BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

YAH: KUFUTA MIKATABA NA KUSIMAMISHA KUUZA MUZIKI WA BONGO FLEVA,GOSPEL,DANSI NA TAARABU KWENYE MITANDAO YA SIMU.

Written By Koka Albert on Tuesday, July 31, 2012 | 7:07 AM

Husika na kichwa cha habari hapo juu, 

Kwa ujumla wetu sisi Wasanii toka Tanzania tunaofanya muziki wa Gospel, Rhumba , Taarabu pamoja na Bongo fleva tumeamua kutoa agzio kwenu la kusimamisha mauzo ya kazi zetu za muziki katika mtindo wa Ringtone na Callertunes katika mitandao ya simu ya Vodacom, Zantel,Tigo na Airtel na kufuta mkataba tuliosaini kati yetu sisi Wasanii na Kampuni yako mpaka hapo tutakapokaa sisi kama wasanii, nyinyi kama wasambazaji wa muziki wetu, pamoja na Mitandao ya simu ili kuzungumzia namna mpya ya sisi na nyinyi tutakavyofanya kazi. 

Sababu ya sisi Wasanii kusimamisha na kufuta mikataba kati yetu na wanaofanya biashara ya kuuza maudhui yetu ni pamoja kampuni husika kushindwa kuweka wazi taarifa za mauzo ya nyimbo pamoja na kutolipa katika muda husika kama ilivyoanishwa katika mikataba husika.


Sababu ya pili ni mitandao ya simu kuchukua kiasi kikubwa cha fedha ambacho ni asilimia themanini ya mauzo yote ya maudhui yetu, jambo hili linatuumiza na limetufanya tuendelee kuishi kwa kutegemea aina moja ya pato toka kwenye shoo.

Hivyo tumeziagiza kampuni zote zinazofanya kazi ya kuuza maudhui yetu kutoa maelekezo kwenye mtandao husika kuwaelekeza kusimamisha mauzo ya kazi zetu za sanaa ndani ya siku saba kuanzia leo tarehe 30/07/12 ikiwa pamoja na kusimamisha matangazo yote yanayotangaza mauzo ya kazi zetu kwa njia ya Television , Radio , blogs, website, Magazeti na Ujumbe Mfupi wa maneno mpaka hapo tutakapofikia muafaka.

Jumla ya wasanii 153 wameshasaini barua hizo na wengine wanaendelea kusaini.

Mwisho tunawashukuru kwa ushirikianao wenu, na tunaambatanisha sahihi zetu ili kuonyesha uthibitisho wa umoja wetu katika jambo hili.

Asante.

Vituko vya familia ya ngariba

Written By Koka Albert on Sunday, July 29, 2012 | 12:00 AM

Wankyo Mwikwabe akiwa na mume wake Mwikabe Mwita Magesa.
WAILALAMIKIA SERIKALI KUZUIA UKEKETAJI,WADAI KAZI ILISAIDIA KUSOMESHA WATOTO
Anthony Mayunga
MKOA wa Mara ni miongoni mwa mikoa nchini inayotajwa kuongoza kwa matukio ya vitendo vya ukeketaji wanawake, hususan watoto wadogo.
Pamoja na juhudi za Serikali na mashirika mbalimbali ya kijamii kutoa elimu dhidi ya mila hizo potofu, bado vitendo hivyo viliendelea kufanywa, ama kwa siri au wakati mwingine hadharani kabisa.

Hata hivyo, juhudi hizo sa Serikali na mashirika binafsi zimeonesha kuzaa matunda kwa baadhi ya wahusika kukiri kuacha kufanya vitendo hivyo baada ya kupata elimu ya kutosha juu ya madhara ya ukeketaji kiafya.
Katika kijiji cha Nyanchabhakenye, Kata ya Kisumwa, Wilaya Rorya, mkoani Mara nakutana na Wankyo Mwikwabe (64) maarufu kama Chunguza.
Mama huyu amekuwa Ngariba kwa zaidi ya miaka 20, na baada ya kupata elimu ya kutosha juu ya athari za ukeketaji, sasa ameamua kustaafu kazi hiyo iliyokuwa ikimuingizia kipato. Hata hivyo uamuzi wake kwa upande mwingine umekuwa mwiba kwa familia yake, hasa mume wake, Mwikwabe  Mwita Magesa(66).

Bila kuficha hisia zake Magesa anasema, “Kama si mkazo wa Serikali kupiga marufuku ukeketaji, mke wangu alitakiwa kuendelea maana kazi hiyo ilisaidia kipato cha familia, tulisomesha watoto ,chakula kizuri lakini sasa ndivyo hivyo mmeishaamua tutafanyaje.”

Anabainisha kuwa, uamzi wa Serikali wa kupiga marufuku ukeketaji umepelekea athari kiuchumi kwenye familia hiyo lakini pia imekuwa changamoto ya kujipanga kuhakikisha familia haiyumbi kiuchumi.

“Mimi nilikuwa napata vitu kutoka kwa mke wangu, kila alipokwenda tuliongozana ,kama ni pombe akipewa ananipa, chakula tulitengewa kizuri maana aliheshimiwa sana kila anakopita,” anasema Magesa.

Anabainisha kuwa, kazi ya ungariba aliyokuwa akifanya mke wake, ilichangia kupata wateja wengi na mapato kuongezeka ambapo walifanikiwa kusomesha watoto.
Hatahivyo anasema hawakuweza kufanya mambo mengi ya maendeleo kwa kuwa fedha hizo zina masharti magumu .

“Mapato yatokanayo  na ukeketaji yana masharti magumu sana ,huwezi kununua mifugo wala kufanyia biashara zaidi ya kula na kuvaa ,yalitusaidia kusomesha hata watoto wetu…,sheria hizi zimetuathiri,”anasema.

Hata hivyo, Magesa anasema anakubaliana na uamuzi uliofikiwa na mke wake wa kuachana na kazi ya ungariba na kuomba Serikali kufanya utaratibu wa kuwawezesha mangariba waliokuwa wakitegemea kazi hiyo kuendesha maisha yao.

Mtoto wao, Mwita Mwikwabe(26), anasema kazi ya mama yake iliwasaidia kupata kipato kikubwa kwani yeye alikuwa akikodiwa kupiga muziki wa asili kila mama yake alipokuwa kwenye shughuli ya ukeketaji.

“Nilikuwa napata mialiko mingi sana na ikizingatiwa kuwa mama ndiye alikuwa ameshika soko la ukeketaji,nilikuwa nalipwa kati ya Sh100,000 hadi Sh150,000,” anasema.
Hata hivyo kijana huyo anabainisha kuwa muziki wake si mahususi kwa shughuli za ukeketaji pekee, na kuongeza kuwa alikuwa akipata mialiko mingi kupitia umaarufu wa mama yake.

Ngariba anena
Wankyo mwenyewe adai hakujua kama ukeketaji una madhara na kuongeza kuwa anajisikia amani sana kuachana na kazi ya ukeketaji baada ya kupata elimu kwa kuwa aliifanya kama kudumisha mila na desturi bila kujua madhara kwa aliokuwa akiwakeketa.

“Mimi niliwakeketa kwa utalaam na walikuwa wanapona haraka na wanawahi kuolewa na hata kuzaa mapema …nilipata sifa kubwa nikabatizwa jina la Chunguza kwa kuwa niliwachunguza na kuwatengeneza vizuri,” anasema mama huyo.

Kutokana na ongezeko la wateja anasema aliweza kupata kati ya kati ya Sh200,000 hadi 300,000 kwa msimu mmoja wa ukeketaji kwani alikuwa akitoza Sh5,000 kwa kila mtu. Anaongeza kuwa wanawake walioolewa walikuwa wakitozwa bei kubwa zaidi, tofauti na wale ambao walikuwa hawajaolewa. “Wanawake walioolowa na kuzaa niliwatoza Sh10,000 hadi Sh15,000 kwani ilikuwa kazi sana kuwatahiri kwasababu walishafanya tendo la ndoa tayari.

Kuwa Ngariba
Anasema ameanza kazi ya ungariba mwaka 1990  baada ya kile alichokieleza ni kusumbuliwa na ndoto za ajabu usiku. “Baada ya kudumu kwa ndoto hizo kwa muda, nilienda kwa kwenda kwa waganga wa jadi nikapiga ramli na kuniambia marehemu bibi yangu ndiye ananitaka nianze kazi yakukeketa,”anasema.

Aliowakeketa
Ngariba huyo anasema kwa miaka 10 aliyofanya kazi hiyo, ameshakeketa watoto na wasichana zaidi ya 2000. Anafafanua kuwa ameamua kuacha kazi ya ungariba baada ya Serikali kulivalia njuga suala hilo na kupiga marufuku vitendo vya ukeketaji, pia mafundisho ya dini yalichangia kumfanya aweke vifaa vya ukeketaji chini mwaka 2010.

 “Uamuzi wa kuacha uliridhiwa na familia kwa kuhofu kukamatwa na kufungwa kwa kuwa elimu ya kupinga vitendo hivyo ikawa kila kona,nikaamua kwenda Kanisa Katoliki huko Baraki nikaanza mafundisho ili nibatizwe,”anabainisha. Hata hivyo hajawahi kubatizwa kutokana na kufuatwa na mizimu kila wakati usiku na kumfanya akate tamaa.

“Shetani ananifuata sana nakunizuia kubatizwa, ananitaka niendelee kukeketa ,naomba  aniachie lakini ananibana sana sijui anataka nifungwe,”anasema kwa unyonge.

Jogoo mwenye shanga, hirizi azua kizazaa

Written By Koka Albert on Saturday, July 28, 2012 | 11:53 PM

WAKAZI wa Mtaa wa Nyanchenche Road mjini Sengerema juzi walifurika kushuhudia tukio la  kuonekana jogoo asiye na manyoya akitembea huku akiwa amefungwa shanga na hirizi mbili shingoni na mabawa yake yakiwa yamechanjwa chale na kupakwa dawa nyeusi.

Tukio hilo lililovuta umati wa watu lilitokea juzi  saa 7:00 mchana kwenye moja ya familia ya mtaa huo[jina limehifadhiwa]ambaye alidai kwamba kuku huyo alijitokeza nyumbani kwake bila kufahamu alikotokea.

Kuku huyo wa ajabu alikutwa na wananchi katika mji huo ulioko  kando kando ya barabara,jambo lililowashtua wakazi wa Sengerema waliofika kulishuhudia huku wakilihusisha na imani za kishirikina.

Katika tukio hilo hakuna  mwananchi aliyejitokeza kumshika kuku huyo,  huku wenyeji wa mji husika wakiendelea na shughuli zao licha ya kuonyesha mshituko.

Akizungumza na waandishi wa habari,Mwenyekiti  wa kitongoji hicho Leah James alieleza kushangazwa na tukio hilo aliloliita la ajabu, na kwamba halijawahi kutokea  katika kitongoji hicho kwani limeibua hisia tofauti miongoni mwa wanajamii.

รฌNimepata taarifa za tukio hili ilikuwa mchana muda wa saa saba na tumefika mpaka eneo la tukio, kwa kweli inashangaza na kusikitisha, huyo kuku wa ajabu hana nyoya hata moja wala alama ya kidonda na amechanjwa chale kwenye mbawa zake,kavishwa hirizi mbili shingoni na amefungwa shanga kwenye mbawa zakeรฎalisema mwenyekiti.

Baada ya tukio hilo uongozi wa eneo hilo na sungusungu uliamua kuitisha mkutano siku iliyofuata leo(jana) ambapo walifuatilia na kumbaini mmiliki wa kuku huyo kuwa ni  Leticia Makoye ambaye alidai kuku huyo ni wake na  humtumia katika shughuli za uganga wa kienyeji .

Kikao hicho kiliamua kumrudishia kuku huyo ingawa alikuwa tayari amekufa kutokana na kupigwa baridi usiku kucha,maamuzi yaliyopingwa na wananchi na hivyo kulazimika kumshambulia kwa mawe hadi nyumbani kwake huku viongozi wa mtaa huo wakimpatia ulinzi hadi alipoingia ndani ya nyumba.

Baadhi ya wananchi waliozungumza eneo la tukio wamekuwa na hisia tofauti huku baadhi yao wakilihusisha na imani za kishirikina kutokana na vitu alivyokutwa navyo kuku huyo ikiwa ni pamoja na shanga,hirizi,na chale alizochanjwa kwenye mbawa zake.

Grece Michael (32), Fadhili Alfani (45), na Daniel Marco walisema  matukio ya ajabu kama hilo ni dalili za mwisho wa dunia kutokana na vitendo vya kishirikina kuongezeka na kwamba njia pekee ya kuepukana navyo ni kudumu katika sala na imani.

NEW HIT BY HUSSEIN MACHOZI-ADDICTED

Linex Aifola Official Video

Baghdad Official video-Tom boy

Watch new video by Ben Pol-Maneno

Wale watoto kwenye video yangu sio wa mtaani

Kitaani kumeibuka tetesi kwamba wale watoto walioonekana kwenye video mpya ya Ben Pol inayoitwa MANENO kuwa wale ni watoto wa mtaani. Sasa kutokana na maswali kuwa mengi nikabidi nimtafute Ben Pol na kumuuliza juu ya hili na yeye akanijibu hivi...Namnukuu
"Wale watoto kwanza amewatafuta producer wake Karabani, mimi nilichokifanya nilimlipa gharama zote za kila kitu, na yeye ndo aliyekwenda kuongea na wazazi wa wale watoto mnaowaona halafu wale sio watoto wa mtaani wale wana nyumbani kwao wale na wawili pale ni ndugu  so walitengenezwa tu kidizaini,"

Nikamuuliza je vipi ulipata nafasi ya kuwaona au kukutana nao maana kwenye ile video kama umeonekana vipande vichache sana tofauti na video zingine anaonekana mwanzo mwisho
"Yeah niliwaona na nikapiga nao story na pia wao walikuwa wanatamani kuniona, na siku moja tulishoot wote, kama video ukiitizama pale darajani mimi nilikuwa juu ya daraja na wao walikuwa kwa chini. Kuonekana ndio nilionekana kidogo ili kuweka maana ya wimbo kwa kuonekana vitendo wafanyavyo watoto wa mtaani ambao ni yatima"

Sheria mpya mifuko ya jamii yazua mtafaruku nchin

Written By Koka Albert on Wednesday, July 25, 2012 | 12:31 AM

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Nicolaus Mgaya
Marekebisho ya Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya 2012 yaliyofanywa na Bunge yamezua mtafaruku na sintofahamu, huku wafanyakazi wa sekta mbalimbali wakiyapinga kwa maelezo kwamba ni kandamizi na yanalenga kuwanyima haki ya fedha wanazokatwa kwa mujibu wa sheria kuchangia mifuko hiyo.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Nicolaus Mgaya aliliambia gazeti hili jana kuwa, watafungua kesi katika Mahakama ya Kazi nchini, kupinga hatua ya Serikali kubadili Sheria ya muda wa lazima wa kuchukua mafao hayo ambao ni kati ya miaka 55 na 60.

Tangu juzi watu kutoka sehemu mbalimbali hasa jijini Dar es Salaam wamekuwa wakipiga simu katika chumba cha habari cha Mwananchi kwa lengo la kupata ufafanuzi wa mabadiliko hayo ya sheria yaliyopitishwa na mkutano wa saba wa Bunge, Aprili 13 mwaka huu.

Kadhalika sheria hiyo inayozuia mwanachama wa mfuko wowote wa hifadhi ya jamii kuchukua mafao kabla ya umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria ambao ni miaka 55, lilichukua nafasi kubwa katika mijadala ya mitandao ya kijamii ambako wengi wa wanaliochangia, wameiponda sheria hiyo na kuiita kuwa ni ya ‘kinyonyaji’.

Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Irene Isaka alisema jana kuwa: “Hakuna haja ya watu kuwa na wasiwasi, maana sheria hii itafuatiwa na kanuni na miogozo mingine ambayo ninaamini kwamba itaondoa wasiwasi uliopo”.
Isaka alisema miongoni mwa mambo yatakayozingatiwa katika miongozo hiyo ni iwapo mwanachama atafukuzwa au kuachishwa kazi, wanachama ambao wako kwenye kazi za mikataba na wale wanaopata ulemavu wa kudumu wakiwa kazini.

“Kimsingi ni kwamba suala la mafao ya kuacha kazi kabla ya umri wa kisheria wa kustaafu limefutwa kwa mifuko yote, isipokuwa katika mazingira hayo niliyoyaeleza litawekewa miongozo, na hii ni kwa faida ya wachangiaji,”alisema Isaka.

Alisema baada ya sheria hiyo kuwa imepitishwa na Bunge, kisha kusainiwa na Rais Jakaya Kikwete mwezi Juni mwaka huu, SSRA ilianza mchakato wa kuweka miongozo na baada ya hapo kinachofuatia ni kutoa elimu kwa umma na baadaye kuanza kutumika kwake rasmi.

“Lakini sasa tumelazimika kuanza kutekeleza sheria hiyo mapema kuliko tulivyopanga hasa baada ya kutokea kwa suala hili kwenye public (umma) kabla ya muda tuliokuwa tumekusudia,”alisema mkurugenzi huyo.

Isaka aliongeza kuwa chimbuko la sintofahamu iliyojitokeza ni baadhi ya mifuko kuchezeana rafu kwa lengo la kupata wanachama wapya kwenye migodi na kwamba wao kama wadhibiti tayari wametoa onyo kwa mifuko iliyohusika.

“Kwanza hakuna mfuko wowote ambao una mamlaka ya kutangaza kuanza kutumika kwa sheria, ni SSRA tu wenye mamlaka hayo, kwa hiyo tumewapa onyo, kama wanajitangaza wajitangaze kwa kueleza uzuri wa mfuko wao ni siyo kuchafuana au kuchafua wengine,” alisisitiza.
Wasemavyo wafanyakazi
Mgaya alisema sheria hiyo ni kandamizi kwani inamnyima fursa mfanyakazi aliyestaafu au kufukuzwa kazi kupata malipo yake ambayo ni halali.

“Sheria hii sisi hatuikubali na tunaipinga kwa nguvu zote na tutakwenda Mahakama ya Kazi kufungua kesi ya kupinga kutumika,” alisema Mgaya na kuongeza:

“Tutafanya mawasiliano na Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii kuwaeleza kuhusu sheria hii ili watusaidie na ikishindikana azma yetu ni kwenda mahakamani.”
Katibu Mkuu huyo alifafanua kwamba haiwezekani mtu anafukuzwa kazi akiwa na miaka 45 na baadhi yao hawataki tena kuajiriwa wanataka kufanyabiashara halafu unamnyima mafao yake hadi afikishe miaka 55,  kitu ambacho kitamfanya mtu huyo aishi maisha magumu.

“Sheria hiyo ingekuwa na usawa ingetumika kwa wafanyakazi wote wa Serikali na kutowabagua kama inavyojieleza kwamba, Mbunge akimaliza miaka yake mitano anachukua mafao yake. Sasa  kwa nini iwe kwao tu na si kwetu pia?,” alihoji Mgaya.

Kwa upande wao Chama cha Wafanyakazi wa Migodini (Tamico) Wilaya ya Geita, kimesema kitapeleka maombi maalumu kwa Rais Kikwete kupinga marekebisho ya Sheria ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
Katibu wa Tamico Wilaya ya Geita, Benjamin Dotto alisema wameamua kupiga kura ya maoni juu ya mabadiliko ya sheria hiyo, ili wanachama wao waamue wenyewe kama wanaitaka au la.

”Tunamwomba Rais aagize kupelekwa muswada wa marekebisho bungeni, kwa ajili ya  kipengele ambacho kimeleta mtafaruku,” alisema Dotto.

Alisema kipengele cha kuzuia mfanyakazi kuchukua mafao yake hadi afikishe umri wa miaka 55, kinakandamiza masilahi ya mfanyakazi mnyonge ambaye kwa kiasi kikubwa amekuwa akichangia mapato ya nchi kupitia kodi anayokatwa.
Chimbuko la sheria
Mabadiliko ya sheria hizo za mifuko ya hifadhi ya jamii yalifanywa na Bunge Aprili 13 mwaka huu, baada ya muswada husika kuwa umesomwa kwa mara ya kwanza bungeni Februari 1, 2012.

Ibara ya 107 ya muswada huo ndiyo ilipendekezwa kufutwa kwa Ibara za 37 na 44 za Sheria ya Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF) ambavyo vilikuwa vikiruhusu mafao ya kujitoa.

Meneja uhusiano wa SSRA Sara Mssika alisema jana kuwa kufutwa kwa ibara hizo kulimaanisha kwamba hakuna mfuko wowote unaoruhusiwa kutoa tena mafao ya aina hiyo hadi hapo miongozo mipya itakapotolewa.

“Hakuna sheria ya mfuko mwingine iliyokuwa ikiruhusu mafao ya kujitoa, na kama wapo waliokuwa wakifanya hivyo, basi walikuwa wanafanya hivyo pengine kwa taratibu nyingine ambazo ni nje ya sheria za kuanzishwa kwa mifuko yao,”alisema Mssika.

Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka akiwasilisha maelezo ya muswada huo bungeni alisema lengo la marekebisho katika Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ni kuiwezesha SSRA kufanya kazi yake kikamilifu na kusimamia na kudhibiti Sekta ya Hifadhi ya Jamii.

Alisema muswada huo uliandaliwa kwa kuwashirikisha wadau wote wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii, wakiwamo wafanyakazi, waajiri na Serikali, pia
mifuko yenyewe kupitia vikao vya wadau na Baraza la Ushauri wa Masuala ya Kazi Jamii na Uchumi.

“Kimsingi, wadau wote waliunga mkono mapendekezo yaliyomo katika muswada huu,” alisema Kabaka na kuongeza kuwa mabadiliko hayo yatawezesha kupanuliwa kwa wigo wa wanachama kwenye mfuko kwa kuruhusu wafanyakazi wanaoingia kwenye ajira kwa mara ya kwanza ama kujiajiri wenyewe ili waweze kujiunga.

Gari la askari polisi lakamatwa na nyara

Written By Koka Albert on Thursday, July 19, 2012 | 6:16 AM

Daniel Mjema,Moshi
 POLISI katika mji mdogo wa Himo, mkoani Kilimanjaro, wamefanikiwa kulikamata gari aina ya Toyota Noah, linalomikiwa na askari mmoja wa polisi likiwa na shehena ya pembe za ndovu.

Taarifa za uhakika zilizopatikana jana, zilisema gari hilo linalomilikiwa na askari  polisi mwenye cheo cha koplo lilikamatwa saa 2:00 asubuhi nje kidogo ya mji wa Himo.

Ofisa mmoja mwandamizi wa polisi, aliliambia gazeti hili kuwa gari hilo lililokuwa na abiria 10, liliondoka katika mji mdogo wa Tarakea wilayani Rombo, kwenda mjini Moshi.

Alisema baaada ya kufika eneo hilo, lilisimamishwa na polisi wa kikosi cha kudhibiti magendo wakishirikiana na trafiki na lilipopekuliwa lilikutwa na vipusa hivyo.

“Hizo pembe zilikuwa kwenye mifuko ya kuhifadhidia mboea,  hivi tunavyozungumza gari limeletwa hapa kituo cha kati cha polisi na abiria waliokuwa katika gari hilo wanahojiwa,”alisema.

Wilaya ya Rombo inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Tsavo, nchini Kenya na haikufahamika  kama nyara hizo za Serikali zilitokea huko au katika hifadhi ya jirani ya Amboseli nayo ya Kenya.

Hata hivyo wakati gari hilo likikamatwa, polisi huyo anayefanya kazi katika Kituo cha Polisi cha Tarakea, hakuwamo katika gari hilo lakini baada ya kuarifiwa alitoa ushirikiano kwa polisi.

Taarifa nyingine zilisema awali polisi walikuwa wamedokezwa kuwa gari hilo lilikuwa libebe waharamiaji haramu kutoka nchini Somalia, lakini hadi kufika subuhi mtego haukufanikiwa.

Kamanda wa Polisi mkoani ilimanjaro, Robert Boaz, alikiri kuwapo kwa tukio hilo lakini akaahidi kulitolea ufafanuzi kwa njia ya ujumbe mfupi (sms) kwa vile alikuwa ziarani.

“Hilo tukio lipo lakini kwa sasa niko kwenye msafara ngoja nikuandikie kwa meseji” alisema Kamanda Boaz.

BOTI YAZAMA NA ABIRIA 250, KATI YAO 60 WAHOFIWA KUFARIKI DUNIA

Askari wa vikosi vya Ulinzi na Usalama wakiwa wamebeba moja ya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya boti ta Stargic iliyotokea jana karibu kabisa na Unguja.Picha na Ramadhan Othman
WATU 60 wanahofiwa kufa maji na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya boti iliyokuwa imebeba abiria wanaokadiriwa kufikia 250 ikitokea Dar es Salaam kwenda Unguja, Zanzibar kuzama baharini.Hii ni ajali ya pili mbaya kutokea katika kipindi cha miezi 10 tangu ilipotokea nyingine ya Meli ya Mv Spice Islander ambayo inakadiriwa kuwa watu wapatao 200 walifariki dunia.Boti hiyo iliyoondoka jana Dar es Salaam majira ya saa 6:00 mchana na kutarajiwa kufika Bandari ya Malindi, Zanzibar saa 9:30 jioni, ilizama eneo la Pungume karibu kilomita 48 kutoka Bandari ya Zanzibar.
Inaelezwa kuwa, ilianza kuzama saa 7:30 mchana kutokana na kupigwa na mawimbi mazito ya bahari.

Hata hivyo, Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu wa Zanzibar, Hamad Masoud Hamad alithibitisha vifo vya watu 12 hadi vilivyoripotiwa ilipotimu saa 12:30 jioni jana wakati kazi ya uokoaji ikiwa inaendelea.

Baadaye saa 1:00 Ofisa Habari na Mawasiliano wa Wizara hiyo, Nafisa Madai aliwaambia waandishi wa habari kuwa idadi hiyo ilikuwa imeongezeka hadi kufikia 24 na majeruhi walikuwa 145.Madai alisema wakati boti hiyo inaondoka Dar es Salaam, ilikuwa na abiria 250 wakiwamo watoto 31 na wafanyakazi tisa.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Said Shaaban akizungumzia ajali ya boti hiyo ya Mv Skad, inayomilikiwa na Kampuni ya Meli Seagull alisema: “Vikosi vya uokoaji tayari vinaelekea katika eneo hilo ili kusaidia majeruhi na kufuatilia yaliyotokea.”

Maofisa kadhaa wa Serikali wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi walifika Bandari ya Malindi na Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu Zanzibar, Hamad Masoud Hamad aliongoza msafara wa viongozi wengine kwenda katika eneo la tukio.

Awali, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alisema kuwa, hadi alipopata taarifa, watu waliokuwa wamefariki dunia ni saba na 124 ndiyo waliokuwa wameokolewa. Alisema meli hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 300 na waliosafiri siku ya tukio hawazidi 250.

Awali, taarifa zilieleza kuwa watu 10 waliokolewa na maiti zaidi ya 60 zimenasa katika boti hiyo na kuvifanya vikosi vya uokoaji vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi na KMKM kupata wakati mgumu kwenye zoezi la uokoaji.Kazi ya kuokoa maisha ya watu waliozama kwenye boti hiyo na kuopoa maiti ilifanywa kwa kutumia boti nne zikiwamo za Serikali na zile zinazomilikiwa na Kampuni ya Azam Marine.
Hata hivyo, ilielezwa kwamba boti za polisi zilichelewa kwenda katika eneo la tukio kutokana na kukosekana kwa mafuta.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kufika bandarini, Balozi Seif aliwataka wananchi kutulia na kusubiri wakiwa nyumbani wakati Serikali ikifanya juhudi za uokoaji.
Shughuli nyingi za usafiri zilivurugika kutokana na tukio hilo na Meli ya Mv Sea Bus ililazimika kufuta safari zake kupisha kazi hiyo ya uokoaji.
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imesema inafuatilia tukio hilo kwa karibu ili kubaini chanzo.
Ofisa Uhusiano wa Sumatra, David Mziray alisema jana muda mfupi baada ya ajali hiyo kuwa, wanawasiliana na Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Majini (MRCC), ili kupata taarifa kamili kabla ya kuujulisha umma.
Spika Makinda achafua hali ya hewa

Kutokana na ajali hiyo, muda mfupi baada ya kipindi cha jioni kuanza, Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed alisimama na kuomba mwongozo kwa kutumia Kanuni ya 47(3) kulitaka Bunge lipitishe Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mafungu bila ya kutolewa ufafanuzi ili wabunge waweze kupata muda wa kujadili tukio hilo.
Hata hivyo, Spika Anne Makinda alipinga hoja ya Hamad na kutaka Bunge liendelee akieleza kwamba kanuni hiyo imekuwa ikitumiwa vibaya na kwamba tayari ameshawasiliana na waziri husika na kwamba taarifa kamili zitakapopatikana angelitaarifu Bunge.
Baada ya kauli hiyo Spika Makinda aliruhusu shughuli za Bunge ziendelee na kumwita Silima kutoa ufafanuzi wa hoja za wabunge.

Lakini wakati Naibu Waziri huyo akielekea kutoa hotuba yake, wabunge wote wa CUF, Chadema na baadhi wa CCM walitoka nje na kwenda katika Ukumbi wa Msekwa ili kupeana taarifa za ajali hiyo na kupanga mikakati ya jinsi ya kutuma ujumbe wa haraka kwenda Zanzibar kushirikiana na waokoaji.
Ukumbi huo uligeuka kuwa wa maombolezo kwa muda baada ya wabunge wengi kuangua vilio pale walipopewa taarifa rasmi za ajali hiyo.

Jali muda kustawisha bishara yako

Written By Koka Albert on Friday, July 13, 2012 | 12:07 AM

Staphord Kwanama
MUDA ni rasilimali muhimu katika biashara. Kwa lugha ya ujasiriamali, muda ni kipimo kizuri cha kujua kama kweli wewe ni mjasiriamali au mbabaishaji.

Fikiria chini ya jua, kila mtu bila kujali jinsia katika muda wa saa 24, kuna watu wanafanikiwa na kuna watu mambo yao hayaendi kabisa.

Kwa kuzingatia ukweli kwamba muda ni rasilimali muhimu kwako wewe mjasiriamali. Kwa kuwa muda ni muhimu,  tathimini namna unavyotumia muda wako. Kwa mfano, kama unatumia muda wa kutosha kwa shughuli za kukuingizia fedha au unatumia kwenye bla bla na porojo tu. Ainisha ni mambo gani ambayo siyo ya msingi sana kwako huingilia muda wako mara kwa mara na yanatokana na nini.

Vidokezo vya namna ya kutumia muda wako vizuri; jipangie muda maalumu wa kumaliza jambo na hakikisha unakuwa na msimamo kumaliza jambo hilo ndani ya muda ulojipangia, unaweza kujipongeza endapo umemaliza kwa wakati.

Kwa mfano, pumzika dakika kadhaa kwa kunywa kiburudisho unachokipenda.

Jipangie kipaumbele kwa shughuli ulizonazo, ipi ianze kwanza na ipi ifuate na ipi iwe ya mwisho. Hakikisha unafanya kitu kimoja kwa wakati, usichanganye mambo mara umeshika hiki mara kile, mwisho wa siku, mwezi hata mwaka utajikuta hujafanya jambo lolote.

Katika ofisi yako weka taratibu na sera kuhusu kujali muda ili eleweke kwa kila mmoja ofisini. Mathalani unaweza kuwa na daftari la kuingia kazini na kutoka ili wafanyakazi wako wafike kwa wakati na pia iwe wazi wanatoka muda gani.

Pia hakikisha una kitabu cha kumbukumbu ya mikutano. Mjasiriamali anapaswa kuandika mambo mnayokubaliana kuhusu  wafanyakazi au wateja.

Katika hatua hii, itasaidia kutorudia rudia uamuzi ambao mmekubaliana awali na badala yake, mtakuwa na mambo mapya kuweza kusonga mbele.
Kasimu madaraka au majukumu kwa mfanyakazi mwingine ambaye unaona anaweza kufanya.

Acha kabisa kufanyakazi za watu wengine, kama umemwajiri inaamana unamlipa mshahara sasa iweje ufanye majukumu yake, sisitiza kila mtu afanye majukumu yake hii itaongeza uzoefu na ubunifu katika kazi, na hatimaye tija huongezeka.

Pia ainisha na fanya kazi kidogo muhimu kwa ufanisi kwa mfano, asilimia 20 ya kazi, lakini muhimu ambayo itakuzalishia asilimia 80 ya matarajio ya biashara yako.

Wataalamu wanashauri kufanya kazi zinazohitaji ujuzi na umakini wa hali ya juu wakati wa asubuhi. Usiache au kukatiza kazi bila sababu za msingi. Fika kazini kwako mapema. Pia jipumzishe walau saa moja baada ya kazi.

Pia weka utaratibuwa mtiririko maalumu katika kazi zako,  mathalani shughuli unayofanya leo lazima iwe na uhusiano na malengo ya siku inayofuta au iwe na malengo ya muda mrefu ya biashara yako.
Weka mambo yako wazi na taratibu nzuri za namna ya kila mtu katika biashara yako atatekeleza majukumu yake.
Jaribu kuainisha au kutumia teknolojia ya kisasa katika biashara yako ili kurahisisha kazi na kupunguza muda ambao ingefanyika bila nyenzo au teknolojia.

Kwa mfano,  badala ya kutuma mtu kupeleka barua sehemu fulani na kumlipa fedha, tumia kompyuta, mtandao wa barua pepe au nukushi ambao utakusaidia kufikisha ujumbe ndani ya sekunde tu na majibu kupatikana ndani ya muda mfupi. Teknolojia pia inategemeana na ukubwa wa biashara mathalani kama biashara ni ndogo unaweza kutumia excel katika kutunza kumbukumbu za hesabu na taarifa mbalimbali za biashara kama mauzo.

Lakini biashara inapokuwa kubwa unahitaji kutumia pakeji maalumu kama ya uhasibu.

Fanya biashara yako kitaalamu, muda ni mali, pangilia mambo yako kwa mizania na toa kipaumbele kwa shughuli za kibiashara zinazokuingizia fedha.

Pia jipangie muda kwa mfano, mara moja kwa mwezi kutathimini mwenendo mzima wa biashara yako na weka mikakati ya kuboresha.

Mbunge CCM atimuliwa bungeni

Written By Koka Albert on Thursday, July 12, 2012 | 11:18 PM

Neville Meena, Dodoma
NAIBU Spika wa Bunge, Job Ndugai amemwadhibu Mbunge wa Kigamboni (CCM), Dk Faustine Ndungulile kutohudhuria vikao vitatu mfululizo baada ya kushindwa kuthibitisha tuhuma kwamba madiwani wa Halmashauri ya Manispaa Temeke walihongwa ili kuukubali Mradi wa Mji Mpya wa Kigamboni.

Ndugai alitumia kifungu cha 73 (3) ambacho kinampa mamlaka ya kumwadhibu mbunge aliyeshindwa kuthibitisha tuhuma alizozitoa, huku pia akiwa amekaidi kufuta kauli yake kuhusiana na tuhuma hizo.

“Kwa kutumia kifungu namba 73 cha Kanuni za Bunge, hutahudhuria vikao vya Bunge mara tatu mfululizo, askari mtoeni nje,” aliagiza Ndugai.

Awali, Dk Ndungulile alishtakiwa na madiwani wanne wa Kigamboni kwamba aliwatuhumu kupewa rushwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ili waunge mkono mradi wa kuendeleza mji huo mpya wa Kigamboni.

Madiwani hao jana waliliandikia Bunge kukanusha tuhuma zilizotolewa na Dk Ndungulile kuwa walihongwa fedha na

Profesa Tibaijuka ili kufika bungeni

Katika malalamiko yao, madiwani hao ambao walihudhuria kikao cha Bunge hapo juzi wakati Bajeti ya Makadirio ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ikisomwa, walipinga madai ya Ndungulile kuwa wakazi wa Kigamboni wamemtuma na kuwa wanaupinga Mradi wa Mji Mpya wa Kigamboni.

Akisoma barua ya malalamiko ya madiwani hao  iliyowasilishwa bungeni, Ndugai alinukuu maandishi katika barua hiyo yaliyosema:

“Sisi madiwani tunakanusha taarifa zilizotolewa na mbunge wetu, Faustine Ndungulile kuwa tulipewa fedha ili kuja bungeni,” inasema sehemu ya barua hiyo.

Madiwani hao waliendelea kulalamika kwamba, matamshi yaliyotolewa na mbunge huyo yamewadhalilisha na kuondoa imani ya wananchi juu yao kama viongozi, na kuwa wanamtaka aifute kauli yake na kuwaomba radhi.

Sehemu ya barua hiyo pia ilisema hakuna diwani yeyote aliyefika bungeni hapo kwa kupewa fedha na mtu yeyote, bali kwa ridhaa yao wenyewe.

Baada ya kusoma barua hiyo, Ndugai alisema atamtaka mbunge huyo ama kuifuta kauli juu ya madiwani hao au kuthibitisha tuhuma hizo.

“Ndiyo maana, kila siku tunawaonya hapa tusitamke maneno tusiyokuwa na uhakika nayo, wakati mwingine yanaweza kutuweka matatani,” alisema Ndugai.

Juzi, Ndungulile aliipinga vikali Bajeti ya Wizara ya Ardhi  na kumtuhumu ProfesaTibaijuka kuwahonga madiwani hao ili waupigie debe mradi huo ilhali wakazi wa Kigamboni hawautaki.

Alipotakiwa kuthibitisha tuhuma hizo, Ndungulile alisema hakuwataja madiwani hao kwa majina bali alisema madiwani 43 ndiyo waliokuja kwa kuhongwa kwa kutumia fedha za wizara.

“Hata kanuni za Takukuru zinaonyesha kuwa walichokifanya kina mazingira ya waziwazi ya rushwa,” alisema Ndungulile.

 Alifafanua kwamba, mazingira hayo ya rushwa yanakuja baada ya waziri kuwaita madiwani wa Temeke badala ya madiwani wa jimbo lake la Muleba.

Mnyika naye matatani

Kwa upande wake Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika anakabiliwa na madai ya kumtuhumu Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba kwamba ni mmoja wa watuhumiwa wa wizi wa Fedha za Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).


Tuhuma dhidi ya Nchemba zilizotolewa na Mnyika, sasa zitapelekwa katika Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge inayoongozwa na Mbunge wa Mlalo (CCM), Hassan Ngwilizi.

Ndugai alitoa mwongozo huo baada ya Nchemba kuomba mwongozo bungeni, kwa kutumia Kanuni ya 68 (7) na kusema anahitaji Mnyika athibitishe tuhuma hizo kwa kuwa siku saba za kufanya hivyo tayari zimeshapita.

Nchemba alidai kwamba tuhuma hizo hazikuwa za kweli kwani wakati wizi huo unafanyika yeye hakuwa mwajiriwa wa BoT kama Mnyika alivyodai, na kwamba zililenga kumdhalilisha na kumharibia jina kwa wapiga kura wake.

Ndugai alisema Mnyika alifikisha uthibitisho wa maandishi ambao hata hivyo, si uthibitisho kamili bali ni utangulizi tu wa maneno ambayo ndani yake hayathibitishi tuhuma dhidi ya mbunge mwenzake.

“Ni kweli kuwa siku saba alizopewa Mnyika kuthibitisha tuhuma dhidi ya mheshimiwa Nchemba zimepita, lakini tulichopokea si uthibitisho kamili bali ni kama maelezo tu. Kwa hiyo tutalifikisha suala hilo mbele ya Kamati ya Maadili," alisema Ndugai.

Ndugai aliongeza kuwa, wabunge wanaotoa tuhuma bila kuleta uthibitisho waache tabia hizo kwani zinachochea chuki na zinawaondolea wananchi imani kwa viongozi wao.


“Wabunge ni viongozi wakubwa na wanaoaminiwa na wananchi. Tunapodiriki kusema uongo tunajiharibia sifa zetu za uongozi, kama huna uhakika na tuhuma unazozitoa basi usizilete mbele ya Bunge,” alisema.

Hata hivyo, jana mchana Mnyika alisema uamuzi wa Ndugai wa kupeleka suala lake katika Kamati ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge ulikuwa umepangwa na unakiuka kanuni za Bunge.

Mnyika akizungumza na waandishji wa habari nje ya bunge, alisema ni wazi kwamba Ndugai alikiuka Kanuni za Bunge na kuwa yeye na Nchemba walikuwa wamejipanga kufanya propaganda bungeni.

Alisema, Kanuni ya Bunge ya 73 (3),  inamhusu mbunge ambaye ameshindwa kutoa uthibitisho bungeni katika muda uliopangwa.

Alisema badala yake, Naibu Spika aliamua kulipeleka jambo hilo katika kamati ambayo siyo kazi yake ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge.

Mnyika alisema kamati hiyo kazi yake ni kushughulikia masuala ya wabunge wanaowatuhumu bungeni watu walio nje ya Bunge na kushughulikia migogoro ya kimasilahi.


Akizungumzia uthibitisho wake, Mnyika alisema Jenister Mhagama  aliyekuwa anaongoza kikao siku hiyo, alikurupuka kwa kumtaka alete ushahidi kwa kitu ambacho hakukisema.

“Mimi sikuzitaja tuhuma anazotuhumiwa Mwigulu, nilisema anatuhumiwa na hata pale nilipomtaka Mhagama aniruhusu nizitaje tuhuma zenyewe, hakuniruhusu badala yake akakimbilia kutoa uamuzi kuwa nilete uthibitisho kuwa Mwigulu anahusikaje na EPA.

“Katika barua yangu ya ushahidi kwa Spika, nilipeleka uthibitisho wangu kwa kile nilichokisema na nimenukuu ‘hansard’ (Taarifa rasmi ya bunge), kwa hiyo sijathibitisha kitu ambacho sikukisema,” alisema Mnyika.

Mnyika pia alisema amekata rufaa katika Kamati ya Kanuni kuwashtaki Spika, Naibu Spika na wenyeviti wa Bunge kwa kulinyima Bunge fursa ya kuisimamia Serikali katika mambo muhimu, kwa kisingizo kuwa mambo hayo yapo mahakamani.

Giza lakatisha Bunge

Katika hatua nyingine, Ndugai alijikuta akiahirisha shughuli za Bunge  jana kabla ya wakati, baada ya umeme kukatika na jenereta iliyopo kushindwa kukidhi haja katika jengo hilo.

Umeme ulikatika wakati kikao cha Bunge kikiingia katika shughuli muhimu ya kupitisha makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.


Ndugai alitoa maagizo kuwa Bunge liendelee na shughuli zake katika hali hiyo ya giza, ambapo waziri wa wizara hiyo, Profesa Tibaijuka aliendelea kujibu maswali ya wabunge huku ukumbi ukiwa katika giza totoro.

Kikao kiliendelea gizani kwa takriban  dakika kumi ambapo wabunge watatu walitaka majibu katika hali hiyo ya giza na Profesa Tibaijuka akayajibu katika hali hiyohiyo.

Hata hivyo, hakukuwa na utulivu hasa wakati wabunge wengine walipokuwa wakiuliza maswali yao na wengine kusoma kitabu cha makadirio ya wizara ya bajeti hiyo kwa kutumia simu za mikononi.

Ndipo Ndugai alipoamua kuahirisha kikao hicho hadi leo saa 3:00 asubuhi ambapo Bunge litaendelea kupitisha bajeti hiyo kifungu kwa kifungu.

“Hatutaweza kuendelea katika hali hii, kwa hiyo naahirisha kikao hiki hadi hapo kesho,” alisema.

Ukosefu wa nishati vijijini ni janga la taifa

Written By Koka Albert on Tuesday, July 10, 2012 | 6:05 AM

Elias Msuya
NI miaka 50 sasa tangu Tanzania ilipojipatia uhuru wake huku ikiendelea kuogelea kwenye lindi la umaskini. Siyo kwa sababu ya kukosa rasilimali, bali kutokana na sababu mtambuka.
Moja kati ya mambo yanayodhihirisha umaskini huo ni ukosefu wa nishati ya uhakika katika maisha ya kila siku na kwa maendeleo ya taifa.
Ni kweli tuna umeme wa Gridi ya Taifa, lakini hadi sasa umeme unatumiwa na asilimia 14 pekee ya Watanzania. Maana yake, hadi sasa asilimia 86 ya Watanzania hawana umeme huo, badala yake ama wanatumia umeme unaozalishwa kwa jenereta, jua au njia nyingine zisizo za uhakika.
Asilimia 14 ya hao wanaotumia  umeme ni wanaoishi mijini huku pia kukiwa na viwanda vichache vinavyozalisha bidhaa kwa masoko ya ndani na nje.
Watanzania wengine asilimia 80 ya wanaoishi vijijini hubaki wakitumia misitu kama chanzo kikuu cha nishati kwa kukata miti ili kupata kuni na kuchoma mkaa.
Kwa jumla, asilimia 90 ya nishati inayotumika nchini inatokana na mimea yaani matumizi ya mkaa na kuni huku asilimia nane pekee ya nishati inayotumika nchini hutokana na mafuta na kiasi kilichobaki hutegemea maji.
Matumizi ya kuni na mkaa huchangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira. 
Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa Tanzania ina ekari 33 milioni za misitu, ambazo ni sawa na asilimia 39 ya ardhi yake yote.
Lakini kutokana na uharibifu wa misitu hiyo, inakadiriwa kuwa kila mwaka Tanzania hupoteza hekta 500,000 za misitu ambapo hekta 300,000 sawa na kilometa za mraba 3,320 za misitu hupotea kwa kuchoma mkaa kila mwaka.
Katika matumizi ya mkaa, tafiti zinaonyesha kuwa Jiji la Dar es Salaam pekee hutumia magunia 35,000 ya kuni kwa siku, huku taarifa nyingine zikionyesha magunia kati ya 15,000 hadi 20,000 ya mkaa huingia Dar es Salaam kila siku.
Mikoa mingine inayotajwa kwa matumizi makubwa ya mkaa ni pamoja na Mwanza, Shinyanga, Tabora, Morogoro na Mbeya.
Benki ya Dunia inakadiria kuwa, kila mwaka Tanzania hutumia tani milioni moja za mkaa, huku Jiji la Dar es Salaam likitumia nusu ya mkaa huo kwa mwaka.
Kwa hali hiyo, wataalamu wanasema kuwa Tanzania itakuwa imemaliza misitu yote miaka 10 ijayo ikiwa juhudi za makusudi hazitachukuliwa kunusuru misitu. Hili ni janga linaloinyemelea Tanzania.
Pamoja na tishio hilo, bado Serikali haionekani kuchukua hatua madhubuti  ili kupambana nalo.
Serikali imejikita zaidi kwenye miradi ya umeme wa maji, gesi ili kutafuta suluhisho la nishati nchini

Yondani:Simba mnapoteza muda

Kalunde Jamal
KELVIN Yondan amesema usajili wake Yanga hauna dosari yoyote, na kwamba jitihada za Simba kumwekea vikwazo hazitafanikiwa.

Uhamisho wa Yondani toka Simba kwenda klabu hiyo ya Jangwani, bado una utata kutokana na jina lake kuwa halali kwa klabu zote mbili

Simba ilitangaza kumwekea pingamizi Yondan ili asicheze michuano ya Kombe la Kagame kwa madai ni mchezaji wao halali.

"Uamuzi wangu kusajili Yanga ni sahihi kabisa, hakuna shida hata kidogo nawashangaa Simba kuendelea kuning'ang'ania," alisema Yondani.

"Nilikuwa mikononi mwao hata baada ya mkataba wangu kumalizika na hawakuniambia lolote, sasa nimesajili Yanga wanaanza kuleta chokochoko."

Dk Slaa, Mnyika, Lema matatani

POLISI KUWAHOJI KWA MATAMSHI KWAMBA WANATISHIWA MAISHA, DK NCHIMBI ASEMA WANASABABISHA CHUKI
Neville Meena na Florence Majani, Dodoma
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Godbless Lema huenda wakajikuta matatani kutokana na madai waliyoyatoa juzi kwamba wanatishiwa kuuawa na kigogo mmoja wa Idara ya Usalama wa Taifa.Kutokana na matamshi hayo, jana Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi ameliagiza Jeshi la Polisi kuwahoji viongozi hao ambao walidai kuwa mauaji hayo yamepangwa kufanywa kwa kuwekewa sumu kwenye chakula au kwa kutumiwa makundi ya ujambazi.

Akizungumza na waandishi wa mjini hapa jana, Dk Nchimbi alisema licha ya kudai kwamba wanatishiwa, ameshangazwa na msimamo wa viongozi hao kukataa kupeleka suala hilo polisi kwa madai ya kuhofia suala hilo halitafanyiwa kazi.

Alisema watawahoji viongozi hao kwa sababu suala la usalama wa Mtanzania yeyote si la hiari, bali ni la kikatiba na la kisheria hivyo, ni lazima polisi watimize wajibu wao.

“Ni lazima tuwahoji ili tujue ni nani amewatisha na kwa sababu zipi. Hatutamuomba mtu ruhusa ya kumlinda kwa sababu huo ni wajibu na kazi yetu kuwalinda raia, hilo halina mjadala. Hatua zitachukuliwa endapo itabainika kuwa madai yao yana ukweli,” alisema Dk Nchimbi.

Aliwataka viongozi  wote wa kisiasa wakiwamo wa Chadema wanapohisi kutishiwa usalama wao, watoe taarifa polisi ili vyombo vya dola viyafanyie uchunguzi malalamiko yao ili utaratibu ufanyike kuhusu usalama wao kama sheria inavyotaka.

Alionya tabia ya viongozi kuzungumza nje ya utaratibu akisema haikubaliki kwani inaweza kuwa ni mbinu za kujitafutia umaarufu wa kisiasa.

Dk Nchimbi alisema jambo hilo si jema kwani linajenga hofu miongoni mwa Watanzania na kuwafanya wasiviamini vyombo vyao vinavyowalinda kwa mujibu wa sheria.
“Ni kweli kuwa kila mwanasiasa anataka kukubalika na umma lakini, akubalike katika taratibu zinazokubalika,” alisema Dk Nchimbi na kuongeza:

“Ingekuwa Serikali inataka kukubali umaarufu kama huo, basi ingetumia mwanya wa haohao Chadema wakati mitandao ya kijamii iliposambaza taarifa kuwa Chadema ilihusika na kifo cha marehemu, Chacha Wangwe.”

Alisema Serikali haikukurupuka na kuwakamata, badala yake ilifanya uchunguzi kwanza na matokeo yake alikamatwa  dereva wake ambaye ameshachukuliwa hatua.
Alisema kama Serikali ingekuwa inatafuta umaarufu, ilikuwa ni fursa nzuri kwake kujipatia umaarufu na kukivuruga chama hicho kwa kuwakamata viongozi wa Chadema hasa baada ya kuwapo kwa uvumi kwamba wamemuua kiongozi huyo.

“Viongozi wetu wa kisiasa ni lazima wafanye mambo ambayo kesho na keshokutwa watakiri mchango wao, ama katika ujenzi au uharibifu wa nchi yetu. Kila siku wakilalamika kuwa wanataka kuuawa basi ni lazima watu watawashangaa kwani badala ya kutatua matatizo ya wananchi wanabaki wakilalama wanataka kuuawa. Watu kama hawa wanafanya hivi kwa masilahi yao, wanaweza kuwagombanisha wananchi.”

Waziri Nchimbi aliwataka wananchi na viongozi wa kisiasa kuondoa hofu kwani Serikali ina wajibu wa kuwalinda na hakuna mtu atakayenufaika kwa mauaji ya wanasiasa hao.

Kuhusu madai kwamba polisi wamekuwa wakipuuza malalamiko ya wapinzani, Dk Nchimbi alikiri kuwapo kwa baadhi ya polisi wenye kasoro katika utendaji wao lakini akasema wengi ni waadilifu.
Alisema ikiwa kuna mtu haridhishwi na utendaji wa polisi kwa kutopata huduma kama inavyostahili, ana uhuru wa kutoa taarifa katika ngazi za juu hata ikiwa ni kwake.

Ikulu nayo yatoa tamko

Katika hatua nyingine, Ikulu imesema hakuna mpango wowote unaoratibiwa na Idara ya Usalama wa Taifa kwa lengo la kuwaua viongozi hao wa Chadema.
Jana, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alihoji sababu za Serikali kutaka kuwaua viongozi hao wakati si tishio lolote kwa nchi.

Balozi Sefue alisema Idara ya Usalama wa Taifa haiko kwa ajili ya kuua raia au viongozi, bali kulinda masilahi ya taifa na kuhoji: “Sasa kwa nini wauawe? Wana nini hasa hadi Idara ya Usalama ifanye hivyo?”

Alisema ni vyema wakati mwingine kukawa na umakini kwa kuangalia namna siasa zinavyoweza kufanya kazi... “Hii inaweza kuwa siasa tu. Sisi serikalini hatuna mambo ya vyama, tunafanya kazi kwa ajili ya watu wote.”

Alisema Idara ya Usalama wa Taifa na Serikali hazifanyi kazi kisiasa, bali kwa kuangalia masilahi ya Watanzania wote: “Huku serikalini sisi hatuna ugomvi na wanasiasa. Tunafanya kazi na watu wote.”
Alisema wanaoweza kufikiria kuwa kuna siasa katika Serikali na vyombo vyake wao ndiyo wanaweza wakawa wanafanya siasa.

Tuhuma za Chadema
Kauli hizo za Serikali zinatokana na tuhuma za Chadema kwamba kimebaini njama za kuwaua viongozi wake hao waandamizi ambazo zinaratibiwa na kigogo mmoja wa Idara ya Usalama wa Taifa na kwamba nyendo zao zimekuwa zikifuatiliwa kwa saa 24.

Tuhuma hizo za Chadema zilitolewa juzi na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni akisema: “Sisi Chadema hatuna mambo ya siri tunayotaka kufanya katika nchi hii. Matatizo ya Watanzania yapo wazi na yanajulikana na kila mmoja, Serikali ya CCM itekeleze sera na ahadi zao kwa wananchi na si vitisho.”

Mapokezi ya kocha mpya ya Yanga

Written By Koka Albert on Wednesday, July 4, 2012 | 7:41 AM

 
Kocha mpya wa Yanga, Mbelgiji Thom Saintfiet amewasili mida hii Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam na kulakiwa na mamia ya wapenzi wa klabu hiyo. Tazama mapokezi yake tangu anatokea ndani ya Uwanja wa Ndege, hadi akiwa ndani ya gari tayari kwa safari ya Jangwani.










GRAND LAUNCH NEW MAISHA CLUB DODOMA

Sakata la Ulimboka latikisa Bunge

Written By Koka Albert on Tuesday, July 3, 2012 | 7:15 AM

MBILINYI AFANANISHA WALIOMTEKA NA JANJAWEED, WAZIRI NAGU AINGILIA KATI
Waandishi Wetu
KITENDO cha kutekwa nyara, kuteswa na kisha kuumizwa mwili mzima, kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka jana kilitikisa Bunge huku wabunge wa CCM na Chadema wakitupiana mpira kuhusu nani waliohusika na tukio hilo.

Msuguano huo ulianza baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi kudai kuwa waliofanya kitendo hicho ni sawa na wanamgambo hatari wa Janjaweed wa Sudan.  

Kauli hiyo ya Mbilinyi maarufu kwa jina Sugu, ilizusha tafrani ndani ya Bunge kwani Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji), Dk Mary Nagu aliomba mwongozo wa Mwenyekiti wa Bunge, Sylivester Mabumba aliyekuwa akiendesha Bunge jana jioni akihusisha matamshi hayo na kuituhumu Serikali kutumia watu kama Janjaweed katika kumteka Dk Ulimboka jambo ambalo alisema siyo la kweli.

Akichangia Hotuba ya Ofisi ya Rais, (Utumishi, Utawala Bora, Ikulu na Mipango) Mbilinyi alisema kitendo alichofanyiwa Dk Ulimboka ni cha kinyama na baadhi ya watu wanaamini kwamba Serikali ilihusika, hatua ambayo ilimfanya Dk Nagu kusema Mbilinyi alikuwa akizungumzia jambo ambalo hana uhakika nalo na kutaka aamriwe kuthibitisha.

Mwenyekiti Mabumba alimtaka Mbilinyi athibitishe kauli yake au aifute. Wakati Mabumba akimtaka Mbilinyi kuthibitisha au kufuta kauli yake, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu alitaka kuingilia kati suala hilo na hata kuwasha kinasa sauti, lakini Mabumba alimwamuru akae chini.
Mbilinyi alipopewa nafasi alisisitiza: “Waliomteka Dk Ulimboka walikuwa na silaha kama siyo askari, basi hawana tofauti na kikundi cha Janjaweed ambacho kilifanya mauaji makubwa na kumfanya Rais wa Sudan, Omar Al Bashir ambaye sasa anatakiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai kuhusu kufanya uhalifu dhidi ya binadamu.”

Alifafanua kwamba, hakusema kama Serikali inatumia Janjaweed, bali alizungumzia namna Al Bashir alivyotumia wapiganaji hao kufanya uhalifu badala ya jeshi.
Hali hiyo ilizidi kuzua mvutano kati ya kiti cha Spika na Mbilinyi uliodumu kwa dakika tatu, huku Lissu naye akitaka apewe nafasi atoe hoja yake.

Baadaye Mabumba alitumia busara na kuamua kumalizia suala hilo kwa kumtaka Mbilinyi aendelee kuchangia na mbunge huyo wa Mbeya akiendelea kuzungumzia zaidi hilo, alitaka Bunge liunde tume ya uchunguzi kwa sababu hana imani na Serikali kuunda tume kuchunguza ukatili huo.

Baada ya Mbilinyi kumaliza, Mabumba alimtaka Lissu atoe dukuduku lake na aliposimama alimpinga Mwenyekiti huyo wa Bunge kwa maelezo kwamba alitumia kifungu kisicho sahihi kumwamuru Mbilinyi atoe maelezo ya kuthibitisha au kufuta kauli. Hata hivyo, alimtaka akae chini akisema: “Usitafute umaarufu hapa.”

Baadaye alisimama Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Stella Manyanya ambaye alikituhumu Chadema kwa kuchochea mgomo huku akidai kwamba kilihusika kumteka na kumjeruhi Dk Ulimboka.

Mbunge wa Ubungo (Chadema),  alikuja juu baada ya kauli hiyo akimtaka Mwenyekiti amtake Manyanya kuthibitisha au kufuta kauli yake. Badala yake, Mabumba alimtaka Mnyika kuthibitisha kwamba chama hicho hakihusiki.

Mnyika alisema Chadema hakihusiki na suala hilo na kueleza kwamba ripoti ya Kamati ya Bunge iliyoundwa kuchunguza mgogoro wa madaktari na Serikali inathibitisha hivyo, akitaka iwasilishwe bungeni na isomwe.

Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba alisema Chadema kinaunga mkono mgomo wa madaktari akirejea hotuba ya upinzani bungeni iliyotolewa jana ikisema inawaomba wananchi kwa kushirikiana na madaktari kuiunga mkono Chadema kuishinikiza Serikali hadi wapate haki zao.

Manyanya alisimama tena na kudai kwamba hata waliomteka daktari huyo walikuwa wamevaa magwanda ambayo yanatumiwa na makada wa Chadema kauli ambayo iliibua mzozo huku wabunge wengi wa Chadema wakisimama kutaka kuzungumza.

Mwenyekiti Mabumba alilazimika kutumia dakika kadhaa kuwataka wabunge watulie na wakae chini lakini Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali alikataa kutii amri hiyo akitaka kuzungumza hali ambayo ilimfanya Mabumba kuamuru atolewe nje ya eneo la Bunge na kumtaka Manyanya aendelee kuzungumza.

Muhimbili utata mtupu
Wakati uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ukisema huduma katika hospitali hiyo zimerejea katika hali ya kawaida baada ya madaktari kurejea kazini jana, madaktari bingwa wa hospitali hiyo nao wametangaza kuanza mgomo.

Taarifa iliyotolewa jana na msemaji wa uongozi wa Muhimbili, Aminiel  Aligaesha imesema wagonjwa wote waliolazwa wodini jana walihudumiwa na baadhi ya kliniki za huduma ya upasuaji zilifanyika na kuongeza: “Hata hivyo, upasuaji haukufanyika kwani hakukuwa na orodha ya wagonjwa waliopangwa kufanyiwa upasuaji.”

Lakini wakati uongozi wa Muhimbili ukisema hivyo, madaktari bingwa walikutana jana katika hospitali hiyo na kutangaza kuanza mgomo. Akizungumza muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkutano wao uliofanyika katika hospitali hiyo, msemaji wao Dk Catherine Mng’ongo alisema:
“Sisi madaktari bingwa kufanya kazi bila Interns haiwezekani. Tungeanza kufukuzwa sisi kwanza. Kuanzia sasa hatutafanya kazi hadi hapo Serikali itakapokubali kuwarejesha wote kazini na kufungua meza ya majadiliano yenye nia ya dhati ya kumaliza mgogoro.”
Dk Mng'ong'o alisema zaidi ya madaktari 200, waliokuwa kwenye mafunzo ya vitendo Muhimbili na Taasisi ya Mifupa (Moi) wamepatiwa barua za kufukuzwa kazi na idadi yao nchi nzima inafikia 300.

Tamko la Rais Kikwete

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania , Dk Godbles Charles ameeleza kushangazwa na kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwa Serikali haihusiki katika sakata hilo na akidai ameingilia kazi ya tume iliyoundwa na Polisi kuchunguza tukio hilo.
“Je, ni sahihi kwa Rais kutamka waziwazi kuwa Serikali yake haihusiki kwa namna yoyote ile hata kabla ya ripoti ya uchunguzi?” alihoji Dk Charles.
Habari zilizopatikana jana zilieleza kuwa hali ya Dk Ulimboka inaendelea vizuri anakotibiwa Afrika ya Kusini.
Hospitali nyingine
Madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC wamekubaliana na kuendelea na mgomo wakisubiri uamuzi wa mkutano mkubwa wa madaktari utakaofanyika leo.
Jumamosi iliyopita, uongozi wa KCMC uliwatimua madaktari zaidi ya 80 walioko kwenye mafunzo kwa vitendo na kuwataka wasionekane katika eneo la hospitali wala kukusanyika hapo.

Uongozi wa Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru, umelazimika kuitisha kikao cha pamoja na madaktari wa hospitali hiyo kwa lengo la kuwasihi waachane na mgomo.

Vyanzo vya habari hospitalini hapo, vilidai ya kwamba katika kikao hicho uongozi wa hospitali hiyo chini ya Mganga Mkuu Mfawidhi, ulilazimika kuitisha kikao siku moja baada ya tukio la Dk Ulimboka na kuwaangukia madaktari hao waachane na mgomo.

Huko Mbeya, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Mbeya, Dk Eliuter Samky amesema utoaji huduma kwa wagonjwa siyo wa kuridhisha  kutokana na kuathirika kwa kiasi kikubwa kwa baadhi ya sekta muhimu.

Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, Samky alisema mgomo huo umesababisha kuzorota kwa huduma kwa wagonjwa licha ya kusitisha huduma nyingine za kawaida na kubaki kuendelea kutoa huduma za dharura.

Habari hii imeandikwa na Leon Bahati, Geofrey Nyang’oro Aidan Mhando,Victoria Mhagama, Godfrey Kahango, Mbeya, Daniel Mjema, Moses Mashalla, Arusha.

Bolt beaten again! Jamaican rival Blake stuns Usain for second time in three days

Written By Koka Albert on Monday, July 2, 2012 | 1:02 PM

Usain Bolt was beaten for the second time in three days by training partner Yohan Blake, this time surrendering his supremacy in the 200metres.

The Jamaican world record holder and Olympic champion was edged out by his rival in their nation's trials for this summer's Games in London. Blake came home in 19.80, 0.03seconds ahead of Bolt. 

In a result that can no longer be considered a surprise, Blake started edging into the lead near the turn, then burst past Bolt for the narrow victory.
Come back here: Usain Bolt congratulates Yohan Blake after his 200m triumph
Come back here: Usain Bolt congratulates Yohan Blake after his 200m triumph at the Jamaican Olympic Trials

The win came two days after Blake, the reigning world 100 champion, beat Bolt in the 100 by running a 9.75. 

If everything goes to form, their next meeting will be at the London Olympics. 
'I can never be discouraged,' Bolt said. 'I'm never worried until my coach gets worried, and my coach isn't worried, so I'm OK.'
Flat out: Bolt received treatment on the track after the 200m final
Flat out: Bolt had time to reflect on his defeat as he received treatment on the track after the 200m final

Glen Mills, who coaches both runners, said: 'Usain, he has the experience, the ability, he has been there already. He might be a little off at the moment, but I'm sure when the time of delivery comes around, he'll be on top of his game.'

When asked if he was carrying an injury or was holding back, Bolt said: 'I don't want to get into that.
'I was just working (the leg) around for a few moments to get myself back together. I'm not far off. I can get it done.'
Bolt added: 'I was very sad with my turn, it was awful, but I've been working more on the 100 meters.
'I can't blame it on that, though. Just have to get my things together and get it done.'
Showdown: Yohan Blake (right) and Usain Bolt (left)
Treat in store: Blake (right) and Bolt (left) will renew their rivalry at the London Olympics in under a month
Dip for the line: Bolt tries to edge in front but is beaten by his rival
Dip for the line: World record holder Bolt desperately tries to edge in front but is beaten by his rival
Blake will be making his first trip to the Olympics, which can be a daunting prospect. After these pair of benchmark victories, he sounded ready for more work, not a celebration. 

'It leaves me to get back into training,' Blake said. 'It's not over. I still have the Olympics to go.'
Like a racecar driver catching a glimpse of something lurking in his rearview mirror, Blake could see Bolt making up ground out of the corner of his eye. The best ones know how to close things out. 
'I felt him on my right-hand side. No need to panic,' Blake said. 'I just stayed focused.'

In the women's 200, Shelly-Ann Fraser-Pryce ran a personal best 22.10 seconds to also complete the 100-200 sweep. She'll be joined by Sherone Simpson and two-time defending Olympic champion Veronica Campbell-Brown.

Who's the daddy now, Mario? After suffering heartache in Euro 2012 final, Balotelli is due to become father

It has been a rollercoaster week even by the standards of Mario Balotelli.
First he scored two stunning goals in the Euro 2012 semi-final against Germany. Then it was heartache in the final against Spain on Sunday.
But now Balotelli has received perhaps the biggest news of all - that he is to become a father.
Down and out: Mario Balotelli reacted angrily to Italy's Euro 2012 defeat
Down and out: Mario Balotelli reacted angrily to Italy's Euro 2012 defeat
The 21-year-old has been told by his pregnant former girlfriend Raffaella Fico that it is his child.
He was told on the eve of the match against Germany when he grabbed a brace to book his country's place in the final. He reportedly told her: 'You gave me the best news of the world.'

And Italian model Raffaella has claimed that the pair are patching up their relationship.
She said: 'Mario and I are rebuilding our relationship. He never stopped loving me. Those who think I've wanted to trap the rich and famous footballer will have to think again. 

'Last Christmas, he told me: "Let's get married and make a son" and I accepted. Now I'm waiting for Mario to discover the sex of the child, although he would prefer a boy, and to choose the name.'
Meanwhile, AC and Inter Milan have been warned that Balotelli is worth £200million following his star showing at Euro 2012.
Balotelli's? The Italian model, who split up with the striker two months ago, was at a charity event when she showed off her bump and has reportedly said it is Mario's
Baby bump: Mario Balotelli's ex-girlfriend Raffaella Fico has sparked rumours she's pregnant with his child after showing off her baby bump
 Baby bump: Mario Balotelli's ex-girlfriend Raffaella Fico sparked rumours after showing off her baby bump
As they were: Mario and Raffaella dated for a year until they broke up two months ago
As they were: Mario and Raffaella dated for a year until they broke up two months ago
Balotelli, 21, a self-confessed Milan fan, is a target for the Italian giants but will set any prospective suitor back the eye-watering figure, according to his agent.

The striker could not prevent Italy crashing to a 4-0 Euro 2012 final defeat to Spain on Sunday night but stole the limelight by scoring two superb goals in his national team's 2-1 triumph over Germany in the semi-finals of the tournament in Poland and Ukraine.

'I have always said that Mario Balotelli is one player that could become the strongest in the world,' Balotelli's agent Mino Raiola told Sky Italia. 'He is probably amongst the strongest in Europe.
'How much is he worth? He is worth what the market says, he is one that can make a difference.
'In the actual market I don't think there is a value for him but if I had to give a price I would say he is worth 250million (euros).
Down and out: Mario Balotelli reacted angrily to Italy's Euro 2012 defeat
Down and out: Mario Balotelli reacted angrily to Italy's Euro 2012 defeat
'I say this to give a figure but you would have to ask the City owner (Sheikh Mansour) how much he is worth.'

Raiola added that he could see no immediate return to Italy for Balotelli. 'I'm 200 per cent certain that Mario will not return to Italy at least while I'm his agent.' Balotelli is under contract at the Etihad Stadium until June 2015.

The volatile front-man was reduced to tears in the wake of the Euro 2012 final. He endured a frustrating evening as Spain romped to a historic third successive major international tournament victory.
Firing blanks: Balotelli was unable to prevent Spain from running away with the trophy
Firing blanks: Balotelli was unable to prevent Spain from running away with the trophy
And unfortunately after the match the ugly side of his game came to the fore once more after the striker clashed with members of Italy's backroom staff.

Balotelli had had a splendid tournament until that point, most notably when he blasted Italy into Sunday's showpiece with a stunning double to down Germany.

However at the full-time whistle in Kiev, the Manchester City man made a beeline for the dressing room. He came up against resistance from senior figures and appeared to push one. 

After several minutes, Balotelli could then be seen on his haunches in the centre of the pitch. He later collected his medal but broke down in tears as soon as he returned to the pitch.

Italy coach Cesare Prandelli says his player will emerge stronger from the shattering experience.
'I told Mario that these are experiences you have to deal with and have to accept,' said Prandelli. 'You have to hold your hands up and say the opponents were better, accept defeat.

'But you also have to make sure this helps you going forward and you can grow from the experience. This has happened to a number of players, and will happen again, but this is what sport is all about.'
I'm outta here: Mario stormed off at full-time
                                           I'm outta here: Mario stormed off at full-time
.
Words of sympathy: Italy coach Cesare Prandelli comforted his striker
                Words of sympathy: Italy coach Cesare Prandelli comforted his striker

JK: Hatuhusiki unyama aliofanyiwa Ulimboka

SEMA MADAKTARI WASIOKUBALI MSHAHARA WA SERIKALI WAFUNGASHE VIRAGO
Boniface Meena
WAKATI Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka akiendelea na matibabu Afrika Kusini, Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali haihusiki na kilichomtokea daktari huyo kwa kuwa alikuwa kiungo muhimu katika majadiliano baina ya pande hizo mbili.

Rais Kikwete alisema hayo jana katika hotuba yake ya kila mwezi, ambapo mbali na suala hilo, pia alizungumzia sababu za mgomo wa madaktari na usafirishaji wa wahamiaji haramu.

Dk Ulimboka ambaye alikuwa anaratibu mgomo wa madaktari unaoendelea nchi nzima kutokana na Serikali kushindwa kutimiza madai yao mbalimbali, anatibiwa figo na majereha aliyoyapata katika sehemu mbalimbali za mwili, baada ya kutekwa na watu wasiojulikana, kisha kupigwa, kung'olewa kucha, meno mawili na kutupwa katika Msitu wa Pande, usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita.

Tangu kutokea kwa unyama huo uliofanywa na watu wasiojulikana, baadhi ya wananchi na wanaharakati wamekuwa wakiilaumu Serikali kuwa inahusika na utekaji huo na wengine wakienda mbali zaidi, kuwa watekaji walikuwa wanamlazimisha kueleza nani yuko nyuma ya mgomo wa madaktari.

Rais Kikwete, kama awali alivyosema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, walisema wanatambua kuwa, Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka kuhusu kilichomtokea Dk Ulimboka, lakini yeye ameshangazwa na hisia hizo, kwani haoni sababu ya Serikali kufanya hivyo.

"Dk Ulimboka alikuwa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na madaktari. Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya.  Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam madaktari wanamwamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali," alisema Rais Kikwete.

Alisema Serikali haina sababu ya kumdhuru Dk Ulimboka kwa sababu suala la mgomo, Mahakama Kuu imekwishatoa amri ya kuusitisha, hivyo anayekaidi amri hiyo atakuwa ananunua ugomvi na mhimili huo wa dola, ambao wenyewe una mamlaka ya kumtia adabu.

"Hivi baada ya kufika hapo Serikali iwe na ugomvi na Dk Steven Ulimboka kwa sababu ipi na jambo lipi hata iamue kumdhuru?" alihoji na kuongeza:

"Kama kuna mtu wa Serikali kafanya, itakuwa kwa sababu zake binafsi na siyo za Serikali au kwa kutumwa na Serikali," alisema Rais Kikwete.

Alisema alichofanyiwa Dk Ulimboka kimemsikitisha na kumhuzunisha kwa kuwa ni kitendo cha kinyama na kinyume kabisa na mila na desturi za Tanzania.

Alisema Watanzania hawajazoea mambo hayo na kwamba ameelekeza vyombo vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi wa kina ili ukweli ujulikane.

"Nimesema kuwa ningependa ukweli huo ujulikane mapema ili tuondoe wingu baya la kutiliana shaka na kulaumiana kunakoendelea hivi sasa," alisema.

Alisema anatoa mkono wa pole kwa Dk Ulimboka na kumwombea apone haraka ili aungane na familia yake na Watanzania wenzake katika ujenzi wa taifa.

Rais Kikwete pia alimpongeza Juma Mgaza ambaye alimsaidia Dk Ulimboka kumtoa katika pori alikotupwa na kumpeleka kituo cha polisi kwa moyo wake wa huruma.

Kuhusu mgomo
Kuhusu mgomo unaoendelea Rais Kikwete alisema, kiwango cha mshahara cha Sh3.5 milioni wanachokitaka madaktari Serikali haina uwezo wa kukitoa, hivyo daktari anayeona kuwa hawezi kufanya kazi serikalini bila ya kulipwa mshahara huo, awe huru kuacha kazi na kwenda kwa mwajiri anayeweza kumlipa kiasi hicho.

Rais Kikwete alisema, kwa sasa Serikali haiwezi kuwaahidi kuwa inao uwezo wa kuwalipa mshahara wa kuanzia wa Sh3.5 milioni na posho zote zile, kwani ikifanya hivyo malipo ya daktari anayeanza kazi yatakuwa Sh7.7 milioni kwa mwezi, kitu ambacho haitakiweza.

"Si vyema kutoa ahadi hewa kwa watu tunaowaheshimu na kuwathamini kama walivyo madaktari. Kutokana na ukweli huo basi kama daktari anayeona kuwa hawezi kufanya kazi serikalini bila ya kulipwa mshahara huo awe huru kuacha. Nasi tutamtakia kila la heri,"alisema Rais Kikwete.

Rais Kikwete alisema, madaktari hawana sababu ya kugoma ili washinikize kulipwa mshahara huo kwani uwezo haupo.

"Kwa nini upate usumbufu wa kuachishwa kazi na kutakiwa kuondoka kwenye nyumba ya Serikali ndani ya saa 24. Jiepushe na yote hayo kwa kujiondoa mwenyewe," alisema.

Alisema mamlaka za ajira zimeanza kuchukua hatua hizo kwa wale wanaokwenda kinyume na sheria za kazi na wataendelea kufanya hivyo kwa wote wanaoendelea kugoma.

Alisema anajua baada ya hatua hizo kuchukuliwa kuna manun’guniko ya kuonewa yatajitokeza, lakini ni bora kufanya hivyo ili ijulikane Serikali haina daktari.

"Mlitegemea mwajiri afanyeje? Ni bora kufanya hivyo ili ajue hana daktari aweze kufanya utaratibu wa kuziba hilo pengo na huyo anayekuja awe na mahali pa kuishi."

Kutokana na hali hiyo amewasihi madaktari kuacha mgomo na kurejea kazini, kwani Watanzania wanateseka na kupoteza maisha.

Sababu za mgomo
Rais Kikwete alisema kwamba, kuna masuala matatu ambayo yamekuwa na mwafaka kwa kiasi fulani na kutoafikiana kwa baadhi ya mambo kati ya madaktari na Serikali.

Alisema suala la kwanza ni suala la kufanya kazi katika mazingira hatarishi ambalo Serikali imekubali hoja ya kuchukua hatua ya kuwalinda madaktari wanaofanya kazi katika mazingira hatarishi.

Pia alisema Serikali imeeleza dhamira ya kurudisha posho ya mazingira hatarishi kwa watumishi wa umma wanaostahili na utekelezaji wake utafanyika baada ya uchambuzi wa kina wa kubainisha mazingira hatarishi ni yapi, viwango stahiki viwe vipi na nani hasa wahusike.

Rais Kikwete alisema kuwa, madaktari wamekataa suala hilo la kufanya uchambuzi, wanataka kiwango kiwe kama wanavyotaka wao, yaani asilimia 30 ya mshahara na kianze mara moja.

Alisema suala la pili ambalo wamekubaliana nusu nusu ni kuhusu nyumba za kuishi ambalo Serikali imekiri wajibu wake wa kuwapatia nyumba za kuishi.

Rais Kikwete aliongeza kwamba, kwa maeneo ambayo madaktari wanalipwa posho ya pango, Serikali imesema waajiri wataendelea kufanya hivyo kwa mujibu wa taratibu zilizopo kwa watumishi wa umma wenye stahili ya kupewa nyumba.

Alisema jambo hilo limekataliwa na madaktari na kutaka lazima walipwe asilimia 30 ya mshahara kama posho ya nyumba.

Rais Kikwete alisisitiza kwamba, Serikali kwa upande wake imeona vigumu kufanya hivyo na kuwasihi wakubali wanayotendewa kama wafanyakazi wengine wote wa umma.

Alisema suala lingine ambalo lilikuwa na makubaliano ya nusu nusu ni kuhusu posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu na pande zote mbili ziliafikiana kuwa yapo baadhi ya maeneo nchini yanayo mazingira magumu kwa watumishi wa umma, hivyo hatua zichukuliwe kuwasaidia watumishi hao.

Kuhusu posho, alisema Serikali imekubali kuwapo posho ya aina hiyo ila itatekelezwa baada ya kufanya uchambuzi wa kuainisha mazingira husika, kutambua watumishi waliopo na gharama zake.

Alisema madaktari hawajakubali kusubiri zoezi la uchambuzi lifanyike, wanataka Serikali ilipe posho hiyo sasa.

"Tofauti hapa si posho hiyo kuwapo, bali ni rai ya Serikali ya kubaini maeneo yenyewe na kupanga aina ya hatua na viwango vya posho kulingana na mazingira halisi ya maeneo. Madaktari hawaoni haja ya kufanya hayo," alisema.

Alisema kuna mambo mawili ambayo hayakuwa na mwafaka kabisa kati ya pande hizo mbili na la kwanza ni posho ya kuitwa kazini (on call allowance).

Rais Kikwete alisema, Serikali ilishaongeza posho hizo tangu Februari, 2012 posho iliongezwa kutoka Sh10,000 hadi Sh25,000 kwa daktari bingwa, Sh20,000 kwa dakari mwenye usajili wa kudumu na Sh15,000 kwa madaktari waliohitimu ambao wapo katika kipindi cha mafunzo kazini (Interns).

Alisema hata hivyo, madaktari kwa upande wao hawakukubali uamuzi huo wa Serikali na kusisitiza walipwe asilimia 10 ya mshahara.

Rais Kikwete alisema ugumu wa kukubali pendekezo la madakari ni kuwa sharti la malipo haya ni mtu kuitwa kazini na kwamba ukitaka ilipwe kiwango cha mshahara ina maana kuwa hata kama daktari hakupangwa kuitwa au alipangwa na hakutokea aendelee kulipwa.

Alisema jambo la pili ambalo mwafaka haukufikiwa baina ya Serikali na madaktari ni kuhusu mshahara wa kuanzia kazi wa daktari ambao madaktari wanataka uwe Sh3.5 milioni wakati Serikali inasema kiasi hicho hatukiwezi.

Alisema Serikali imeeleza utayari wake wa kuongeza mshahara kwa kati ya asilimia 15 mpaka 20 kama ambavyo itafanya kwa watumishi wote wa umma katika mwaka huu wa fedha.

Rais Kikwete alisema, kwa kiwango cha sasa cha mshahara wao, daktari ataanzia kati ya Sh1.1 milioni na Sh1.2 milioni kutegemea kiwango kipi hatimaye kitaamuliwa.

"Madaktari wamekataa katakata na wameng’ang’ania Sh3.5 milioni," alisema.

Alisema ni muhimu madaktari wakatambua kuwa wagonjwa wanateseka na wengine kupoteza maisha kwa mgomo usiokuwa halali kisheria ambao pia haustahili kuwapo hata kwa mujibu wa maadili ya udaktari.

Alisema viongozi wa MAT na wenzao wanawaingiza madaktari katika mgogoro na mahakama na waajiri wao isivyostahili.

Rais Kikwete alisema ni vyema viongozi wa madaktari na madaktari wakatambua kuwa wanashiriki katika mgomo usiokuwa halali ambao pia kiongozi wao mkuu amekana mahakamani kuwa hahusiki nao.

Rais Kikwete alisema madaktari lazima watambue pia kwamba ajira zao wanaziweka hatarini kwani mfanyakazi hana kinga ya kutofukuzwa kazi na mwajiri kwa kushiriki mgomo unaokubalika kisheria.

"Huu siyo. Watapoteza ajira, hawana pa kukimbilia, hawana cha kuwalinda. Kwa madaktari interns, wanahatarisha maisha yao, kwani hawatapata cheti cha kudumu wakishiriki mgomo usiokuwa halali. Lazima watafakari kwa hayo wafanyayo," alisema.

Hoja za madaktari
Rais Kikwete alisema katika mambo 12 ambayo madaktari waliyawasilisha pande zote mbili zilifikia mwafaka na kukubaliana kwa pamoja kwa mambo saba.

Alitaja la kwanza ni kuhusu usafiri wa kwenda na kurudi kazini ambalo limeshashughulikiwa.

Alisema jambo la pili, ni madaktari kupatiwa Green Card za Bima ya Afya ambalo Serikali na Wizara ya Afya zimechukua hatua za utekelezaji wake.

Jambo la tatu, alilitaja Rais Kikwete kuwa ni hatua za kinidhamu kuchukuliwa dhidi ya Watendaji Wakuu wa Wizara ya Afya ambalo tayari Serikali imechukua hatua.

"Uongozi wa juu wa wizara umebadilishwa na sasa kuna uongozi mpya. Lakini, jambo la kustaajabisha hata Waziri mpya wa Afya alipowataka waonane kuzungumzia hoja walikataa kumuona.  Kwanza walisema hawaoni sababu kwa vile wameyazungumza na kamati yake kwa miezi mitatu bila ya mafanikio," alisema.

Rais Kikwete alisema kuwa, jambo la nne walilokubaliana ni viongozi kuwalazimisha kupewa rufaa ya kutibiwa nje suala ambalo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amewaeleza madaktari wazingatie maadili ya kazi zao na kukataa kutoa rufaa kwa mtu asiyestahili awe kiongozi au asiwe kiongozi.

Alisema jambo la tano ambalo pande zote mbili zilikubaliana ni kuhusu madaktari waliofukuzwa.

"Hawa ni wale Interns waliokuwa wamerudishwa wizarani kutoka Muhimbili na kupangiwa hospitali za Temeke, Ilala, Mwananyamala na Lugalo. Hili ni jambo ambalo lilikuwa limemalizika kitambo na wote walikuwa wamerudi Muhimbili," alisema.

Rais Kikwete alisema jambo la sita ni kuhusu mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa na madaktari kuhusu kuboresha huduma ya afya ambalo Serikali imeliafiki.

Rais Kikwete alisema jambo la saba, ambalo pande zote walilokubaliana ni kuhusu kuongeza posho ya uchunguzi wa maiti.

Alisema jambo hilo jipya halikuwepo mwazoni, hata hivyo, Serikali imelikubali na posho hiyo imeongezwa kutoka Sh 10,000 hadi kufikia Sh100,000 kwa daktari na Sh50,000 kwa wasaidizi wake,” alisema.
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger