BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

MBUYU NDANI YA YANGA

Written By Koka Albert on Friday, August 24, 2012 | 3:32 AM

Beki mpya wa Yanga, Mbuyu Twite akifanya mazoezi jana asubuhi kwenye Uwanja wa Amahoro jijini Kigali. Yanga leo itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Rayon Sports. Picha na Doris Maliyaga.
BEKI mpya wa Yanga, Mbuyu Twite jana asubuhi alianza mazoezi rasmi na mabingwa wa Kombe la Kagame ambao leo watashuka dimbani kuivaa Rayon Sports kwenye Uwanja wa Amaholo jijini Kigali.

Katika siku za karibuni Mbuyu alitawala vichwa vya habari vya magazeti kufuatia sakata lake la kujiunga na Yanga muda mfupi baada ya Simba kutangaza kumsajili.

Akizungumzia na Mwananchi, Mbuyu alisema anajisikia vizuri kuungana na wachezaji wenzake na kuomba kupewa ushirikiano ili wafanikiwe kutwaa mataji mengi zaidi.

"Nimefurahi kujiunga na wenzangu, najisikia furaha kuwa nao na naahidi kushirikiana nao vizuri ili kuipa Yanga mataji ,"alisema Mbuyu aliyekuwa amevaa jezi namba 9 mgongoni wakati wa mazoezi hayo.

Naye kocha mkuu wa Yanga, Tom Saintfiet alisema,"Mbuyu ni mchezaji mzuri naamini ataisaidia Yanga, lakini hiyo yote itatokana na juhudi zake pamoja na wenzake."

Kocha Saintfiet alisema katika mchezo wao wa leo anategemea Mbuyu ataanzia benchi kwa kuwa ndio kwanza ameanza mazoezi na wenzake.

"Mazingira ya kambi ni mazuri, uwanja ni mzuri na tumefanya mazoezi kwa siku mbili (juzi na jana) na kesho (leo) tunacheza mechi bila shida," alisema Saintfiet.

Alisema,"mechi hiyo ni muhimu kwetu kwa sababu timu tunayocheza nayo ni nzuri na ina ushindani, naamini tutapata mazoezi ya kutosha hapa Kigali."

Katika mazoezi ya jana asubuhi kwenye Uwanja wa Amaholo, Yanga walianza kwa kukimbia na kufanya mazoezi ya viungo baada ya hapo, Saintfiet aliwataka wachezaji kucheza kwa nafasi na walitumia nusu Uwanja pamoja na kupiga mashuti.

Baada ya hapo walicheza mpira kwa mtindo wa mechi katika vikosi viwili tofauti.

Kwa mujibu wa mazoezi ya jana kikosi cha Yanga kitakuwa hivi katika mechi ya leo: Ally Mustapha, Shadrack Nsajigwa, Oscar Joshua, Nadir Haroub, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na Nizar Khalfan.

Mramba azidi kumkandamiza Mkapa mahakamani

Waziri wa zamani Fedha, Basil Mramba (Kushoto), Waziri wa zamani wa Nishati, Daniel Yona (Katikati) na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Grey Mgonja wakiwa ndani ya chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana, wakisubiri kuendelea kwa kesi yao ambapo wote wanatuhumiwa kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh11.7 Bilioni wakati wa uongozi wao. Picha na Venance Nestory
ALIYEKUWA Waziri wa Fedha Basil Mramba, jana aliendelea kumkandamiza aliyekuwa bosi wake na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, akimhusisha moja kwa moja na kutolewa kwa msamaha wa kodi kwa kampuni ya Alex Stewart Government Business Assayers.

Mramba aliyaeleza hayo jana wakati akijitetea dhidi ya tuhuma zinazomkabili za matumizi mabaya ya ofisi za umma na kuisababishia Serikali hasara ya Sh11.7 bilioni na kwamba alitoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo ili kutekeleza matakwa ya mkataba.

Alidai kuwa kifungu cha 4.3.1  kilichopo kwenye  mkataba huo ulioingiwa kati ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Alex Stewart Government Business Assayers kinasema malipo yoyote  yatakayolipwa na mkataba huo hayatotozwa kodi.
“Mimi nilichofanya ni kutekeleza  matakwa ya mkataba huu kwa sababu Waziri wa Fedha  pekee ndiye mwenye mamlaka  ya kutekeleza mkataba huo,” alidai Mramba.

Mramba alikiri kuruhusu gavana wa BoT kuilipa kampuni ya Alex Stewart,  Dola za Marekani 1 milioni kama malipo ya awali, kwa ajili ya kufanya maandalizi ya ukaguzi wa migodi ya madini, na kwamba fedha nyingine zingelipwa kwa awamu.
Mramba alisema aliruhusu malipo hayo kufanyika kutokana na kuwapo kwa barua  ya Mei 13, 2003, kutoka kwa Katibu Mkuu wa Rais, Patrick Mombo  kwenda kwa Katibu Mkuu wa Nishati na Madini kuhusu mkaguzi wa dhahabu ikisema “Rais amekubali Waziri wa Fedha na BoT watafute njia ya kuilipa kampuni ya Alex Stewart Government Business Assayers”.
“Maagizo yote mimi niliyachukulia  kama ni ya Rais, alikuwa akiagiza watendaji wake kutekeleza majukumu yote,”alisema Mramba na kuongeza kuwa kwa kuzingatia makubaliano hayo alitafuta fedha hizo kupitia bungeni katika Bajeti ya Serikali ya 2003/04.

Kuhusu mkataba, Mramba alisema kuwa anachofahamu yeye sheria ya BoT inampa mamlaka Gavana kuingia mikataba na kuisaini na kwamba mikataba yote aliyoingia na watu wengine ni lazima kodi isamehewe.
Mramba aliiambia mahakama hiyo kuwa, kampuni ya Alex Stewart Government Business Assayers ilikuwa ikitaka malipo bila kodi na kwamba, wao walikubali kutomtoza kodi kutokana na ushauri kutoka kwa wataalamu akiwamo gavana kuwa wamsamehe kodi vinginevyo wangemlipa zaidi. 
Hata hivyo, alisema mkataba baina ya BoT na kampuni hiyo haukuwahi kupitia katika kikao cha Baraza la Mawaziri. “Sikudhani kama angeweza kutiliana nao saini kwenye mkataba huo,  bila Baraza la Mawaziri kuridhia,”alisema Mramba.
Ushauri wa TRA

Mramba alibainisha kuwa Bethar Soka  ambaye alikuwa kwenye kamati iliyofanya mchakato wa kuitafuta kampuni hiyo ya ukaguzi wa dhahabu, aliomba kupata kauli ya TRA  kama kampuni ya Alex Stewart Government Bussines Assayers isamehewe kodi ama la, Mei 26, 2003.

Alidai kuwa baada ya  Soka kupeleka ombi hilo Mei 26, 2003, TRA katika majibu yao ya Juni 24, 2003 walisema kuwa hawapendekezi mkaguzi huyo wa dhahabu asamehewe kodi na kwamba barua hiyo ilipelekwa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha wakati BoT na kampuni ya Alex Stewart Government Business Assayers iliingia mkataba  Juni 14, 2003.

“Inaonyesha barua hiyo ya TRA ilichelewa  kwa siku 10, baada ya mkataba kusainiwa,  hata hivyo, ushauri huu wa TRA hatukuuhitaji  hata kama ungekuja  haungekuwa na manufaa,” aliongeza kudai Mramba.

Baada ya maelezo hayo, mmoja wa wanaosikiliza kesi hiyo, Hakimu Saul Kinemela, alimuuliza Mramba, Wizara ya Fedha  iliomba ushauri  huo TRA kwa kazi gani?

Akijibu swali hilo, Mramba alisema, "Siyo Wizara ya Fedha iliomba ushauri TRA, bali Soka aliomba ushauri huo kama mwanakamati iliyokuwa ikifanya mchakato wa kutafuta kampuni hiyo na  kwamba  Soka yeye  alikuwa ni mtumishi wa wizara yake.

Alibainisha kuwa  Soka  asingeweza  kumshauri  Waziri,  anayeweza kumshauri ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu.

Mbali na Mramba, wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja.
Jaji John Utamwa aliiahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 12, mwaka huu itakapoendelea na utetezi.
Utetezi wa awali

Mramba (71) alianza kujitetea, Agosti 22, mwaka huu  ambapo alidai kuwa Serikali iliiteua BoT ifanye kazi ya kutafuta  kampuni inayoweza kufanya kazi hiyo hivyo ikaingia mkataba na kampuni iliyochaguliwa  ya Alex Stewart Government Bussines Assayers.

Waziri huyo wa zamani aliongeza kudai kuwa aliyeagiza BOT kufanya kazi hiyo ya kumtafuta mkaguzi wa dhahabu ni Rais wa Awamu ya Tatu, Mkapa na kwamba wakati huo yeye akiwa Waziri wa Wizara ya Fedha alipewa jukumu la kuhakikisha gharama za kumlipa mkaguzi huyo zinapatikana ndani ya Serikali au BoT ama pengine popote.

Alifafanua kuwa kati yake yeye na gavana  hakuna aliyekuwa na mamlaka  juu ya mwingine na kwamba gavana alikuwa  na wajibu wa kufanya mchakato wa kumtafuta mkaguzi wa dhahabu.

Mramba alisisitiza kudai kuwa yeye hakuhusika kwenye mchakato huo kwa kumtafuta wala kumleta hapa nchini  wala kumtuma mwakilishi  yeyote  kumwakilisha kwenye kamati iliyoteuliwa  kufanya mchakato huo bali alipewa agizo la kumlipa.

“Mimi kama waziri sikuwa na mtu wangu kwenye ile kamati, lakini Wizara ilituma mwakilishi, ambaye alikuwa mwanasheria Bethar Soka wakati wa kuhoji kampuni mbili  ili wachague na kwenye kujadili vipengele vya mkataba,”alisema.

Inadaiwa kuwa, kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14, mwaka 2004, jijini Dar es Salaam, washtakiwa wakiwa watumishi wa umma, walitumia vibaya madaraka yao na kuisababishia Serikali hasara ya Sh11.7 bilioni.

Ilidaiwa kuwa washtakiwa hao waliipatia msamaha wa kodi isivyo halali, Kampuni ya M/S Alex Stewart ya Uingereza.

JIMBO LA IGUNGA WAZI

Written By Koka Albert on Tuesday, August 21, 2012 | 5:06 AM

*******Breaking newzzz???????????********
Mahakama kuu mkoa wa Tabora imemvua ubunge mheshimiwa Kafumu,kuanzia sasa jimbo la Igunga lipo huru bila mbunge

TP MAZEMBE YAFANYA MAUAJI, SAMATTA ANG'ARA, ATUMBUKIZA LA USHINDI

Written By Koka Albert on Monday, August 20, 2012 | 12:18 AM

Samatta
TOUT Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imejiweka sawa kwenye mbio za kuwania ubingwa wa Afrika, baada ya kuifunga  Zamalek ya Misri nyumbani kwao, Cairo mabao 2-1.
Shukrani kwake, mshambuliaji chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ‘Sama Goal’ aliyefunga bao la ushindi katika mchezo uliomalizika dakika chache zilizopita kwenye Uwanja wa chuo cha Jeshi, Al-Qahirah mjini Cairo, dakika ya 44, akiunganisha pasi ya Tressor Mputu Mabi.
Katika mchezo huo wa Kundi B, Himoonde alitangulia kuifungia Mazembe inayofundishwa na Lamine N'Diaye dakika ya 34 pasi ya Mputu, lakini Omotoyossi akaisawazishia Zamalek inayofundishwa na kocha Jorvan Vieira dakika ya 36, pasi ya Mohamed Ibrahim.
Ushindi huo wa kwanza ugenini kwa Mazembe katika hatua ya makundi, unaifanya Mazembe ifikishe pointi saba, baada ya kucheza mechi nne, kushinda mbili, sare moja na Berekum Chelsea na kufungwa moja na Al Ahly ugenini.
Al Ahly iliyotoa sare ya 1-1 na Berekum Chelsea nchini Ghana leo, bado inaongoza kundi hilo kwa pointi zake 10, wakati wababe wapya wa Ghana wanashika nafasi ya tatu kwa pointi zao tano na Zamalek wanashika mkia wakiwa hawana pointi hata moja.  
Kwa mara ya kwanza, katika mchezo wa leo, mshambuliaji mwingine wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu alikaa benchi, kwani awali amekuwa havai hata jezi.
Ulimwengu tangu asajiliwe Mazembe msimu uliopita, hii ni mechi yake ya kwanza anakaa benchi kwenye michunao ya Afrika, hizi zikiwa ni dalili njema kwamba anakaribia kuanza kucheza.
Katika mchezo huo, kikosi cha Zamalek kilikuwa; Abdel Wahed El Sayed, Mahmoud Fathalla, A. Mendomo, Sabri Rahil, Hazem Emam/ Said Kotta dk 77, Hani Saied, Ahmed Samir, Ibrahim Salah/ Mohamed Ibrahim Islam Awad/dk63, R. Omotoyossi/ Ahmed Gaafar dk71.
Mazembe; M. Kidiaba, H. Himoonde, F. Kasonde/ M. Ndonga dk 46
, J. Kasusula, S. Sunzu, J. Kimwaki, R. Kalaba, P. Ochan/ N. Kasongo dk 63, M. Mputu, G. Singuluma, M. Samata/ D. Kanda Dk 86.


Usajili Yanga watua TFF

Written By Koka Albert on Friday, August 17, 2012 | 6:56 AM

KLABU ya Yanga jana imewasilisha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), majina ya wachezaji 28 iliowasajili kwa ajili ya msimu ujao, yakiwamo pia majina ya Kelvin Yondani na Mbuyu Twite, ambao Simba wanadai wana mikataba nao.
Klabu ya Simba nayo inatarajia kupeleka usajili wake, yakiwemo majina ya Yondani na Twite, beki wa kimataifa aliyekuwa akicheza timu ya APR ya Rwanda kabla ya vigogo kila mmoja kudai ni mali yake.

Katika usajili wa Yanga uliowasilishwa jana TFF mbali na jina la Yondani na Twite, pia kuna makipa Yaw Berko, Ally Mustapha na Said Mohamed.

Walinzi wa Pembeni ni Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Juma Abdul, Oscar Joshua, David Luhende na Stephano Mwasika.
Walinzi wa kati ni Nadir Haroub, Ibrahim Job na Ladislaus Mbogo.

Viungo wa ulinzi ni  Athuman Idd,  Juma Seif Kijiko na Salum Telela, wakati wa pembeni ni Nizar Khalfan, Shamte Ally, Idrisa Rashid na Omega Seme.

Kwa upande wa viungo washambuliaji, Haruna Niyonzima, Rashid Gumbo na Nurdin Bakari, huku washambuliaji wakiwa Said Bahanunzi, Hamis Kiiza, Didier Kavumbagu na Jeryson Tegete

 Mbali na kikosi hicho pia Yanga imewasilisha majina 22 ya timu ya vijana U20 ambayo wapo pia wachezaji wa timu ya taifa Saimon Msuva na Frank Domayo ambayo majina yao yamepelekwa kwa timu ya vijana lakini wataitumikia timu hiyo kwa kucheza mechi za wakubwa.

Wengine, Geofrey Nyalusi, Yusuf Abdul, Said Manduta, Zuberi Juma, Said Mashaka, Benson Michael, Issa Ngao, Rashid Said.

Majina mengine kwenye orodha hiyo ni Frank Domayo, Omary Nasry, Clever Charles, Mwinyi Bakari, Mpenda Abdallah, Abdulahman Ally, Hussein Moshi, Abdallah Salum na  Rehani Kibingu.

Wengine ni Saimon Msuva, George Banda, Notikely Masasi, Suleiman Ussi na Kassim Jongo.

Hii Kweli Kali,,,,

Written By Koka Albert on Thursday, August 16, 2012 | 6:14 AM


Muamba 'devastated' after being told his career is over five months after heart attack

Written By Koka Albert on Wednesday, August 15, 2012 | 6:28 AM

Bolton midfielder Fabrice Muamba has spoken of his devastation at being forced to retire from football due to the heart attack he suffered in March.
The npower Championship club have announced that the 24-year-old - who had hoped to make a comeback - had made the decision to retire from the professional game after taking medical advice.
'While the news is devastating, I have much to be thankful for,' said Muamba.
Miracle recovery: Bolton's Fabrice Muamba suffered a heart attack in March
Miracle recovery: Bolton's Fabrice Muamba suffered a heart attack in March
Back at Bolton: Muamba (centre) at a club 'family fun day' last Sunday
Back at Bolton: Muamba (centre) at a club 'family fun day' last Sunday
Torchbearer: Muamba carried the Olympic Flame through Waltham Forest
Torchbearer: Muamba carried the Olympic Flame through Waltham Forest
'I thank God that I am alive and I pay tribute once again to the members of the medical team who never gave up on me.'
The Bolton midfielder 'died' for 78 minutes on the pitch at White Hart Lane after suffering a cardiac arrest during an FA Cup match.
Muamba collapsed while playing for Bolton against Tottenham at White Hart Lane in an FA Cup match on March 17.
He received lengthy attention on the pitch and it later emerged that his heart had stopped for 78 minutes.
Fateful day: Muamba suffered a cardiac arrest on the pitch at White Hart Lane in March
Fateful day: Muamba suffered a cardiac arrest on the pitch at White Hart Lane in March
Helpless: Bolton and Spurs players, and Wanderers boss Owen Coyle (centre), watched the terrifying scenes unfold
Helpless: Bolton and Spurs players, and Wanderers boss Owen Coyle (centre), watched the terrifying scenes unfold
Remarkably he made a stunning recovery and left hospital a month later.
Muamba told Bolton's official website: 'Since suffering my heart attack and being discharged from hospital, I have remained utterly positive in the belief I could one day resume my playing career and play for Bolton Wanderers once again.
'As part of my on-going recovery, last week I travelled to Belgium to seek further medical advice from a leading cardiologist.
'But the news I received was obviously not what I had hoped it would be and it means I am now announcing my retirement from professional football.
Tributes: Hundreds of get-well messages were left for Muamba at Bolton's Reebok Stadium while he was in hospital
Tributes: Hundreds of get-well messages were left for Muamba at Bolton's Reebok Stadium while he was in hospital
Rallying round: The football world united to send Muamba a get-well-soon message to the stricken Muamba
Rallying round: The football world united to send Muamba a get-well-soon message to the stricken Muamba
'Football has been my life since I was a teenage boy and it has given me so many opportunities.
'Above all else, I love the game and count myself very lucky to have been able to play at the highest level.
'I would also like to thank everyone who has supported me throughout my career, and the Bolton fans who have been incredible.
'I am blessed to have the support of my family and friends at this time.'
Thank you: Muamba with cardiologist Dr Andrew Deaner (left) and consultant cardiologist Dr Sam Mohiddin, the doctors who saved his life following his heart attack
Thank you: Muamba with cardiologist Dr Andrew Deaner (left) and consultant cardiologist Dr Sam Mohiddin, the doctors who saved his life following his heart attack
Bolton chairman Phil Gartside said: 'To have Fabrice here and with us is truly amazing and we are all very thankful for that.
'We are all hugely disappointed that Fabrice will be unable to return to his playing career but we have to be guided by the medical recommendations and the best interests of Fabrice.
'The most important thing is that Fabrice and his family have the rest of their lives ahead of them.'
Bolton boss Owen Coyle said: 'We have spoken with Fab and he knows we will always support him in whatever he wants to do and that we will always be here for him.
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Miracle man: Muamba with his fiancee Shauna after his stunning recovery
Miracle man: Muamba with his fiancee Shauna after his stunning recovery
'He is obviously massively disappointed that he won't be able to carry on his career, but everyone has seen what a fighter and strong person he is in mind and body.
'We know that he will go on to achieve great things and within all this disappointment, the most important thing is that he is here, alive, today.'
Muamba and his family fled war in the Democratic Republic of Congo, seeking asylum in the UK.
Despite arriving in London age 11, unable to speak English, he went on to achieve 10 GCSEs and three A levels and joined Arsenal's youth academy in 2002. He later joined Birmingham, before moving to Bolton in 2008.
All smiles: Muamba received an Honorary Degree from Bolton University
    All smiles: Muamba received an Honorary Degree from Bolton University

Dk Ulimboka: Niko tayari kwa lolote

Written By Koka Albert on Monday, August 13, 2012 | 2:07 AM


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Stephen Ulimboka baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam jana akitokea Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa.Picha na Fidelis Felix
ALAKIWA DAR KWA KISHINDO, ASEMA NIKO FITI TAYARI KWA KAZI
Raymond Kaminyoge na Geofrey Nyang’oro
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Stephen Ulimboka amerejea nchini jana akitokea Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa na kulakiwa na mamia ya watu huku akisema haogopi lolote na yupo tayari kwa kazi.

Dk Ulimboka aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere saa 8.15 mchana kwa ndege ya Shirika la South African Airways.
Baada ya kumaliza taratibu zote uwanjani na kutoka nje, Dk Ulimboka alilakiwa na umati mkubwa wa wananchi wakiwemo madaktari na wanaharakati ambao walijaza karibu eneo kubwa la lango la abiria wanaowasili jambo lililoonekana dhahiri kumsisimua kiasi hadi kufikia kububujikwa wa machozi.

Dk Ulimboka ambaye alipelekwa Afrika Kusini akiwa hawezi kutembea wala kula mwenyewe baada ya Juni 27 mwaka huu kutekwa na watu wasiojulikana, kupigwa na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili, kisha kutupwa katika Msitu wa Pande, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, amerejea akiwa anatembea na mwenye afya njema.

Akizungumza uwanjani hapo, Dk Ulimboka alisema: “Nawashukuru Watanzania kwa kuniombea, nawashukuru madaktari wenzangu, ndugu na jamaa zangu kwa kunisaidia kupata matibabu hadi leo hii narudi nyumbani nikitembea mwenyewe. Hivi sasa niko fiti na niko tayari kwa kazi yoyote.”
Uwanja huo ulikuwa umefurika mamia ya wananchi wakiwemo madaktari ambao walikuwa na shauku ya kumwona Dk Ulimboka, lakini wengi hawakufanikiwa kumwona.

Wingi wa watu ulisababisha kutokea kwa msuguano kati ya madaktari na waandishi wa habari. Wakati wanahabari wakitaka kumwuliza maswali Dk Ulimboka, baadhi ya madaktari walikuwa wakimzuia Dk Ulimboka kujibu maswali licha ya mwenyewe kuonekana kuwa tayari kuulizwa.
Baadhi yao walifikia hatua ya kushika kamera za waandishi huku wengine wakisema... “Mwacheni akapumzike bwana, kwa nini mnamsumbua sumbua.”

Baadhi ya madaktari hao walifikia hatua ya kutumia nguvu dhidi ya wapiga picha wa magazeti na televisheni na hivyo kusababisha vurugu na kelele nyingi katika eneo hilo.

Muda wote wakati Dk Ulimboka akielekea kwenye gari akiwa na maua mkononi aliyokadhibiwa baada ya kuwasili uwanjani hapo, madaktari hao walikuwa wakiimba nyimbo za kuhamasishana ukiwamo Wimbo wa Taifa huku wengine wakisema: “Mtakufa nyie, lakini si Dk Ulimboka.”
Baada ya kupanda gari aina ya Nissan Patrol nyeusi, madaktari hao na wanaharakati na wananchi wengine wakiongozwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Ananileya Nkya walilisukuma gari hilo hadi katika lango la kutokea katika uwanja huo.

Wanaharakati
Mbali na Nkya, kulikuwa na idadi kubwa ya wanaharakati wengine wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP, Usu Malya.
Wanaharakati hao walikuwa na mabango yaliyoandikwa,  “Dk Ulimboka karibu nyumbani uliumizwa kikatili ukitetea afya bora kwa Watanzania.”
Bango jingine lilisomeka: “Dk Ulimboka damu yako ilimwagika na kuamsha ari kwa wananchi kudai za afya.”

Jingine, “Dk Ulimboka wewe ni mpigania haki ya afya bora kwa wananchi wote Mungu na Watanzania wote tuko nawe.”
Malya akizungumza uwanjani hapo alisema kupona kwa Dk Ulimboka na kurejea nchini ni uthibitisho kwamba Mungu amesikia sauti za wanyonge.

“Dk Ulimboka alisimamia haki za madaktari na za Watanzania wote akitaka huduma bora zipatikane kwenye hospitali za umma kwa ajili ya Watanzania wote,” alisema.
Mkurugenzi wa Tamwa, Nkya alisema amefurahi kumpokea Dk Ulimboka akiwa hai kwa sababu hali yake ilikuwa mbaya wakati akipelekwa kwa matibabu nje ya nchi.

Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Edwin Chitage alisema kurejea kwa Dk Ulimboka akiwa amepona kunathibitisha kwamba nchi za wenzetu kuna vifaa vya tiba za kisasa na dawa.

“Kurejea kwa Dk Ulimboka ni mapenzi ya Mungu, huu ni uthibitisho kuwa hapa nchini hakuna vifaa tiba na dawa zinazoweza kusaidia wananchi kama ilivyo kwa wenzetu,” alisema Dk Chitage na kuongeza:

“Madaktari tumefarijika na hii imetupa nguvu licha ya vitisho tunavyopata tutaendelea kupigania haki zetu, haya ni mapambano ya muda mrefu, ”alisema.

Dk Chitage alisema kupona na kurejea nchini kwa Dk Ulimboka ni uthibitisho kuwa watu wengi wasio na uwezo wanapoteza maisha kutokana na kukosekana kwa vifaa tiba na dawa hapa nchini... “Madaktari tupo, lakini tatizo ni vifaa na dawa, hiki ndicho tunachopigania ni haki wananchi kupata huduma za afya nchini.”

Katibu Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk Rodrick Kabangila alisema kurejea kwa Dk Ulimboka kutasaidia kuwatambua watu waliohusika katika tukio la kumteka, kumpiga na kumtupa katika Msitu wa Pande.

“Sisi tumefurahi sana, Dk Ulimboka alisimamia haki za madaktari na sekta ya afya kwa ujumla, kurudi kwake kunatupa nguvu ya kuendelea kudai haki za madaktari na wananchi,” alisema.
Dk Ulimboka anarejea nchini huku Serikali na madaktari wakiwa hawajafikia mwafaka kuhusu madai yao.

Madai ya madaktari hao ni hali bora ya mazingira ya utoaji afya nchini, ongezeko la mishahara, posho za kufanya kazi katika mazingira magumu, posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi na posho za kuitwa kazini.

Safari ya Dk Ulimboka kwenda kwenye matibabu nchini Afrika Kusini ilitawaliwa na usiri mkubwa alipoondoka nchini Juni 31 mwaka huu, akisindikizwa na Dk Pascal Lugajo na kaka yake, Dk Hobakile Ulimboka na mke wake,  Dk Judith Mzovela.

Kutekwa
Dk Ulimboka alitekwa na kufanyiwa vitendi vya ukatili wakati akiratibu mgomo wa madaktari uliokuwa ukiendelea na aliokotwa na msamaria mwema akiwa amefungwa mikono na miguu akiwa katika hali mbaya.

Kutokana na tukio hilo, wanaharakati wa haki za binadamu waliituhumu Serikali kuhusika na tukio hilo, huku Serikali ikikana na kuliagiza Jeshi la Polisi kuwasaka waliohusika.
Akisimulia mkasa huo Dk Ulimboka alisema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Juni 27 katika Klabu ya Leaders, Dar es Salaam alikokuwa na daktari mwenzake na mtu mwingine aliyekuwa amemwita hapo (Leaders).

“Mara, katikati ya maongezi tukaona huyo mtu aliyeniita anaongea na simu. Ghafla tukiwa tunasema tuagane, wakaja watu kama watano hivi na bunduki, wakasema wewe na yule bwana mko free (huru), tunakuchukua wewe (Dk. Ulimboka). Sijakaa sawa, nikaona nimeshaburutwa nikaanguka kwenye lami, wakaniinua na kuniingiza kwenye gari nyeusi, lakini ilikuwa haina namba.”
Wakati Dk Ulimboka alipokuwa akiendelea na matibabu Afrika Kusini, Rais Jakaya Kikwete alisema Serikali haihusiki na kilichomtokea daktari huyo kwa kuwa alikuwa kiungo muhimu katika majadiliano baina ya Serikali na madaktari.

Rais Kikwete alisema hayo katika hotuba yake ya mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
“Dk Ulimboka alikuwa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na madaktari. Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam madaktari wanamwamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali,” alisema Rais Kikwete.
Alisema alichofanyiwa Dk Ulimboka kimemsikitisha na kumhuzunisha kwa kuwa ni kitendo cha kinyama na kinyume kabisa na mila na desturi za Tanzania.
Kauli ya Rais Kikwete kuhusu mgomo wa madaktari inafanana na ile iliyokuwa imetolewa awali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisema wanatambua kuwa Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka kuhusu kilichomtokea Dk Ulimboka, lakini ameshangazwa na hisia hizo akisema haoni sababu ya Serikali kufanya hivyo.

Dk Ulimboka alisafirishwa kwenda Afrika Kusini Juni 31, mwaka huu kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi baada ya jopo la madaktari waliokuwa wakimhudumia, kueleza mabadiliko ya hali ya afya yake, yaliyosababisha figo kushindwa kufanya kazi.

Ulinzi nyumbani
Nyumbani kwao, eneo la Ubungo Kibangu kulikuwa na watu kadhaa waliokuwa nje ya nyumba huku ulinzi ukiwa umeimarishwa.
Vijana wasiopungua watatu wakiwa wamevaa kawaida walikuwa wamekaa jirani na lango la kuingilia wakiratibu nyendo za wanaopita na wanaotaka kuingia katika nyumba hiyo iliyopo karibu na Shule ya Msingi Ubungo Kibangu.
“Watu walikuwa wengi hapa lakini wametakiwa kuondoka ili kutoa nafasi kwa dokta kupumzika na hakuna ambaye anaruhusiwa kuingia kwa sasa labda kama ni daktari mwenzao,” alisema kijana mmoja anayeishi jirani.

Awali, mama mmoja ambaye alifahamika kama ndugu wa familia hiyo anayeishi karibu na nyumba ya Dk Ulimboka alipoulizwa nyumbani kwa kiongozi huyo wa madaktari alihoji anatafutwa na nani na hata mwandishi walipojitambulisha alimtaka aondoke na kurejea alikotoka.
“Baba wewe nenda nyumbani kwako tu, usitake kujua zaidi,” alisema mama huyo majibu ambayo yalionekana kufanana na ya majirani wengi wa daktari huyo.
Nyongeza na Joseph Zablon

Malawi kutopigana na Tanzania

Written By Koka Albert on Friday, August 10, 2012 | 11:33 PM

MALAWI imesema imeondoa ndege zake zilizokuwa zikifanya utafiti wa mafuta katika Ziwa Nyasa kwa kuwa haitaki kuingia vitani, badala yake imeamua kupeleka mgogoro huo Mahakama ya Kimataifa.

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Mambo ya Ndani na Uhusiano wa Kimataifa kwa Mambo ya Kiusalama wa Malawi, Uladi Mussa alipokuwa akizungumza na gazeti linalochapishwa nchini humo la Nyasa Times.

“Nawahakikishia wananchi mtaendelea kuishi kwa utulivu. Tupo kwenye mazungumzo na Serikali ya Tanzania, bila shaka mambo yataenda vizuri. Kama hali ikishindikana tutalipeleka suala hili kwenye Mahakama ya Haki ya Kimataifa,” alisema Mussa.

Kauli ya Waziri huyo imekuja wakati baadhi ya wananchi wa Malawi wanaoishi katika Vijiji vya Karonga na Chitipa vilivyopo kando ya Ziwa Nyasa upande wa Malawi wakiwa wameanza kuvihama vijiji hivyo kuhofia usalama wa maisha yao.

Baadhi ya wakazi hao wamekaririwa na Nyasa Times wakisema kuwa wameamua kuchukua hatua hiyo kunusuru maisha kutokana na kuwapo kwa dalili za kutokea vita kati ya Malawi na Tanzania.
Waziri Mussa amesema suala hilo la mgogoro wa mpaka litaamuliwa kwa njia ya amani na hivyo kuwataka wananchi kuendelea na shughuli zao bila wasiwasi.

Waziri huyo aliwahakikishia wananchi hao kuwa Serikali ya Malawi ina ushahidi wa kutosha kuwa ziwa lote la Malawi (Nyasa)ni mali ya Malawi na Tanzania haina nguvu ya kuwasimamisha kuendelea na kazi ya kutafuta mafuta.

“Kimsingi hapa hakuna hoja ya kubishania. Wote tunajua ziwa hili ni mali yetu (Malawi),” alisema.
“Kama malalamiko haya yangekuwa yametolewa na Msumbiji, hapa tungekuwa na hoja ya kubishania, lakini si Tanzania.” alisisitiza.

Alisema ushahidi wao wa mipaka ni wa tangu mwaka 1890 wakati ambako wakoloni wa Uingereza na Ujerumani walitiliana saini juu ya suala hilo.

Aliendelea kueleza kuwa umiliki huo wa ziwa  umeongezewa nguvu na maazimio ya mwaka 1963 ya Wakuu wa uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (OAU) kwamba wanachama wanapaswa kuheshimu mipaka waliyorithi kwa wakoloni.

Kauli za wananchi
Wakati Serikali ya Malawi ikitoa msimamo huo watu kadhaa waliohojiwa wameonyesha hofu ya nchi hizo kuingia katika vita.

Heckley Christopher ambaye ni raia wa Malawi anayefanya biashara eneo la Mbambabay mkoani Ruvuma anasema: " Malawi ni nchi ndogo sana kupigana na Tanzania, ni nchi yenye mikoa minne tu, kukiwa na vita itaangamia mara moja."

Raia mwingine wa Malawi ni Vilion Gordon ambaye alisema Tanzania na Malawi ni marafiki wa siku nyingi, hivyo hawana sababu za kugombania ziwa ambalo lilikuwapo tangu enzi hizo.

"Nashauri wakae chini wapatane, kwa nini tugombane sasa wakati ziwa hilo lilikuwapo tangu enzi hizo?"alisema.

Mtanzania mkazi wa Kijiji Lundo kilichoko Mbambabay mkoani Ruvuma, Zakhia Chengula ameitaka Serikali ya Tanzania kuendelea kuimarisha ulinzi na kukubali kuingia katika mazungumzo na Malawi badala ya kufikiri vita.

"Hapa sisi ni kwetu, vita ikiingia sisi tutakufa tu hakuna pa kukimbilia. Tunaiomba Serikali iimarishe ulinzi eneo hilo na ikae na Malawi kuzungumzia mgogoro huo," alisema.

Mkuu wa Wilaya mpya ya Nyasa, Ernest Kahindi alisema hakuna hofu yoyote kwa wakazi wanaoishi kando ya Ziwa Nyasa upande wa Tanzania.
Amewataka wananchi hao kuendelea na shughuli zao za uzalishaji mali kama kawaida kwani suala hilo sasa linashughukiliwa kitaifa.

"Mwanzoni kulikuwa na hofu kubwa, lakini baada ya Serikali ya Tanzania kutoa tamko la kutaka ndege za Malawi ziondoke na zenyewe kutii amri hiyo, hakuna tatizo lolote," alisema na kuendelea;
"Shughuli katika eneo hili zinaendelea kama kawaida. hakuna mwananchi aliyepigwa risasi wala ndege iliyotunguliwa, mambo yako shwari."
Jeshi laimarisha ulinzi

Katika hatua nyingine Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limeimarisha ulinzi katika mwambao wa Ziwa Nyasa na kupiga marufuku wananchi kukatisha eneo lao la jeshi.

Super Sport kumjaribu Bocco

Written By Koka Albert on Thursday, August 9, 2012 | 5:25 AM

MSHAMBULIAJI wa Azam FC, John Bocco ataondoka wiki ijayo kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa na klabu ya Super Sport ya nchini Afrika Kusini.

"Nimepata taarifa kwamba natakiwa kwenda kufanya majaribio Afrika Kusini, lakini ukweli ni kwamba viongozi wangu bado hawajaniambia," alisema Bocco.

“Nasubiri kuelezwa taarifa za safari hiyo kama kweli ipo kama ambavyo nimekuwa nikisikia kwa watu mbalimbali na vyombo vya habari," alisema Bocco.

Habari kutoka chnazo cha kuaminika ndani ya klabu ya Azam, kimethibitisa taarifa za Bocco kuitwa Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya majaribio.

Bocco, mfungaji wa mabao matatu katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Simba, robo fainali ya Kombe la Kgame zaidi ya wiki mbili zilizopita, alionyesha kiwango cha juu kwenye michuano hiyo.

“Anakwenda kufanya majaribio, hizi ni taarifa za kweli kabisa," alisema mpashaji huyo wa habari.
Aliongeza: "Ni vigumu kuamini nayokueleza, lakini fahamu kwamba (Bocco) ana safari ya kwenda kucheza kwa majaribio nchini Afrika Kusini."

Wakati wa michuano ya Kombe la Kagame, Bocco alifunga mabao matato, na kukamatana nafasi ya tatu ya ufungaji bora.Msimu uliiopita wa Ligi Kuu Bara, Bocco aliibuka kuwa mfungaji bora baada ya kukwamisha wavuni mpira mara 18 na kuwapiku washashambuliaji, Emmanuel Okwi, Kenneth Asamoah na Davies Mwape.

Ndege za Malawi zafungasha virago Ziwa Nyasa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe
SIKU chache baada ya Serikali kuzitaka ndege zinazozunguka Ziwa Nyasa upande wa Tanzania kufanya utafiti wa mafuta kuondoka mara moja, Serikali ya Malawi imetii na kuziondoa kampuni zinazofanya kazi hiyo katika ziwa hilo.

Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yake Jumatatu iliyopita, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe aliitaka Malawi kuziondoa ndege na kampuni zinazofanya utafiti wa mafuta katika eneo hilo kwa kuwa ni mali ya Tanzania.

Mbali na Waziri Membe, viongozi wengine waliozungumzia mgogoro huo na kuitaka Malawi iache uchokozi ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Edward Lowassa.

Wakati Sitta akiwataka Watanzania kuendelea na shughuli zao bila hofu kwa kuwa Serikali iko tayari kwa tishio lolote, Lowassa alisisitiza kuwa Tanzania imejiandaa kiakili na kivifaa kuingia vitani na Malawi kama italazimika kufanya hivyo.

Jana kwa nyakati tofauti, Wakuu wa Wilaya nne zilizo mpakani mwa Tanzania na Malawi za Ileje, Mbozi, Mbeya, Kyela na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro walieleza kuwa mara baada ya kauli hizo, ndege hizo za Malawi ziliondoka na kampuni zilizokuwa zikitafiti mafuta katika Ziwa Nyasa zimeacha.
“Hapa tuko cool (tulivu) kabisa tangu zile ndege zilipoacha kuruka, tofauti na hizo kauli zinazotolewa na viongozi wa Serikali (ya Malawi),” alisema Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Dk Michael Kadeghe na kuongeza:

“Hapa niko kwenye Sherehe za Nanenane na Malawi wana banda lao nimetoka kulitembelea. Hali iko shwari, tunaendelea na uhusiano kama kawaida.”

BREAKING NEWS ....NAIBU WAZIRI AFRIKA MASHARIKI APATA AJALI JIONI HII

Written By Koka Albert on Tuesday, August 7, 2012 | 7:06 PM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhABQMiDFDn92_2t29HUcCWR82ZdudREmd2ECVVcSyp_rlP39QCDrj-s3eysIrvu2vKkOzJOx3x3qeGG8RRzEZnJC7AMlHa4eWHSww0_n6UMLn_YPG6mUNHLnTMKxx5uC_d2-vnG4kocx81/s1600/NAIBU+2.JPG 
Wananchi wakitazama gari la naibu waziri wa Afrika Mashariki
 
 
Mzimu wa ajali kwa wabunge na viongozi wa Taifa umeendelea kushika kasi hapa nchini baada Naibu waziri wa Afrika Mashariki,Abdullah Juma Abdalla Saddallah na familia yake kupata ajali mbaya eneo la Tumbi Kibaha wakati akitoka Bungeni na familia yake.

Ajali hiyo mbaya ilitokea majira ya jioni hii wakati naibu waziri huyo akitokea Bungeni kuelekea jijini D'salaam akiwa na mkewe pamoja na watoto wake wawili na a dereva wake ambaye aliumia vibaya na kukimbizwa hospital yaTumbi-KibahaMashuhuda wa ajali hiyo akiwemno Abdulaziz Video amedai kuwa chanzo cha ajali hiyo inasemekana alikuwa analikwepa Lori alilokuwa akipishana nalo na hivyo gari lake kuhama njia na kupinduka .

Imeelezwa baada ya ajali hiyo umati wa wananchi wakiwemo vibaka walifika eneo hilo kutaka kupora mali mbali mbali ila hawakuweza kufanikiwa baada ya raia wema kusaidia kuepusha hali hiyo .

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Taifa Mohamed Mpinda alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo baada ya kuhojia na mwandishi wa habari hizi na kuwa hali ya naibu waziri huyo si mbaya sana zaidi ya dereva wake ambaye ameumia kichwani."

Taarifa ambayo nimeipata kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa 11 jioni na tayari nimewasiliana na kamanda wa polisi wa mkoa huo na amekwenda eneo la tukuio"

Cazorla raring to go as Spain midfielder finally completes £16.5m move to Arsenal

Santi Cazorla has revealed he can't wait to get started at Arsenal after completing his £16.5million move.
The 27-year-old Spain international arrives at the Emirates from Malaga as Arsene Wenger shakes up his squad.
Cazorla said: 'I'm so happy to be joining Arsenal. This is a club with great players, a fantastic stadium and huge support.
Already there! Santi Cazorla was already in training with Arsenal in Hennef, Germany on Tuesday
Already there! Santi Cazorla was already in training with Arsenal in Hennef, Germany on Tuesday
Santi Cazorla holds up his new Arsenal shirt after his £16.5million signing was finalised
Santi Cazorla holds up his new Arsenal shirt after his £16.5million signing was finalised
'The club has one of the best managers in football and their style of play is recognised and admired all over the world.

'I'm so excited to be joining one of the greatest teams in Europe and also in the Premier League. I will do my best to help Arsenal challenge for trophies and make all the supporters happy.'
Wenger, who has already signed Lukas Podolski and Olivier Giroud, is delighted to have finally secured Cazorla.

He said: 'Santi Cazorla is a great signing for us. He is a player with good experience at both club and international level, who will add significant quality to our squad.
'He is a versatile, attacking midfield player who can play comfortably on either side of the pitch or centrally. He has good pace, is technically gifted and will be a huge asset to Arsenal Football Club. We are delighted that he is joining us.'

Cazorla is already with Arsenal at their German training camp, where he has been since Monday when his now former employers, Malaga, allowed him leave while the finer points of the deal were eked out by the two clubs.
The tricky midfielder is on course to make his debut against Cologne on Saturday in a bid to slot in with his new side as quickly as possible.

After making his way through the ranks at Villarreal, the 27-year-old earned his first Spanish cap in 2008, and has been part of their title-winning set-up ever since, including their most recent triumph at the European Championships in Poland and Ukraine earlier this summer.
Cazorla seemed at ease with his compatriot and new team-mate Mikel Arteta
Cazorla seemed at ease with his compatriot and new team-mate Mikel Arteta

Means business: Cazorla is hoping he can improve on Arsenal's third place in the Premier LeagueCazorla seemed at ease with his compatriot and new team-mate Mikel Arteta
Means business: Cazorla is hoping he can improve on Arsenal's third place in the Premier League

CUF yataja suluhisho migomo ya walimu

Written By Koka Albert on Monday, August 6, 2012 | 12:09 PM


Geofrey Nyang’oro
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahimu Lipumba amewataka  walimu kuungana na chama hicho kuendesha harakati za kuondoa   CCM madarakani kwa kuwa imeonyesha wazi haina dhamira ya  kutekeleza madai yao.
Profesa Lipumba ambaye pia kitaaluma  ni mtaalamu wa  uchumi alisema chama chake kamwe hakiungi mkono mgomo, lakini kinatambua madai ya walimu na umuhimu wa kuyatatua.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, alisema ingawa katika Ilani ya CCM na hata ahadi  za viongozi wake zilieleza bayana kuwa ingeboresha masilahi ya wafanyakazi, hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ya Agosti Mosi mwaka huu inadhihirisha kuwa CCM haina nia hiyo.


“Katika hotuba ya Rais  ya mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu iliyosomwa mbele ya wahariri wa vyombo vya habari Agositi mosi, sehemu ya hotuba inasema madai ya safari hii ni makubwa mno,yametuzidi kimo.Athari za kuyatekeleza yalivyo yataifanya serikali kutumia asilimia 75 kwa ajili ya mishahara”alisema  Profesa Lipumba akinuuu hotuba ya Rais Kikwete na kuongeza:

“Ukiangalia nukuu hizi,zinathibitisha dhana ya serikali ya CCM katika kutekeleza madai ya walimu,Rais hataji serikali ina mpango gani na kwa kiasi gani itatekeleza mipango hiyo,serikali isiyo na mipango kwa vyovyote vile haiwezi kuwatumikia wakulima na wafanyakazi wa nchi yetu”alisema.
“Sisi (CUF) tunawashauri walimu watambua kuwa CCM haipo madarakani kutatua matatizo yao,muhimu walimu wakaungana wote ili kuhakikisha CUF inaongoza dola na kuleta mabadiliko.
Profesa Lipumba alisisitiza kuwa migogoro inayoendelea hapa nchini ni  uthibitisho wa kuwapo kwa ombwe la uongozi uliojikita katika ,usiri, uzembe, dharau na ubabe.
“Inasikitisha kwamba mvutano kati ya serikali na walimu hauishi, mazingira ya kuaminiana katika kutatua mgogoro, serikali ya CCM haiwezi kutatua kero za walimu na kuwapa motisha wa kuboresha elimu kwa watoto wetu”alisema Lipumba.
Msimamo wa CUF kuhusu mgomo
Mwenyekiti huyo wa CUF alisema chama chake ingawa hakiamini kuwa mgogoro unaweza kumalizwa kwa migomo kinaunga mkono madai ya walimu kuwa ni ya haki.
“Pamoja na kuwa (CUF) hakiamini migomo ya wafanya kazi kama suluhisho la kuisha kwa matatizo yao na bila kuingilia maamuzi ya mahakama tunasisitiza kuwa walimu wana madai sahihi na yanapaswa kupewa kipaumbele”alisema.

Alisema walimu wanafanya kazi katika mazingira mgumu wakati serikali ya CCM inayojiita sikivu haijawasikiliza na kutekeleza madai yao zaidi ya kutishia kuwafukuza kazi na kuwakamata baadhi kuhusiana na mgomo.
Alisema chama chake kilitegemea Rais Kikwete angetoa kauli mahsusi ya mpango maalumu wa kushughulikia madai yao lakini imekuwa tofauti baada ya kusema serikali yake haina uwezo wa kutekeleza.

Lipumba alisema majibu ya Rais Kikwete yalijumulisha madai ya ongezeko la mishahara ya walimu na kuwa ongezeko la wafanya kazi wote serikalin ambalo linafanya kufikia asimilia 75 aliyosema haiwezekani.
Athari za mgogoro wa walimu
Katika mkutano huo Profesa Lipumba alisema athari zitokanazo na mgogoro baina ya walimu na serikali ni kubwa zitakazoweza kudhoofisha juhudi za kujinasua kutoka katika  dimbwi la umasikini.

“Kama walimu wataendelea kulipwa namna hii,ina maana ualimu ni wito na si taaluma kama zilivyo taaluma nyingine muhimu, tusishangae kuwa walimu wetu wataendelea kuuza bagia badala ya kufundisha kwa kuwa kipato chao hakitoshi”alisema.


Alisema tayari kumekuwa na athari kuwa nchini za kuporomoka kwa elimu na kwamba hayo ni matokeo ya serikali kushindwa kuboresha mazingira ya elimu ikiwamo mishahara na vitendea kazi.


“Hivi sasa tumepiga hatua katika suala zima la uandikishaji wanafunzi ambapo tumetoka asilimia 51 mwaka 1990 na kufikia asilimia 97 mwaka 2009,lengo la kuandika watoto wote wenye umri wa kuanza darasa la kwanza limefikiwa tatizo ubora wa elimu”alisema Lipumba.


“Utafiti wa uwezo uliofanywa na Taasisi isiyo ya kiserikali umebaini kuwa watoto watano wanaomaliza darasa la saba mmoja kati yao hawezi kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, katika kipindi cha miaka saba watoto hao wanaelekea kubaki mbumbumbu (hawajui kusoma wala kuandika)maishani mwao….”alisema Lipumba.


Profesa Lipumba alisema ni muhimu kuboresha elimu ya Msingi ili wanaoingia shule iweze kuwasaidia na kwamba ikiwa hatutafanya hivyo taifa liko hatarini kurejea kwenye elimu ya watu wazima (UPE) kama ilivyokuwa miaka ya 80.


Alisema kukua kwa uchumi wa  kisasa na wenye uwezo kuboresha maisha ya wananchi kunategemea wafanya kazi wenye ujuzi na maarifa na kwamba yote yanatokana na elimu bora.

Hivi karibuni Chama cha Walimu Tanzania (CWT)kilitangaza mgomo wa walimu nchi nzima na usio na ukomo uliodumu kwa siku tatu kabla ya kubatilishwa na mahakama.

9.63 seconds... Legend Bolt retains 100m crown after stunning victory over rival Blake sees him shatter his OWN Olympic record

Fittingly, it was the weekend that celebrated 50 years of Jamaican independence. Here were just 9.63 blistering seconds of it. At the end of the shortest Olympic race in history, two men were quite noticeably independent and away from the rest of the field. There was daylight between Usain Bolt and Yohan Blake, but clear air again between Blake and the chasing pack.

The Jamaicans — friends, training partners at the Racers Club in Kingston, now the fiercest rivals on the track — were out on their own. When it came down to it, however, one Jamaican was simply more independent than the other.

Bolt did it again. He did it as he said he would. As predicted, this was his time. Bolt became the first athlete this century to retain his Olympic 100 metres title, the first since Carl Lewis in 1988. Nobody stays the fastest man in the world for long and there were many who thought Bolt would repeat the brief flickering of many past champions. They were wrong, so very wrong.
*SCROLL DOWN TO WATCH VIDEO OF USAIN BOLT'S VICTORY IN THE 100 FINAL
Simply the best: Usain Bolt crosses the finishing line to win gold in the men's 100 metres final
Simply the best: Usain Bolt crosses the finishing line to win gold in the men's 100 metres final

100m... The final


Having given the field, even the brilliant Blake, a head start, he then accelerated. It was as if Batman had flicked the switch on the Batmobile, the one that sends the machine into warp speed. We almost expected to see an ignition of white-hot flame at Bolt’s tail.

And that is what Bolt is, in essence. A  latter-day superhero. He draped the  Jamaican flag around his shoulders like a Caped Crusader, too, and mimed firing his arrow as if an Olympian of old. He is old, Bolt, yet so very new.

His talent is one of the purest skills of all: the ability to run faster than any other man. But his manner is modern. He knows his place in sport’s galaxy, his status, and what it represents. At the pinnacle stands the heavyweight boxing champion and the world’s fastest man; except Bolt has more personality in his discarded woolly hat than the Klitschko brothers have in a lifetime of  perfect punishing victories. If Bolt were a boxer, even Muhammad Ali’s Greatest status might have been under threat.
He is charismatic, mesmerising. Once he entered the track nobody could take their eyes from him; and then when he started running, blink, and he was gone.

At the Ritzy Cinema in Brixton, Bolt as Batman was further emphasised. Jamaica Day celebrations in the area had segued jubilantly into the main event of the night. On the big screen, The Dark Knight Rises gave way to Bolt and a free showing of the BBC Olympics coverage played to an audience comprising the nearest thing a Jamaican athlete could get to a partisan crowd, so far from his island.

Not that he could have heard them as he sped into history. Not that any athlete could hear much above the cacophony of the  Olympic Stadium. After Britain’s Super  Saturday, this was tagged Supersonic  Sunday, as if any further showbiz hype was required. The fastest men in the world know they are the players of the Olympic meeting without further encouragement. They preen, they strut, they perform for the  cameras, and that is just in the heats.

Dip for the line: Bolt finishes ahead of Yohan Blake (second right) and Justin Gatlin (third right) to win the Olympic gold medal
Dip for the line: Bolt finishes ahead of Yohan Blake (second right) and Justin Gatlin (third right) to win the Olympic gold medal


Lightning Bolt: The Jamaican set a new Olympic record after winning the 100m in a time of 9.63 seconds
Lightning Bolt: The Jamaican set a new Olympic record after winning the 100m in a time of 9.63 seconds
Making his point: Bolt celebrates after crossing the finishing line in first in the 100m final at the London Olympic Games
Making his point: Bolt celebrates after crossing the finishing line in first in the 100m final at the London Olympic Games
History boy: Bolt bathes in the glory of his brilliant victory in London's Olympic Stadium
History boy: Bolt bathes in the glory of his brilliant victory in London's Olympic Stadium

The finalists: (from left) Churandy Martina, Ryan Bailey, Usain Bolt, Justin Gatlin, Yohan Blake, Tyson Gay, Asafa Powell and Richard Thompson
The finalists: (from left) Churandy Martina, Ryan Bailey, Usain Bolt, Justin Gatlin, Yohan Blake, Tyson Gay, Asafa Powell and Richard Thompson

Close call: Bolt did not run away with the race as he had done four years ago in Beijing, with Blake, Gatlin and Gay all running super quick times
Close call: Bolt did not run away with the race as he had done four years ago in Beijing, with Blake, Gatlin and Gay all running super quick times

T.I.D ft Mangwear-Kiuno-official Video


Yanga waingia kambini, kujazwa noti leo

Written By Koka Albert on Saturday, August 4, 2012 | 4:34 AM

WACHEZAJI wa Yanga, leo watakabidhiwa 'mzigo' wao ikiwa ni shukurani yao kwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Kagame, michuano iliyomalizika jijini Dar es Salaam.

Yanga ilitwaa ubingwa wa Kombe la Kagame na kuzawadiwa Sh47mil ambazo zitagawanwa kwa wote walioshiriki kuleta ubingwa huo kwa mwaka wa pili mfululizo.

Msemaji wa Yanga, Luis Sendeu alisema jana kuwa wachezaji hao watapewa fedha hizo baada ya kukamilika kwa mchakato wa nani atapata nini.

Katika hatua nyingine, wachezaji wa Yanga wataanza mazoezi yao leo asubuhi kwenye Uwanja wa Kaunda ya kujiandaa na mechi za Ligi Kuu na zile za BankABC baada ya mapumziko ya siku tano ya Michuano ya Kagame.

Sendeu alisema kuwa baada ya mapumziko hayo wachezaji pamoja na benchi zima la ufundi la timu hiyo watajikita zaidi katika hatua nyingine ya mazoezi ya timu hiyo ya kujiandaa na michuano ya Ligi Kuu.

"Kikosi chetu kesho (leo) kinaanza tena mazoezi yake yake ya kujiandaa na Ligi Kuu kufatia benchi letu la ufundi kuwapa wachezaji wiki moja ya mapumziko mara baada kumalizika kwa michuano ya Kagame.

Katika hatua nyingine, wachezaji wa kikosi hicho Nurdin Bakari pamoja na Salum Telela wataendelea kuwa kando na kikosi hicho kutibu majeraha yao ya muda mrefu baada ya kuumia wakijiandaa na Kombe la Kagame.

Mahakama yapiga ‘stop’ mgomo wa walimu

Written By Koka Albert on Friday, August 3, 2012 | 2:52 AM


Rais wa Chama cha Walimu Tanania (CWT), Gratian Mukoba akiwa ameambatana na baadhi ya walimu wakati wakitoka Mahakama kuu, kitengo cha kazi jijini Dar es Salaam jana kusikiliza maamuzi ya mahakama hiyo kuhusu kesi yao dhidi ya Serikali. Mahakamama ilisitisha mgomo wa walimu ikidaiwa kuwa ni batili. Picha na Venance Nestory
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Kazi imesitisha mgomo wa walimu na kuwataka kurudi kazini mara moja.
Mahakama hiyo pia imeuagiza uongozi wa Chama cha Walimu (CWT) kuandaa taarifa kwa umma, kutangaza kusitishwa kwa mgomo huo kama walivyowatangazia wanachama wake wakati ulipoanza.

Mahakama hiyo ilisitisha mgomo huo jana wakati ilipotoa uamuzi wa maombi yaliyowasilishwa mahakamani na Serikali. Jaji Sophia Wambura aliyekuwa akisikiliza maombi hayo, alisema mgomo huo ni batili kwa kuwa haukukidhi masharti ya Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini.

Katika uamuzi wake, mahakama hiyo pia imekitaka CWT kulipa hasara za kifedha au kuwafidia wanafunzi vipindi vya masomo walivyovikosa, hususan wale wa darasa la saba. Mahakama hiyo ilikwenda mbali zaidi na kuwaonya walimu na Serikali kwa kitendo cha kuzungumzia suala hilo wakati tayari lilikuwa mahakamani.

Jaji Wambura alisema kitendo hicho ni uvunjaji wa Ibara ya 4 na ya 107 A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya  mwaka 1977 kama ilivyokwisha kurekebishwa mara kadhaa.

“Vinginevyo, hakukuwa na haja ya kuja hapa mahakamani kabisa. Kama kila mmoja ataachwa awe jaji, itakuwa ni kero na uvunjaji wa utawala wa sheria,” alisema Jaji Wambura.

Jaji huyo alizitaka pande zote kurudi kwenye meza ya mazungumzo na kushauri kuwa, ikiwezekana zialike watu wenye ujuzi wa masuala ya sheria za kazi na uhusiano kazini kuwasaidia ili kufikia makubaliano kwa  amani.

“Chini ya Masharti ya Kifungu cha 81 (1) (2) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini, natamka kuwa mgomo ambao umekuwa ukiendelea kwa siku tatu sasa ni kinyume cha sheria. Ninaamuru usitishwe na walimu wote warudi kazini mara moja,” aliagiza Jaji Wambura.

Msingi wa uamuzi
Jaji Wambura alirejea hoja zilizowasilishwa na pande zote, waombaji wakiwakilishwa na Mawakili wa Serikali Wakuu, Obadia Kameya na Pius Mboya na wajibu maombi (CWT) wakiwakilishwa na Wakili Gabriel Mnyele.

Alisema baada ya kupitia hoja zote na vielelezo vilivyoambatanishwa kwenye hati za viapo pamoja na majibu husika, amebaini kuwa na kuridhika kuwa mgomo huo haukufuata sheria.

Alisema CWT hawakufuata masharti ya kifungu cha 80 (1), cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini na kwamba kulikuwa na dosari kwani kura zilizopigwa zilipotosha wanachama , kwa sababu hazikuwa za kuunga mkono mgomo, bali madai ya walimu.

Jaji huyo alisema upigaji kura ulikuwa ni batili kwani walimu hawakufahamishwa matokeo ya mgomo huo na kwamba haukuzingatia taratibu.

Pia alisema taarifa ya mgomo iliyowasilishwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi Julai 27, 2012 saa 9:00 alasiri wakati mchakato wa upigaji kura ukiwa unaendelea, pia ilikuwa ni batili.

Dosari nyingine ni kutoeleza kikomo cha mgomo na kutokubainisha kama watawalipa wanachama wake wakati wa mgomo.

Aliongeza kwamba, CWT kwa kushindwa kutimiza masharti ya kanuni ya 42 na 43 za sheria husika, kulisababisha kero zisizo za lazima.

Alisisitiza kuwa kitendo cha CWT kuwasilisha taarifa ya mgomo Ijumaa saa 9:00  wakidai  mgomo unaanza Jumatatu, hali wakijua kuwa Jumamosi na Jumapili hazikuwa siku za kazi, ni kinyume cha kanuni na kilifanywa kwa nia mbaya.

Wakili wa CWT, Mnyele alisema anasubiri maelekezo ya wateja wake, lakini Rais wa CWT, Gratian Mukoba alisema watatoa tamko leo.

Mgomo waendelea
Katika baadhi ya shule za Dar es Salaam jana mgomo uliendelea na kusababisha wanafunzi kadhaa kuonekana wakizurura mitaani.

Shule hizo zimo za sekondari na  msingi ambazo ni Mchangani, Mwananyamala Kisiwani, Kunduchi, Pius Msekwa, Pwazo, Pwani, Mtakuja, Mtongani na Kisauke katika manispaa ya Kinondoni.

Walimu walioonekana maeneo ya shule hizo walikuwa wachache huku wanafunzi nao wakionekana wakisambaa hovyo katika maeneo ya shule.

Baadhi ya wanafunzi walikiri kwamba mahudhurio yao pia yamezorota.

Mwalimu Mkuu Msaizi wa Shule ya Msingi Mwananyamala Kisiwani, Abwalib Mfinanga alisema; “Kama unavyoona, walimu hawaingii madarasani kufundisha kutokana na mgomo unao endelea.”

Katika Manispaa ya Temeke baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba walisikika wakilalamika kutotendewa haki.

“Walimu wetu wamesoma na sisi tunataka tuwe kama wao, tunawaomba  watufundishe  ili tuweze kufikia kiwango kama chao,” alisema mwalimu Alfred Mwinuka.

Katika shule ya Msingi Amani wanafunzi walionekana wakicheza katika viwanja vya michezo na  wakati katika shule ya Msingi ya Dovya, baadhi ya madarasa yalikuwa yamefungwa huku baadhi ya  wanafunzi wakiwa wamezagaa nje.

Mwanafunzi Saleh Juma alisema kuwa jana ni mwalimu mmoja tu aliyeingia darasani, na baada ya muda mfupi aliondoka. Mwalimu Mkuu peke yake ndio tunamuona akipita madarasani,” alisema Saleh.
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger