Home »
» Tanzania 1-1 Mozambique
Tanzania 1-1 Mozambique
Written By Koka Albert on Wednesday, February 29, 2012 | 8:06 AM
Timu ya taifa ya Tanzania imeshindwa kufua dafu mbele ya wageni wao Mozambique baada ya kulazimishwa sare ya goli moja kwa moja kwenye uwanja wao wa nyumbani. Shukrani zimuendee mchezaji anayechezea nafasi ya kiungo wa timu hiyo mwenye kipaji cha hali ya juu, Mwinyi Kazimoto kwa kutufungia bao hilo pekee ambalo lilikuwa la kusawazisha dakika chache kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika,.. kwa matokeo haya Stars itawalazimu kushinda,au kupata matokeo ya sare ya magoli zaidi ya mawili katika mchezo wa maruduano ili kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele katika mashindano hayo.
+ comments + 1 comments
Sasa hapo mazoezi yakutosha yanaitajika kwani bila hivyo itakuwa ni balaa, big up sana kwa Mwinyi kazimoto
Post a Comment