Beijing, China
SHABIKI wa soka nchini China, Jiang Xiaoshan amefariki baada kukaa siku 11 bila kulala akiashuhudia kwenye televisheni mechi zote za michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya inayoendelea Poland na Ukraine.
SHABIKI wa soka nchini China, Jiang Xiaoshan amefariki baada kukaa siku 11 bila kulala akiashuhudia kwenye televisheni mechi zote za michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya inayoendelea Poland na Ukraine.
Shabiki huyo anadaiwa kuziunga mkono England na Ufaransa kwenye michuano hiyo, alifariki kutokana kutokana na mwili kuchoka Jumanne wiki hii.
Kwa sababu ya muda tofauti wa kurushwa kwa mechi hizo, Xiaoshan hakuwahi kulala kwa muda wote huo na badala yake alikesha kuangalia mechi hizo na kisha siku iliyofuata kwenda kazini.
Kwa mujibu wa mtandao wa sina.com, shabiki huyo alishuhudia kwenye televisheni mchezo kati ya Ireland na Italia ambapo alirejea nyumbani saa 11 alfajiri na alipoamua kulala hakuamka tena.
Taarifa zaidi zilidai kuwa matumizi ya tumbaku na na pombe na kuchoka kulikotokana na kushindwa kulala, kunaelezwa kuwa chanzo cha sababu.
Mechi zote alizoangalia Xiaoshan ni sawa na dakika 1890, ambapo aliweza kushuhudia mabao 51 kabla ya kufariki kwake.
Post a Comment