Home » » TP MAZEMBE YAFANYA MAUAJI, SAMATTA ANG'ARA, ATUMBUKIZA LA USHINDI

TP MAZEMBE YAFANYA MAUAJI, SAMATTA ANG'ARA, ATUMBUKIZA LA USHINDI

Written By Koka Albert on Monday, August 20, 2012 | 12:18 AM

Samatta
TOUT Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imejiweka sawa kwenye mbio za kuwania ubingwa wa Afrika, baada ya kuifunga  Zamalek ya Misri nyumbani kwao, Cairo mabao 2-1.
Shukrani kwake, mshambuliaji chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ‘Sama Goal’ aliyefunga bao la ushindi katika mchezo uliomalizika dakika chache zilizopita kwenye Uwanja wa chuo cha Jeshi, Al-Qahirah mjini Cairo, dakika ya 44, akiunganisha pasi ya Tressor Mputu Mabi.
Katika mchezo huo wa Kundi B, Himoonde alitangulia kuifungia Mazembe inayofundishwa na Lamine N'Diaye dakika ya 34 pasi ya Mputu, lakini Omotoyossi akaisawazishia Zamalek inayofundishwa na kocha Jorvan Vieira dakika ya 36, pasi ya Mohamed Ibrahim.
Ushindi huo wa kwanza ugenini kwa Mazembe katika hatua ya makundi, unaifanya Mazembe ifikishe pointi saba, baada ya kucheza mechi nne, kushinda mbili, sare moja na Berekum Chelsea na kufungwa moja na Al Ahly ugenini.
Al Ahly iliyotoa sare ya 1-1 na Berekum Chelsea nchini Ghana leo, bado inaongoza kundi hilo kwa pointi zake 10, wakati wababe wapya wa Ghana wanashika nafasi ya tatu kwa pointi zao tano na Zamalek wanashika mkia wakiwa hawana pointi hata moja.  
Kwa mara ya kwanza, katika mchezo wa leo, mshambuliaji mwingine wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu alikaa benchi, kwani awali amekuwa havai hata jezi.
Ulimwengu tangu asajiliwe Mazembe msimu uliopita, hii ni mechi yake ya kwanza anakaa benchi kwenye michunao ya Afrika, hizi zikiwa ni dalili njema kwamba anakaribia kuanza kucheza.
Katika mchezo huo, kikosi cha Zamalek kilikuwa; Abdel Wahed El Sayed, Mahmoud Fathalla, A. Mendomo, Sabri Rahil, Hazem Emam/ Said Kotta dk 77, Hani Saied, Ahmed Samir, Ibrahim Salah/ Mohamed Ibrahim Islam Awad/dk63, R. Omotoyossi/ Ahmed Gaafar dk71.
Mazembe; M. Kidiaba, H. Himoonde, F. Kasonde/ M. Ndonga dk 46
, J. Kasusula, S. Sunzu, J. Kimwaki, R. Kalaba, P. Ochan/ N. Kasongo dk 63, M. Mputu, G. Singuluma, M. Samata/ D. Kanda Dk 86.


Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger