Home » » LEMA ASHINDA RUFAA YAKE NA SASA KUENDELEA NA UBUNGE TENA WA JIMBO LA ARUSHA

LEMA ASHINDA RUFAA YAKE NA SASA KUENDELEA NA UBUNGE TENA WA JIMBO LA ARUSHA

Written By Koka Albert on Thursday, December 20, 2012 | 11:35 PM

Godbless Lema ambaye ni mbunge wa Jimbo la Arusha Akiongea na wafuasi wa Chadema na baadhi ya wananchi waliojitokeza kusikiliza hukumu ya kesi yake mara baada ya kushinda rufaa yake leo katika Mahamaka Kuu 
..............................................
Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema ameshinda rufaa yake ambayo ilikua inasikilizwa leo katika Mahakama Kuu. Ambapo Kesi ya kupinga ubunge wake ilifunguliwa na makada wa tatu wa CCM ambapo awali waliweza kumvua ubunge Lema Kwa Kushinda Kesi hiyo iliyotolewa Hukumu katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha. Baadae Lema alikata Rufaa kupitia kwa wakili wake Tundu Lisu huku wakiokatiwa rufaa wakiwa na wakili wao Alute ambaye ni kaka yake Tundu Lisu.

Rufaa hii imechukua sura mpya baada ya Wakili wa Upande wa Utetezi Ambaye ni Mh Tundu Lisu akiwa ni mdogo wa damu kwa Wakili wa Waliokatiwa Rufaa Mh Alute, Hapa Ndipo palipovuta hisia za watu wengi ukizingatiwa ilikua kama Mechi kati ya CCM na Chadema huku Kaka na Mdogo Wake Wakipambana Vikali....

Huku Dk Slaa naye akimpatia PONGEZI ZAKE akiwa ameandika katika page yake ya Facebook


Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger