BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

UZINDUZI WA VICOBA NA MH. LOWASSA KATIKA MAONYESHO YA MIAKA KUMI YA VICOBA JIJINI DAR

Written By Koka Albert on Monday, October 22, 2012 | 2:23 AM


Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Mratibu wa Maonyesho ya VICOBA Tanzania,Aldo Mfinde wakati alipokuwa akiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar tayari kwa Uzinduzi rasmi wa maonyesho ya VICOBA Tanzania.Wa pili Kulia ni Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Makongoro Mahanga na Kulia ni Mwenyekiti wa CCM,Wilaya ya Ilala,Mh Assaa Simba.
Mratibu wa Maonyesho ya VICOBA Tanzania,Aldo Mfinde akizungumza machache wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Maonyesho ya Miaka Kumi ya Wafanya biashara ndogo ndogo na Wajasiliamali wa  VICOBA uliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.wa Tatu kulia ni Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo,Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.Wengine ni Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Makongoro Mahanga (pili kulia) na Mwenyekiti wa CCM,Wilaya ya Ilala,Mh Assaa Simba.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (kulia) akimpongeza Mratibu wa Maonyesho ya VICOBA Tanzania,Aldo Mfinde mara baada ya kumaliza kuitambulisha Kamati ya VICOBA Tanzania iliokuwepo viwanjani hapo.
Burudani ya Ngoma za Asili.
Mjumbe wa Kamati ya VICOBA Tanzania,Bi. Magreth Mapunda akisoma Risala ya Chama chao hicho mbele ya Mgeni Rasmi,Mh. Edward Lowassa wakati wa hafla ya Uzinduzi rasmi wa Maonyesho ya Miaka Kumi ya Wafanyabiashara ndogo ndogo na Wajasiliamali wa  VICOBA uliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar
es Salaam  jana.
Mjumbe wa Kamati ya VICOBA Tanzania,Bi. Magreth Mapunda (kushoto) akikabidhi Risala hiyo kwa Mgeni Rasmi,Mh. Edward Lowassa.
Mwenyekiti wa CCM,Wilaya ya Ilala,Mh Assaa Simba akisalimia Wanachama wa VICOBA Tanzania.
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Makongoro Mahanga akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi kuzungumza na Wanachama wa VICOBA.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akitoa hotuba yake mbele ya wanachama wa VICOBA Tanzania wakati hafla ya Uzinduzi wa Maonyesho ya Miaka Kumi ya Wafanya biashara ndogo ndogo na Wajasiliamali wa  VICOBA uliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar  es Salaam  jana .Katika Hobuba yake,Mh. Lowassa aliwapongeza wana VICOBA kwa kuweza kujiajiri,kwani tatizo la ajira nchini bado ni tatizo kubwa na ni bomu linaweza kulipuka wakati wowote.Maonyesho hayo yataendelea mpaka jumamosi ijayo Oktoba 27.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (kushoto) akiteta jambo na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Makongoro Mahanga.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akicheza muziki sambamba na Wanachama wa VICOBA Tanzania wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Biashara ya Miaka Kumi yam Wajasilia Mali wa VICOBA tangu kuanzishwa kwakwe,iliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akibonyeza kitufe kwenye kompyuta ikiwa ni ishara ya Uzinduzi rasmi wa Maonyesho ya Miaka Kumi ya Wafanya biashara ndogo ndogo na Wajasiliamali wa  VICOBA uliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono Wanachama wa VICOBA wakati wa kuwaaga mara baada ya kufanya uzinduzi wa Maonyesho ya Miaka Kumi ya Wafanya biashara ndogo ndogo na Wajasiliamali wa  VICOBA uliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa  akiagana na baadhi ya Wanachama wa VICOBA mara baada ya uzinduzi wa Maonyesho ya Miaka Kumi ya Wafanya biashara ndogo ndogo na Wajasilia mali wa  VICOBA uliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa  akiagana na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Makongoro Mahanga.
Wanachama wa VICOBA wakijiburudisha kwa kucheza Muziki.
Maandamano ya Wanachama na Wajasiliamali wa VICOBA yakipita Mbele ya Mgeni Rasmi,ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.

CHADEMA WAELEZA YALIOYO MOYONI KUHUSIANA NA VURUGU ZILIZOTOKEA DAR ES SALAAM NA ZANZIBAR



 Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mabele Marando akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam juzi juu ya matukio makubwa yaliyotokea nchini Tanzania yakiwemo yale ya kuchomwa kwa makanisa, maandamano ya wafuasi wa dini ya Kiislamu pamoja na tukio la kutoweka kwa Sheikh Farid wa Zanzibar ambaye kwa sasa amepatikana akiwa hai.


 Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Prof. Abdallah Safari akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam.

AUNTY EZEKIEL SASA MKE WA MTU

Written By Koka Albert on Saturday, October 20, 2012 | 9:04 AM


Picha Mbali Mbali zikionyesha Aunty Ezekieli Akiwa ndani ya Shela ya Arusi ya Kiislam ..Bi Dada ndio Kashaolewa hivyo ..Hongera zake sana Tunawatakiwa maisha mema yeye na Mume Wake ...Safiiiiiiiiiiiiii





KALA JEREMIAH ATOA NYIMBO NYINGINE INAITWA "DEAR GOD"

 




Bonyeza Hapa kusikiliza

ASKARI WA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA WAMCHAPA ASKARI WA USALAMA BARABARANI KWENYE MATAA YA UBUNGO KWASABABU YA KUWAWEKA KWENYE FOLENI MUDA MREFU

Hapa wanajeshi na magari yao walizuiliwa maeneo ya Tabata Dampo
Hapa Wakitafuta Mwafaka baada ya Wanajeshi Kumchapa askari wa usalama barabarani katika Mataa ya Ubungo na Walipofika Tabata Dampo wakazuiliwa
Baadhi ya wanajeshi wakiwa Kwenye lori lao
Wakasababisha Foleni
Haya Ndio Malori ya Wanajeshi yaliyokuwa kwenye tukio
Hapa Wakitafakari Cha Kuwafanya Wanajeshi Hao

Wanajeshi wanaokadiriwa kuwa 50 kwa pamoja wamemshambulia trafiki kwenye taa za ubungo na kuondoka kwa madai kuwa kawachelewesha kwenye foleni,baada ya kuondoka magari hayo ya jeshi yalizuiwa kwa muda wa zaidi ya saa moja maeneo ya Tabata dampo.kabla ya kuachiwa kuendelea na safari yake.

HIVI UNAFAHAMU TOFAUTI YA COLLEGE, UNIVERSITY NA INSTITUTE. HEBU SOMA UONE KAMA KUNA TOFAUTI KATI YAO.

Written By Koka Albert on Wednesday, October 17, 2012 | 10:57 PM


Hebu tujaribu kuondoa utata wa maana ya majina haya yanayofanana huduma lakini kimuundo na yanayopatikana ndani huwa ni tofauti.
CHUO(COLLEGE):
Kinatoa elimu na kuzawadia wahitimu shahada mbalimbali kwa kuegemea eneo moja tu la elimu. Mfano chuo cha biashara hutoa mafunzo yanayohusu biashara katika ujumla wake na haitagusa taaluma nyingine ya elimu zaidi ya biashara.
CHUO KIKUU(UNIVERSITY):
Kina mkusanyiko wa vyuo tofauti tofauti huku kila chuo kikiegemea eneo fulani la taaluma kwa jamii.
Mfano chuo kikuu cha Dar es salaam kina vyuo tofauti tofauti ndani yake vingine vikifundisha Ualimu, Biashara na hata Sayansi ya jamii.
TAASISI(INSTITUTE):
Ni chombo kinachotoa elimu ya ujuzi na inaweza pia kuwa sehemu ya chuo kikuu au taasisi nyingine za elimu ya juu na mara nyingi huwa ni mkusanyiko wa idara tofauti tofauti.

HIVI, UNATAMBUA MATUKIO YANAYOONGOZA KUVUNJA MOYO WAKO IKIWA UTARUHUSU UENDELEE KUYAFANYA?


Kuna siku niliwahi kukaa 
na kujiuliza,
 ilikuwaje kati ya
 viungo vyote mwilini,
MOYO 
ndiyo uteuliwe kuwakilisha hisia 
zote za binadamu.

Ukiwa katili, mpole, mkarimu, mwizi, au jasiri bado utatumika 
moyo kubeba hizo sifa.
Si kitu cha ajabu kusikia mtu anapewa sifa ya  kuwa na Moyo 
mgumu, moyo mwepesi au moyo wa tamaa. 
Nilipochunguza kwa kusoma vitabu vya kisayansi
 nikagundua kuwa Moyo ndiyo kiungo cha kwanza kuishi 
na cha mwisho kufa 
kwa binadamu,
ndio maana kimepewa nafasi hiyo.
Kutokana na kiungo hiki kubeba matukio mengi muhimu katika maisha yetu ni vyema tukakitunza.

Hivi ni kweli moyo huvunjika?
Kisayansi haiwezekani,
lakini amini usiamini,
 kihisia ni kweli moyo unavunjika.
Na mtu ambaye inasemekana moyo wake umevunjika,
raha ya maisha kwake haipo.
Kuna matukio yanayoongoza kuvunja mioyo ya binadamu,
Hebu tuyaangalie na tuanze kuyakwepa:

1.KURUHUSU WATU WABATILISHE UNAVYOJISIKIA

Kama kuna kitu unajisikia, 
ni kweli ndivyo kilivyo.
Hakuna kingine watu watakachosema 
chenye uwezo wa 
kubadilisha hilo.
Hakuna anayeishi ndani yako 
zaidi ya wewe mwenyewe.
Hakuna anayeweza kuelezea hisia zako
 zaidi ya wewe mwenyewe,
usiruhusu mtu akuhukumu kwa ulilofanya kwa kuwa hajui ulikuwa katika hali gani.
Usiruhusu watu wakuaminishe tofauti na wewe unavyojisikia.

2.KUJUTIA KILA KOSA

Yaani
 kama mpaka leo bado unaendelea
 kujutia kosa ulilofanya muda mrefu uliopita unajivunja moyo wako.
Kumbuka katika kipindi ulichokosea,
 ulifanya kutokana 
na uelewa na uzoefu uliokuwa nao 
muda ule na sio sasa.
Yawezekana kabisa,
 uchanga wa akili 
ndio ulikufanya ufanye vile 
ulivyofanya, 
na ndio maana kama ungepewa nafasi ya leo kufanya maamuzi
 uliofanya miaka iliyopita 
usingefanya  kama vile hata kidogo.
Muda na uzoefu vinatupa nafasi ya kufanikiwa katika yale tunayoyafanyia maamuzi,
kwa hiyo sahau yaliyopita songa mbele.

3.KUWAPOTEZEA WANAOKUPENDA

Unajua 
kuna kipindi unakuwa na watu
 wanakuonyesha upendo halafu wewe unashindwa kuwaonyesha shukrani.
Hii ni sawa na 
kujiandalia bomu ambalo litakuja 
kukulipukia siku ile watakapoondoka kabisa machoni pako.
Na kuna kipindi,
 utatamani angekuwepo karibu yako umueleze unavyojisikia 
au akikusaidia shughuli fulani.
Unatakiwa umuonyeshe shukrani yule anayekufanyia upendo kila muda utakaopata.

4.KURUHUSU MATAMANIO KUKUTAWALA

Kuna kipindi tunafanya uamuzi mbaya,
 sio kwasababu ni wabaya ila 
ni kwasababu 
tumejali zaidi kuwafurahisha wengine 
kuliko fahari yetu.
Unapokubali 
kufanya uamuzi wa tamaa ya kutaka
 uonekane mtu fulani 
ni 
kujitengenezea uasi wa ndani.

5.KUTAKA KUBISHANA KILA HOJA

Kuwa shujaa sio kupigana kila vita 
inayokuja mbele yako,
 au 
si kujibu kila shutuma dhidi yako.
Kama unaona hilo jambo
 litakushushia heshima na utu wako,
 ni heri ukaachana nayo ili yasiweze kuzaa mengine mapya
 na mabaya zaidi.


6.KUHARAKISHA UHUSIANO

Uhusiano 
mzuri ni wa watu ambao kila mmoja
 amempokea mwenzake kwa hali yake 
aliyonayo, 
na kumsaidia atoke 
hapo alipo kwenda katika hali 
iliyobora zaidi ya aliyomkuta nayo.
Usikimbilie
 kuwa katika uhusiano na mtu kwa kuwa, mazingira au 
nafasi imetokea tu.
Tafuta mwenza ambaye atakuhimiza kukua,
asiyeng'ang'ania ufanye 
anachopenda yeye kila wakati,
atakayekuruhusu uchangamane na watu wengine, na atakayekuamini.

7.KUMNG'ANG'ANIA ANAYETAKA KUONDOKA

Ni uchungu sana,
 kumuaga mtu unayetaka abaki,
lakini ni maumivu zaidi kumng'ang'ania anayetaka kuondoka.
Kama unayemuonyesha upendo na,
 hataki kurudisha upendo kwako
 usikae kulazimisha kwani utaendelea kujiumiza tu na
 kuwa mtumwa kwake.
Mtu pekee unayepaswa kuwa naye ni yule anayekuheshimu na anatambua umuhimu wako katika maisha yake.

8.KUKATAA KILA USHAURI 

Si kila
 ushauri utakao pewa 
utakuwa sahihi sawa,
lakini 
si kila ushauri utakuwa mbaya kwako.
Kubali kupokea
 marekebisho kutoka kwa watu
 wengine.
Usijitengenezee mazingira ya kuja kuuvunja moyo wako siku zijazo kwa kujuta.

RAHA YA MAISHA NI KUISHI KWA AMANI NA FURAHA,
KAMA UTAENDELEA KUJIWEKA 
KATIKA MAZINGIRA YA KUJA 
KUUVUNJA MOYO WAKO,
 HAUTAONA LADHA 
YA MAISHA KAMWE.

ANZA LEO KUUTUNZA MOYO WAKO.
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger