BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

MBUYU NDANI YA YANGA

Written By Koka Albert on Friday, August 24, 2012 | 3:32 AM

Beki mpya wa Yanga, Mbuyu Twite akifanya mazoezi jana asubuhi kwenye Uwanja wa Amahoro jijini Kigali. Yanga leo itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Rayon Sports. Picha na Doris Maliyaga.
BEKI mpya wa Yanga, Mbuyu Twite jana asubuhi alianza mazoezi rasmi na mabingwa wa Kombe la Kagame ambao leo watashuka dimbani kuivaa Rayon Sports kwenye Uwanja wa Amaholo jijini Kigali.

Katika siku za karibuni Mbuyu alitawala vichwa vya habari vya magazeti kufuatia sakata lake la kujiunga na Yanga muda mfupi baada ya Simba kutangaza kumsajili.

Akizungumzia na Mwananchi, Mbuyu alisema anajisikia vizuri kuungana na wachezaji wenzake na kuomba kupewa ushirikiano ili wafanikiwe kutwaa mataji mengi zaidi.

"Nimefurahi kujiunga na wenzangu, najisikia furaha kuwa nao na naahidi kushirikiana nao vizuri ili kuipa Yanga mataji ,"alisema Mbuyu aliyekuwa amevaa jezi namba 9 mgongoni wakati wa mazoezi hayo.

Naye kocha mkuu wa Yanga, Tom Saintfiet alisema,"Mbuyu ni mchezaji mzuri naamini ataisaidia Yanga, lakini hiyo yote itatokana na juhudi zake pamoja na wenzake."

Kocha Saintfiet alisema katika mchezo wao wa leo anategemea Mbuyu ataanzia benchi kwa kuwa ndio kwanza ameanza mazoezi na wenzake.

"Mazingira ya kambi ni mazuri, uwanja ni mzuri na tumefanya mazoezi kwa siku mbili (juzi na jana) na kesho (leo) tunacheza mechi bila shida," alisema Saintfiet.

Alisema,"mechi hiyo ni muhimu kwetu kwa sababu timu tunayocheza nayo ni nzuri na ina ushindani, naamini tutapata mazoezi ya kutosha hapa Kigali."

Katika mazoezi ya jana asubuhi kwenye Uwanja wa Amaholo, Yanga walianza kwa kukimbia na kufanya mazoezi ya viungo baada ya hapo, Saintfiet aliwataka wachezaji kucheza kwa nafasi na walitumia nusu Uwanja pamoja na kupiga mashuti.

Baada ya hapo walicheza mpira kwa mtindo wa mechi katika vikosi viwili tofauti.

Kwa mujibu wa mazoezi ya jana kikosi cha Yanga kitakuwa hivi katika mechi ya leo: Ally Mustapha, Shadrack Nsajigwa, Oscar Joshua, Nadir Haroub, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na Nizar Khalfan.

Mramba azidi kumkandamiza Mkapa mahakamani

Waziri wa zamani Fedha, Basil Mramba (Kushoto), Waziri wa zamani wa Nishati, Daniel Yona (Katikati) na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Grey Mgonja wakiwa ndani ya chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana, wakisubiri kuendelea kwa kesi yao ambapo wote wanatuhumiwa kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh11.7 Bilioni wakati wa uongozi wao. Picha na Venance Nestory
ALIYEKUWA Waziri wa Fedha Basil Mramba, jana aliendelea kumkandamiza aliyekuwa bosi wake na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, akimhusisha moja kwa moja na kutolewa kwa msamaha wa kodi kwa kampuni ya Alex Stewart Government Business Assayers.

Mramba aliyaeleza hayo jana wakati akijitetea dhidi ya tuhuma zinazomkabili za matumizi mabaya ya ofisi za umma na kuisababishia Serikali hasara ya Sh11.7 bilioni na kwamba alitoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo ili kutekeleza matakwa ya mkataba.

Alidai kuwa kifungu cha 4.3.1  kilichopo kwenye  mkataba huo ulioingiwa kati ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Alex Stewart Government Business Assayers kinasema malipo yoyote  yatakayolipwa na mkataba huo hayatotozwa kodi.
“Mimi nilichofanya ni kutekeleza  matakwa ya mkataba huu kwa sababu Waziri wa Fedha  pekee ndiye mwenye mamlaka  ya kutekeleza mkataba huo,” alidai Mramba.

Mramba alikiri kuruhusu gavana wa BoT kuilipa kampuni ya Alex Stewart,  Dola za Marekani 1 milioni kama malipo ya awali, kwa ajili ya kufanya maandalizi ya ukaguzi wa migodi ya madini, na kwamba fedha nyingine zingelipwa kwa awamu.
Mramba alisema aliruhusu malipo hayo kufanyika kutokana na kuwapo kwa barua  ya Mei 13, 2003, kutoka kwa Katibu Mkuu wa Rais, Patrick Mombo  kwenda kwa Katibu Mkuu wa Nishati na Madini kuhusu mkaguzi wa dhahabu ikisema “Rais amekubali Waziri wa Fedha na BoT watafute njia ya kuilipa kampuni ya Alex Stewart Government Business Assayers”.
“Maagizo yote mimi niliyachukulia  kama ni ya Rais, alikuwa akiagiza watendaji wake kutekeleza majukumu yote,”alisema Mramba na kuongeza kuwa kwa kuzingatia makubaliano hayo alitafuta fedha hizo kupitia bungeni katika Bajeti ya Serikali ya 2003/04.

Kuhusu mkataba, Mramba alisema kuwa anachofahamu yeye sheria ya BoT inampa mamlaka Gavana kuingia mikataba na kuisaini na kwamba mikataba yote aliyoingia na watu wengine ni lazima kodi isamehewe.
Mramba aliiambia mahakama hiyo kuwa, kampuni ya Alex Stewart Government Business Assayers ilikuwa ikitaka malipo bila kodi na kwamba, wao walikubali kutomtoza kodi kutokana na ushauri kutoka kwa wataalamu akiwamo gavana kuwa wamsamehe kodi vinginevyo wangemlipa zaidi. 
Hata hivyo, alisema mkataba baina ya BoT na kampuni hiyo haukuwahi kupitia katika kikao cha Baraza la Mawaziri. “Sikudhani kama angeweza kutiliana nao saini kwenye mkataba huo,  bila Baraza la Mawaziri kuridhia,”alisema Mramba.
Ushauri wa TRA

Mramba alibainisha kuwa Bethar Soka  ambaye alikuwa kwenye kamati iliyofanya mchakato wa kuitafuta kampuni hiyo ya ukaguzi wa dhahabu, aliomba kupata kauli ya TRA  kama kampuni ya Alex Stewart Government Bussines Assayers isamehewe kodi ama la, Mei 26, 2003.

Alidai kuwa baada ya  Soka kupeleka ombi hilo Mei 26, 2003, TRA katika majibu yao ya Juni 24, 2003 walisema kuwa hawapendekezi mkaguzi huyo wa dhahabu asamehewe kodi na kwamba barua hiyo ilipelekwa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha wakati BoT na kampuni ya Alex Stewart Government Business Assayers iliingia mkataba  Juni 14, 2003.

“Inaonyesha barua hiyo ya TRA ilichelewa  kwa siku 10, baada ya mkataba kusainiwa,  hata hivyo, ushauri huu wa TRA hatukuuhitaji  hata kama ungekuja  haungekuwa na manufaa,” aliongeza kudai Mramba.

Baada ya maelezo hayo, mmoja wa wanaosikiliza kesi hiyo, Hakimu Saul Kinemela, alimuuliza Mramba, Wizara ya Fedha  iliomba ushauri  huo TRA kwa kazi gani?

Akijibu swali hilo, Mramba alisema, "Siyo Wizara ya Fedha iliomba ushauri TRA, bali Soka aliomba ushauri huo kama mwanakamati iliyokuwa ikifanya mchakato wa kutafuta kampuni hiyo na  kwamba  Soka yeye  alikuwa ni mtumishi wa wizara yake.

Alibainisha kuwa  Soka  asingeweza  kumshauri  Waziri,  anayeweza kumshauri ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu.

Mbali na Mramba, wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja.
Jaji John Utamwa aliiahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 12, mwaka huu itakapoendelea na utetezi.
Utetezi wa awali

Mramba (71) alianza kujitetea, Agosti 22, mwaka huu  ambapo alidai kuwa Serikali iliiteua BoT ifanye kazi ya kutafuta  kampuni inayoweza kufanya kazi hiyo hivyo ikaingia mkataba na kampuni iliyochaguliwa  ya Alex Stewart Government Bussines Assayers.

Waziri huyo wa zamani aliongeza kudai kuwa aliyeagiza BOT kufanya kazi hiyo ya kumtafuta mkaguzi wa dhahabu ni Rais wa Awamu ya Tatu, Mkapa na kwamba wakati huo yeye akiwa Waziri wa Wizara ya Fedha alipewa jukumu la kuhakikisha gharama za kumlipa mkaguzi huyo zinapatikana ndani ya Serikali au BoT ama pengine popote.

Alifafanua kuwa kati yake yeye na gavana  hakuna aliyekuwa na mamlaka  juu ya mwingine na kwamba gavana alikuwa  na wajibu wa kufanya mchakato wa kumtafuta mkaguzi wa dhahabu.

Mramba alisisitiza kudai kuwa yeye hakuhusika kwenye mchakato huo kwa kumtafuta wala kumleta hapa nchini  wala kumtuma mwakilishi  yeyote  kumwakilisha kwenye kamati iliyoteuliwa  kufanya mchakato huo bali alipewa agizo la kumlipa.

“Mimi kama waziri sikuwa na mtu wangu kwenye ile kamati, lakini Wizara ilituma mwakilishi, ambaye alikuwa mwanasheria Bethar Soka wakati wa kuhoji kampuni mbili  ili wachague na kwenye kujadili vipengele vya mkataba,”alisema.

Inadaiwa kuwa, kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14, mwaka 2004, jijini Dar es Salaam, washtakiwa wakiwa watumishi wa umma, walitumia vibaya madaraka yao na kuisababishia Serikali hasara ya Sh11.7 bilioni.

Ilidaiwa kuwa washtakiwa hao waliipatia msamaha wa kodi isivyo halali, Kampuni ya M/S Alex Stewart ya Uingereza.

JIMBO LA IGUNGA WAZI

Written By Koka Albert on Tuesday, August 21, 2012 | 5:06 AM

*******Breaking newzzz???????????********
Mahakama kuu mkoa wa Tabora imemvua ubunge mheshimiwa Kafumu,kuanzia sasa jimbo la Igunga lipo huru bila mbunge

TP MAZEMBE YAFANYA MAUAJI, SAMATTA ANG'ARA, ATUMBUKIZA LA USHINDI

Written By Koka Albert on Monday, August 20, 2012 | 12:18 AM

Samatta
TOUT Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imejiweka sawa kwenye mbio za kuwania ubingwa wa Afrika, baada ya kuifunga  Zamalek ya Misri nyumbani kwao, Cairo mabao 2-1.
Shukrani kwake, mshambuliaji chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ‘Sama Goal’ aliyefunga bao la ushindi katika mchezo uliomalizika dakika chache zilizopita kwenye Uwanja wa chuo cha Jeshi, Al-Qahirah mjini Cairo, dakika ya 44, akiunganisha pasi ya Tressor Mputu Mabi.
Katika mchezo huo wa Kundi B, Himoonde alitangulia kuifungia Mazembe inayofundishwa na Lamine N'Diaye dakika ya 34 pasi ya Mputu, lakini Omotoyossi akaisawazishia Zamalek inayofundishwa na kocha Jorvan Vieira dakika ya 36, pasi ya Mohamed Ibrahim.
Ushindi huo wa kwanza ugenini kwa Mazembe katika hatua ya makundi, unaifanya Mazembe ifikishe pointi saba, baada ya kucheza mechi nne, kushinda mbili, sare moja na Berekum Chelsea na kufungwa moja na Al Ahly ugenini.
Al Ahly iliyotoa sare ya 1-1 na Berekum Chelsea nchini Ghana leo, bado inaongoza kundi hilo kwa pointi zake 10, wakati wababe wapya wa Ghana wanashika nafasi ya tatu kwa pointi zao tano na Zamalek wanashika mkia wakiwa hawana pointi hata moja.  
Kwa mara ya kwanza, katika mchezo wa leo, mshambuliaji mwingine wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu alikaa benchi, kwani awali amekuwa havai hata jezi.
Ulimwengu tangu asajiliwe Mazembe msimu uliopita, hii ni mechi yake ya kwanza anakaa benchi kwenye michunao ya Afrika, hizi zikiwa ni dalili njema kwamba anakaribia kuanza kucheza.
Katika mchezo huo, kikosi cha Zamalek kilikuwa; Abdel Wahed El Sayed, Mahmoud Fathalla, A. Mendomo, Sabri Rahil, Hazem Emam/ Said Kotta dk 77, Hani Saied, Ahmed Samir, Ibrahim Salah/ Mohamed Ibrahim Islam Awad/dk63, R. Omotoyossi/ Ahmed Gaafar dk71.
Mazembe; M. Kidiaba, H. Himoonde, F. Kasonde/ M. Ndonga dk 46
, J. Kasusula, S. Sunzu, J. Kimwaki, R. Kalaba, P. Ochan/ N. Kasongo dk 63, M. Mputu, G. Singuluma, M. Samata/ D. Kanda Dk 86.


Usajili Yanga watua TFF

Written By Koka Albert on Friday, August 17, 2012 | 6:56 AM

KLABU ya Yanga jana imewasilisha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), majina ya wachezaji 28 iliowasajili kwa ajili ya msimu ujao, yakiwamo pia majina ya Kelvin Yondani na Mbuyu Twite, ambao Simba wanadai wana mikataba nao.
Klabu ya Simba nayo inatarajia kupeleka usajili wake, yakiwemo majina ya Yondani na Twite, beki wa kimataifa aliyekuwa akicheza timu ya APR ya Rwanda kabla ya vigogo kila mmoja kudai ni mali yake.

Katika usajili wa Yanga uliowasilishwa jana TFF mbali na jina la Yondani na Twite, pia kuna makipa Yaw Berko, Ally Mustapha na Said Mohamed.

Walinzi wa Pembeni ni Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Juma Abdul, Oscar Joshua, David Luhende na Stephano Mwasika.
Walinzi wa kati ni Nadir Haroub, Ibrahim Job na Ladislaus Mbogo.

Viungo wa ulinzi ni  Athuman Idd,  Juma Seif Kijiko na Salum Telela, wakati wa pembeni ni Nizar Khalfan, Shamte Ally, Idrisa Rashid na Omega Seme.

Kwa upande wa viungo washambuliaji, Haruna Niyonzima, Rashid Gumbo na Nurdin Bakari, huku washambuliaji wakiwa Said Bahanunzi, Hamis Kiiza, Didier Kavumbagu na Jeryson Tegete

 Mbali na kikosi hicho pia Yanga imewasilisha majina 22 ya timu ya vijana U20 ambayo wapo pia wachezaji wa timu ya taifa Saimon Msuva na Frank Domayo ambayo majina yao yamepelekwa kwa timu ya vijana lakini wataitumikia timu hiyo kwa kucheza mechi za wakubwa.

Wengine, Geofrey Nyalusi, Yusuf Abdul, Said Manduta, Zuberi Juma, Said Mashaka, Benson Michael, Issa Ngao, Rashid Said.

Majina mengine kwenye orodha hiyo ni Frank Domayo, Omary Nasry, Clever Charles, Mwinyi Bakari, Mpenda Abdallah, Abdulahman Ally, Hussein Moshi, Abdallah Salum na  Rehani Kibingu.

Wengine ni Saimon Msuva, George Banda, Notikely Masasi, Suleiman Ussi na Kassim Jongo.

Hii Kweli Kali,,,,

Written By Koka Albert on Thursday, August 16, 2012 | 6:14 AM


Muamba 'devastated' after being told his career is over five months after heart attack

Written By Koka Albert on Wednesday, August 15, 2012 | 6:28 AM

Bolton midfielder Fabrice Muamba has spoken of his devastation at being forced to retire from football due to the heart attack he suffered in March.
The npower Championship club have announced that the 24-year-old - who had hoped to make a comeback - had made the decision to retire from the professional game after taking medical advice.
'While the news is devastating, I have much to be thankful for,' said Muamba.
Miracle recovery: Bolton's Fabrice Muamba suffered a heart attack in March
Miracle recovery: Bolton's Fabrice Muamba suffered a heart attack in March
Back at Bolton: Muamba (centre) at a club 'family fun day' last Sunday
Back at Bolton: Muamba (centre) at a club 'family fun day' last Sunday
Torchbearer: Muamba carried the Olympic Flame through Waltham Forest
Torchbearer: Muamba carried the Olympic Flame through Waltham Forest
'I thank God that I am alive and I pay tribute once again to the members of the medical team who never gave up on me.'
The Bolton midfielder 'died' for 78 minutes on the pitch at White Hart Lane after suffering a cardiac arrest during an FA Cup match.
Muamba collapsed while playing for Bolton against Tottenham at White Hart Lane in an FA Cup match on March 17.
He received lengthy attention on the pitch and it later emerged that his heart had stopped for 78 minutes.
Fateful day: Muamba suffered a cardiac arrest on the pitch at White Hart Lane in March
Fateful day: Muamba suffered a cardiac arrest on the pitch at White Hart Lane in March
Helpless: Bolton and Spurs players, and Wanderers boss Owen Coyle (centre), watched the terrifying scenes unfold
Helpless: Bolton and Spurs players, and Wanderers boss Owen Coyle (centre), watched the terrifying scenes unfold
Remarkably he made a stunning recovery and left hospital a month later.
Muamba told Bolton's official website: 'Since suffering my heart attack and being discharged from hospital, I have remained utterly positive in the belief I could one day resume my playing career and play for Bolton Wanderers once again.
'As part of my on-going recovery, last week I travelled to Belgium to seek further medical advice from a leading cardiologist.
'But the news I received was obviously not what I had hoped it would be and it means I am now announcing my retirement from professional football.
Tributes: Hundreds of get-well messages were left for Muamba at Bolton's Reebok Stadium while he was in hospital
Tributes: Hundreds of get-well messages were left for Muamba at Bolton's Reebok Stadium while he was in hospital
Rallying round: The football world united to send Muamba a get-well-soon message to the stricken Muamba
Rallying round: The football world united to send Muamba a get-well-soon message to the stricken Muamba
'Football has been my life since I was a teenage boy and it has given me so many opportunities.
'Above all else, I love the game and count myself very lucky to have been able to play at the highest level.
'I would also like to thank everyone who has supported me throughout my career, and the Bolton fans who have been incredible.
'I am blessed to have the support of my family and friends at this time.'
Thank you: Muamba with cardiologist Dr Andrew Deaner (left) and consultant cardiologist Dr Sam Mohiddin, the doctors who saved his life following his heart attack
Thank you: Muamba with cardiologist Dr Andrew Deaner (left) and consultant cardiologist Dr Sam Mohiddin, the doctors who saved his life following his heart attack
Bolton chairman Phil Gartside said: 'To have Fabrice here and with us is truly amazing and we are all very thankful for that.
'We are all hugely disappointed that Fabrice will be unable to return to his playing career but we have to be guided by the medical recommendations and the best interests of Fabrice.
'The most important thing is that Fabrice and his family have the rest of their lives ahead of them.'
Bolton boss Owen Coyle said: 'We have spoken with Fab and he knows we will always support him in whatever he wants to do and that we will always be here for him.
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Miracle man: Muamba with his fiancee Shauna after his stunning recovery
Miracle man: Muamba with his fiancee Shauna after his stunning recovery
'He is obviously massively disappointed that he won't be able to carry on his career, but everyone has seen what a fighter and strong person he is in mind and body.
'We know that he will go on to achieve great things and within all this disappointment, the most important thing is that he is here, alive, today.'
Muamba and his family fled war in the Democratic Republic of Congo, seeking asylum in the UK.
Despite arriving in London age 11, unable to speak English, he went on to achieve 10 GCSEs and three A levels and joined Arsenal's youth academy in 2002. He later joined Birmingham, before moving to Bolton in 2008.
All smiles: Muamba received an Honorary Degree from Bolton University
    All smiles: Muamba received an Honorary Degree from Bolton University
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger