Kalunde Jamal
KELVIN Yondan amesema usajili wake Yanga hauna dosari yoyote, na kwamba jitihada za Simba kumwekea vikwazo hazitafanikiwa.
KELVIN Yondan amesema usajili wake Yanga hauna dosari yoyote, na kwamba jitihada za Simba kumwekea vikwazo hazitafanikiwa.
Uhamisho wa Yondani toka Simba kwenda klabu hiyo ya Jangwani, bado una utata kutokana na jina lake kuwa halali kwa klabu zote mbili
Simba ilitangaza kumwekea pingamizi Yondan ili asicheze michuano ya Kombe la Kagame kwa madai ni mchezaji wao halali.
"Uamuzi wangu kusajili Yanga ni sahihi kabisa, hakuna shida hata kidogo nawashangaa Simba kuendelea kuning'ang'ania," alisema Yondani.
"Nilikuwa mikononi mwao hata baada ya mkataba wangu kumalizika na hawakuniambia lolote, sasa nimesajili Yanga wanaanza kuleta chokochoko."
Post a Comment