Home » » Yondani:Simba mnapoteza muda

Yondani:Simba mnapoteza muda

Written By Koka Albert on Tuesday, July 10, 2012 | 5:59 AM

Kalunde Jamal
KELVIN Yondan amesema usajili wake Yanga hauna dosari yoyote, na kwamba jitihada za Simba kumwekea vikwazo hazitafanikiwa.

Uhamisho wa Yondani toka Simba kwenda klabu hiyo ya Jangwani, bado una utata kutokana na jina lake kuwa halali kwa klabu zote mbili

Simba ilitangaza kumwekea pingamizi Yondan ili asicheze michuano ya Kombe la Kagame kwa madai ni mchezaji wao halali.

"Uamuzi wangu kusajili Yanga ni sahihi kabisa, hakuna shida hata kidogo nawashangaa Simba kuendelea kuning'ang'ania," alisema Yondani.

"Nilikuwa mikononi mwao hata baada ya mkataba wangu kumalizika na hawakuniambia lolote, sasa nimesajili Yanga wanaanza kuleta chokochoko."
Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger