangiliwa na mashabiki wa Yanga, kwani walifanya hivyo wakati alipovaa jezi ya timu ya Taifa kwenye mchezo wa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Gambia Uwanja wa Taifa zaidi ya wiki mbili zilizopita.

Mbali na kelele za kushangiliwa Yondani, pia wachezaji Ladislaus Mbogo aliyejiunga na toka Toto African ya Mwanza, Saimon Msuva (Moro United) pamoja na Frank Domayo (JKT Ruvu) nao waliziteka kelele za kishabiki.

Kocha Felix Minziro alisema anafarahishwa na uwezo ulioonyeshwa na wachezaji wake wapya hali inayomfanya kuwa na matumaini ya kufanya vizuri msimu ujao.

Minziro alisema kipimo chake kikubwa cha kwanza ni michuano ya Kombe la Kagame ambayo Yanga ndiyo mabingwa watetezi.

"Usajili wetu ni mzuri, wachezaji wote wapya wameonyesha uwezo mkubwa, wanajituma na wako tayari kutekeleza majukumu yao bila maelekezo mengi," alisema Minziro.

Aidha alisema uongozi wake kwa sasa unafanya mipango ya kusajili wachezaji wawili wa kimataifa kuziba nafasi za wachezaji Davis Mwape na Kenneth Asamoah ambaye Alihamis hajaonekana kwenye mazoezi tangu Alhamisi.

Kuhusu kutoonekana kwenye mazoezi kwa mchezajiRashidi Gumbo, Minziro alisema hana taarifa zozote ingawa ilidaiwa kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa malaria.

Serikali yaahidi walioua mtalii kukamatwa

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi, wamemhakikishia Balozi wa Uholanzi nchini, Dk Ad Koekkoek, kuwa majangili wote waliohusika na mauaji ya mtalii Eric Brekelmans(53) wanakamatwa.

Hatua hiyo inafuatia agizo la Rais Jakaya Kikwete, kuwaagiza mawaziri hao kufuatilia mauaji hayo, hali iliyosababisha kukatisha kuhudhuria vikao juzi kwenda Arusha kukutana na Balozi Koekkoek na mjane wa Brekelmans, Annelnes.

Kifo hicho kilitokea katika Kambi ya Moivaro,Kijiji cha Robanda, kwa kupigwa risasi na majangili.
Mawaziri hao, waliondoka kwa ndege ya Shirika la Hifadhi za Taifa(Tanapa) juzi mchana mjini Dodoma kwenda Serengeti kufuatilia tukio hilo.

Pia, majangili hao walimuua Meneja msaidizi wa kambi hiyo,  Renatus  Bernard na watalii wengine 40 waliporwa mali zenye thamani ya zaidi ya Sh20 milioni.

Wakizungumza juzi usiku mjini Arusha na balozi huyo na mjane nyumbani kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Leopard, Zuher Fazal,mawaziri hao walitoa pole kwa tukio hilo ambalo walisema siyo la kawaida na ndiyo  maana walitumwa na Rais Kikwetekwenda eneo la tukio.

Balozi Kagasheki alisema,tukio hilo limeisononesha Serikali na Watanzania kwa ujumla, kwani dunia nzima inatambua amani na utulivu uliopo nchini.

Dk Nchimbi alisemaSerikali itahakikisha wote waliohusika na mauaji hayo wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya dola.

Naye mjane Brekelmans, Annelnes aliishukuru Serikali ya Tanzania, kwa ukaribu ilioonyesha na kwamba, mumewe aliuawa kwa kupigwa risasi kifuasi wakati akipambana na majangili hayo, huku yeye akijeruhiwa kwa panga.

Hata hivyo, Annelnes alisema usalama katika kambi hiyosiyo mzuri, kwani ina eneo kubwa na hakuna usalama wa kutosha, jambo ambalo alishauri lirekebishwe.

Kwa upande wake,Balozi Dk Koekkoek alieleza kusikitishwa na tukio hilo, huku akimshukuru Rais Kikwete, mawaziri hao na watu wengine ambao wamekuwa wakishirikiana naye tangu tukio hilo kutokea.

Duuuuuh,,, Kumbe mpaka Twiga Stars Kulikuwa na wasagaji!!!!!!!!!

Written By Koka Albert on Thursday, June 21, 2012 | 3:21 AM

KOCHA aliyetema kibarua cha kuifundisha timu ya taifa ya wanawake (Twiga Stars), Boniface Mkwasa amesema moja ya mambo yaliyokuwa yakimchukiza na kuyakemea kwa nguvu zote ni tabia ya usagaji kwa baadhi ya wachezaji wa timu hiyo.

Mkwasa alitangaza kuachia ngazi kuifundisha Twiga  mwanzoni mwa wiki hii ikiwa ni siku moja baada ya kukosa fursa ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kufuatia kufungwa nyumbani na ugenini na wenzao wa Ethiopia.

Mkwasa, mwanasoka wa zamani wa kimataifa wa Yanga na timu ya Taifa (Taifa Stars), alikiri kuwapo kwa vitendo hivyo kwa baadhi ya wachezaji, na waliobainika walichukuliwa hatua mara moja.
Bila kuwataja majina baadhi ya wachezaji waliokuwa na tabia hizo, Mkwasa alisema uongozi wake ulilazimika kuwatimua waliobainika kupenda mchezo huo.

Mkwasa aliyekuwa akihojiwa na kipindi cha 'Tuongee asubuhi' kilichorushwa na kituo cha televisheni cha Star Tv alisema: “Kwa wale tuliokua tukiwasikia na kupata ushahidi kupenda tabia ya usagaji tuliwaondoa kwenye timu." Mkwasa alisema mara kwa mara alikuwa akiwasiliana na meneja wa timu kufuatilia kwa karibu tabia za wachezaji hao.

“Nilikuwa nawasiliana na meneja wa timu na kuchukua hatua haraka kwa wale wote waliokuwa na tabia ya kupenda kusagana," alisema kocha huyo.

Wakati huohuo, mdau mkubwa wa soka la wanawake nchini na miongoni mwa waanzilishi wa ligi ya wanawake jijini Dar es Salaam, Frank Mchaki, amepongeza hatua ya aliyekuwa kocha wa timu ya Taifa (Twiga Stars), Boniface Mkwasa kuachia ngazi.

Mchaki, alisema uamuzi wa Mkwasa unastahili pongezi hasa kutoka na ukweli kwamba siyo utamaduni wa wengi kukubali kuwajibika pale wanaposhindwa kufikia malengo waliyopewa.

"Nampongeza kwa uamuzi wake,  lakini Chama cha Soka la Wanawake (TWFA), ambacho ndicho chenye jukumu la kuhakikisha soka la wanawake linasonga mbele kinafanya nini,"alihoji Msaki.
Mchaki, Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Soka Kindondoni (Kifa), alisema ni ndoto kwa soka la wanawake kufanikiwa kama hakutakuwa na mpango endelevu wa kuibua vipaji vipya.

"Timu yetu ni ile ile, wachezaji ni walewale miaka nenda, rudi. Sasa katika hali kama hii, Mkwasa anaweza kuleta mabadiliko?" alihoji Mchaki.

Matokeo ya kufanya vibaya kwa Twigani kwa sababu ya kutotiliwa mkazo ligi ya wanawake ambayo ndiyo mhimili mkubwa wa kujenga timu imara ya taifa.

Alitoa ushauri kwa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kukaa chini na kujadili kwa pamoja nini kifanyike ili kuinua soka hilo lililoanza kuvuta hisia za mashabiki wengi.

"Kwa hali ilivyo sasa, kufikia mwaka 2015, Twiga Stars hii tunayoiona sasa haitakuwapo tena kama hakutakuwa na juhudi za haraka kutoka mamlaka zinazosimamia mchezo wa soka," alisema Mchaki.

Mtei akoleza moto wa Mnyika

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi akizungumza na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika katika viwanja vya bunge jana. Mnyika amerejea kuhudhuria vikao vya bunge baada ya juzi kutimuliwa bungeni na Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai. Picha na Edwin Mjwahuzi
Moses Mashalla, Arusha
MWASISI wa Chadema, Edwin Mtei amemtetea Mbunge wa Ubungo, John Myika kuwa alikuwa sahihi kusema kwa Rais Jakaya Kikwete ni dhaifu, kwa kuwa kuna matukio mengi yaliyohitaji uamuzi wake na hakuutoa kwa wakati.

Pia Mtei amelaumu Kanuni za Bunge zilizomwezesha Naibu Spika, Job Ndugai kumtoa nje ya ukumbi wa Bunge mbunge huyo.

  Juzi, Mnyika alitolewa nje ya ukumbi wa Bunge, baada ya kukukataa kufuta kauli yake kuwa ‘Rais Jakaya Kikwete ni dhaifu’.
Akitetea kauli hiyo, Mtei alirejea baadhi ya matukio aliyodai yanaonyesha udhaifu huo, ukiwamo uamuzi ya Rais Kikwete juu ya hatua za kuwachukulia walioiba fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mtei alifafanua kwamba,  kitendo cha Rais  Kikwete kuwataka wezi hao warudishe fedha walizoiba badala ya kuwakamata, kinadhihirisha udhaifu mkubwa wa kiongozi huyo.

  “Rais Kikwete ana udhaifu wa kuwachukulia hatua za kisheria watu ambao wanahujumu taifa  kwa ufisadi…udhaifu wa Rais ni kama kutowadhibiti wezi wa fedha zetu kama fedha za EPA. Aliwaambia wezi warudishe fedha, badala ya kuwatia ndani wanabaki wanatamba kwa kuiba fedha zetu,” alisisitiza Mtei aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu.

 Alisema kibaya zaidi ni kwamba, nchi inayumba kutokana na uongozi mbovu kuanzia ngazi ya urais hadi chini, kwa kuwa tunaongozwa na watu wasiojua na kuisimamia Katiba.

Kauli kuhusu Bajeti
Akitoa maoni yake juu ya Bajeti ya Serikali ya mwaka huu, Mtei alisema Bajeti hiyo haina jipya kwa kuwa haishughulikii matatizo na kero za wananchi.

Alisema Bajeti hiyo ambayo mjadala wake unahitimishwa kesho, haiwezi kukabilina na mfumuko wa bei unaolikabili taifa.

Kuhusu suala la deni la Taifa linalofikia Sh20.2 trilioni, alisema nchi ipo njia panda, hali ambayo ni hatari kwa kuwa ni mzigo kwa taifa na linazidi kuongezeka kila mwaka.

Mwanasiasa huyo ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa Chadema, aliponda vitendo vya Serikali kukopa fedha kila mara kwenye mabenki ya kibiashara nchini, na kuomba kwa wahisani.   MWISHO.     
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger