Home » » Ukosefu wa nishati vijijini ni janga la taifa

Ukosefu wa nishati vijijini ni janga la taifa

Written By Koka Albert on Tuesday, July 10, 2012 | 6:05 AM

Elias Msuya
NI miaka 50 sasa tangu Tanzania ilipojipatia uhuru wake huku ikiendelea kuogelea kwenye lindi la umaskini. Siyo kwa sababu ya kukosa rasilimali, bali kutokana na sababu mtambuka.
Moja kati ya mambo yanayodhihirisha umaskini huo ni ukosefu wa nishati ya uhakika katika maisha ya kila siku na kwa maendeleo ya taifa.
Ni kweli tuna umeme wa Gridi ya Taifa, lakini hadi sasa umeme unatumiwa na asilimia 14 pekee ya Watanzania. Maana yake, hadi sasa asilimia 86 ya Watanzania hawana umeme huo, badala yake ama wanatumia umeme unaozalishwa kwa jenereta, jua au njia nyingine zisizo za uhakika.
Asilimia 14 ya hao wanaotumia  umeme ni wanaoishi mijini huku pia kukiwa na viwanda vichache vinavyozalisha bidhaa kwa masoko ya ndani na nje.
Watanzania wengine asilimia 80 ya wanaoishi vijijini hubaki wakitumia misitu kama chanzo kikuu cha nishati kwa kukata miti ili kupata kuni na kuchoma mkaa.
Kwa jumla, asilimia 90 ya nishati inayotumika nchini inatokana na mimea yaani matumizi ya mkaa na kuni huku asilimia nane pekee ya nishati inayotumika nchini hutokana na mafuta na kiasi kilichobaki hutegemea maji.
Matumizi ya kuni na mkaa huchangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira. 
Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa Tanzania ina ekari 33 milioni za misitu, ambazo ni sawa na asilimia 39 ya ardhi yake yote.
Lakini kutokana na uharibifu wa misitu hiyo, inakadiriwa kuwa kila mwaka Tanzania hupoteza hekta 500,000 za misitu ambapo hekta 300,000 sawa na kilometa za mraba 3,320 za misitu hupotea kwa kuchoma mkaa kila mwaka.
Katika matumizi ya mkaa, tafiti zinaonyesha kuwa Jiji la Dar es Salaam pekee hutumia magunia 35,000 ya kuni kwa siku, huku taarifa nyingine zikionyesha magunia kati ya 15,000 hadi 20,000 ya mkaa huingia Dar es Salaam kila siku.
Mikoa mingine inayotajwa kwa matumizi makubwa ya mkaa ni pamoja na Mwanza, Shinyanga, Tabora, Morogoro na Mbeya.
Benki ya Dunia inakadiria kuwa, kila mwaka Tanzania hutumia tani milioni moja za mkaa, huku Jiji la Dar es Salaam likitumia nusu ya mkaa huo kwa mwaka.
Kwa hali hiyo, wataalamu wanasema kuwa Tanzania itakuwa imemaliza misitu yote miaka 10 ijayo ikiwa juhudi za makusudi hazitachukuliwa kunusuru misitu. Hili ni janga linaloinyemelea Tanzania.
Pamoja na tishio hilo, bado Serikali haionekani kuchukua hatua madhubuti  ili kupambana nalo.
Serikali imejikita zaidi kwenye miradi ya umeme wa maji, gesi ili kutafuta suluhisho la nishati nchini
Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger