BBC-Swahili

Sample Text

Habari

Labels

Labels

Social Icons

About Me

My photo
I would like to welcome all the interested people to join the blog and together we help each other to reach our goals.

Featured Posts

Designed by Edservant. Powered by Blogger.

Sample Text

Latest Post

Usajili Yanga watua TFF

Written By Koka Albert on Friday, August 17, 2012 | 6:56 AM

KLABU ya Yanga jana imewasilisha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), majina ya wachezaji 28 iliowasajili kwa ajili ya msimu ujao, yakiwamo pia majina ya Kelvin Yondani na Mbuyu Twite, ambao Simba wanadai wana mikataba nao.
Klabu ya Simba nayo inatarajia kupeleka usajili wake, yakiwemo majina ya Yondani na Twite, beki wa kimataifa aliyekuwa akicheza timu ya APR ya Rwanda kabla ya vigogo kila mmoja kudai ni mali yake.

Katika usajili wa Yanga uliowasilishwa jana TFF mbali na jina la Yondani na Twite, pia kuna makipa Yaw Berko, Ally Mustapha na Said Mohamed.

Walinzi wa Pembeni ni Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Juma Abdul, Oscar Joshua, David Luhende na Stephano Mwasika.
Walinzi wa kati ni Nadir Haroub, Ibrahim Job na Ladislaus Mbogo.

Viungo wa ulinzi ni  Athuman Idd,  Juma Seif Kijiko na Salum Telela, wakati wa pembeni ni Nizar Khalfan, Shamte Ally, Idrisa Rashid na Omega Seme.

Kwa upande wa viungo washambuliaji, Haruna Niyonzima, Rashid Gumbo na Nurdin Bakari, huku washambuliaji wakiwa Said Bahanunzi, Hamis Kiiza, Didier Kavumbagu na Jeryson Tegete

 Mbali na kikosi hicho pia Yanga imewasilisha majina 22 ya timu ya vijana U20 ambayo wapo pia wachezaji wa timu ya taifa Saimon Msuva na Frank Domayo ambayo majina yao yamepelekwa kwa timu ya vijana lakini wataitumikia timu hiyo kwa kucheza mechi za wakubwa.

Wengine, Geofrey Nyalusi, Yusuf Abdul, Said Manduta, Zuberi Juma, Said Mashaka, Benson Michael, Issa Ngao, Rashid Said.

Majina mengine kwenye orodha hiyo ni Frank Domayo, Omary Nasry, Clever Charles, Mwinyi Bakari, Mpenda Abdallah, Abdulahman Ally, Hussein Moshi, Abdallah Salum na  Rehani Kibingu.

Wengine ni Saimon Msuva, George Banda, Notikely Masasi, Suleiman Ussi na Kassim Jongo.

Hii Kweli Kali,,,,

Written By Koka Albert on Thursday, August 16, 2012 | 6:14 AM


Muamba 'devastated' after being told his career is over five months after heart attack

Written By Koka Albert on Wednesday, August 15, 2012 | 6:28 AM

Bolton midfielder Fabrice Muamba has spoken of his devastation at being forced to retire from football due to the heart attack he suffered in March.
The npower Championship club have announced that the 24-year-old - who had hoped to make a comeback - had made the decision to retire from the professional game after taking medical advice.
'While the news is devastating, I have much to be thankful for,' said Muamba.
Miracle recovery: Bolton's Fabrice Muamba suffered a heart attack in March
Miracle recovery: Bolton's Fabrice Muamba suffered a heart attack in March
Back at Bolton: Muamba (centre) at a club 'family fun day' last Sunday
Back at Bolton: Muamba (centre) at a club 'family fun day' last Sunday
Torchbearer: Muamba carried the Olympic Flame through Waltham Forest
Torchbearer: Muamba carried the Olympic Flame through Waltham Forest
'I thank God that I am alive and I pay tribute once again to the members of the medical team who never gave up on me.'
The Bolton midfielder 'died' for 78 minutes on the pitch at White Hart Lane after suffering a cardiac arrest during an FA Cup match.
Muamba collapsed while playing for Bolton against Tottenham at White Hart Lane in an FA Cup match on March 17.
He received lengthy attention on the pitch and it later emerged that his heart had stopped for 78 minutes.
Fateful day: Muamba suffered a cardiac arrest on the pitch at White Hart Lane in March
Fateful day: Muamba suffered a cardiac arrest on the pitch at White Hart Lane in March
Helpless: Bolton and Spurs players, and Wanderers boss Owen Coyle (centre), watched the terrifying scenes unfold
Helpless: Bolton and Spurs players, and Wanderers boss Owen Coyle (centre), watched the terrifying scenes unfold
Remarkably he made a stunning recovery and left hospital a month later.
Muamba told Bolton's official website: 'Since suffering my heart attack and being discharged from hospital, I have remained utterly positive in the belief I could one day resume my playing career and play for Bolton Wanderers once again.
'As part of my on-going recovery, last week I travelled to Belgium to seek further medical advice from a leading cardiologist.
'But the news I received was obviously not what I had hoped it would be and it means I am now announcing my retirement from professional football.
Tributes: Hundreds of get-well messages were left for Muamba at Bolton's Reebok Stadium while he was in hospital
Tributes: Hundreds of get-well messages were left for Muamba at Bolton's Reebok Stadium while he was in hospital
Rallying round: The football world united to send Muamba a get-well-soon message to the stricken Muamba
Rallying round: The football world united to send Muamba a get-well-soon message to the stricken Muamba
'Football has been my life since I was a teenage boy and it has given me so many opportunities.
'Above all else, I love the game and count myself very lucky to have been able to play at the highest level.
'I would also like to thank everyone who has supported me throughout my career, and the Bolton fans who have been incredible.
'I am blessed to have the support of my family and friends at this time.'
Thank you: Muamba with cardiologist Dr Andrew Deaner (left) and consultant cardiologist Dr Sam Mohiddin, the doctors who saved his life following his heart attack
Thank you: Muamba with cardiologist Dr Andrew Deaner (left) and consultant cardiologist Dr Sam Mohiddin, the doctors who saved his life following his heart attack
Bolton chairman Phil Gartside said: 'To have Fabrice here and with us is truly amazing and we are all very thankful for that.
'We are all hugely disappointed that Fabrice will be unable to return to his playing career but we have to be guided by the medical recommendations and the best interests of Fabrice.
'The most important thing is that Fabrice and his family have the rest of their lives ahead of them.'
Bolton boss Owen Coyle said: 'We have spoken with Fab and he knows we will always support him in whatever he wants to do and that we will always be here for him.
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Not a dry eye in the house: Muamba made an emotional return to the Reebok Stadium in May
Miracle man: Muamba with his fiancee Shauna after his stunning recovery
Miracle man: Muamba with his fiancee Shauna after his stunning recovery
'He is obviously massively disappointed that he won't be able to carry on his career, but everyone has seen what a fighter and strong person he is in mind and body.
'We know that he will go on to achieve great things and within all this disappointment, the most important thing is that he is here, alive, today.'
Muamba and his family fled war in the Democratic Republic of Congo, seeking asylum in the UK.
Despite arriving in London age 11, unable to speak English, he went on to achieve 10 GCSEs and three A levels and joined Arsenal's youth academy in 2002. He later joined Birmingham, before moving to Bolton in 2008.
All smiles: Muamba received an Honorary Degree from Bolton University
    All smiles: Muamba received an Honorary Degree from Bolton University

Dk Ulimboka: Niko tayari kwa lolote

Written By Koka Albert on Monday, August 13, 2012 | 2:07 AM


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Stephen Ulimboka baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam jana akitokea Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa.Picha na Fidelis Felix
ALAKIWA DAR KWA KISHINDO, ASEMA NIKO FITI TAYARI KWA KAZI
Raymond Kaminyoge na Geofrey Nyang’oro
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Stephen Ulimboka amerejea nchini jana akitokea Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa na kulakiwa na mamia ya watu huku akisema haogopi lolote na yupo tayari kwa kazi.

Dk Ulimboka aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere saa 8.15 mchana kwa ndege ya Shirika la South African Airways.
Baada ya kumaliza taratibu zote uwanjani na kutoka nje, Dk Ulimboka alilakiwa na umati mkubwa wa wananchi wakiwemo madaktari na wanaharakati ambao walijaza karibu eneo kubwa la lango la abiria wanaowasili jambo lililoonekana dhahiri kumsisimua kiasi hadi kufikia kububujikwa wa machozi.

Dk Ulimboka ambaye alipelekwa Afrika Kusini akiwa hawezi kutembea wala kula mwenyewe baada ya Juni 27 mwaka huu kutekwa na watu wasiojulikana, kupigwa na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili, kisha kutupwa katika Msitu wa Pande, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, amerejea akiwa anatembea na mwenye afya njema.

Akizungumza uwanjani hapo, Dk Ulimboka alisema: “Nawashukuru Watanzania kwa kuniombea, nawashukuru madaktari wenzangu, ndugu na jamaa zangu kwa kunisaidia kupata matibabu hadi leo hii narudi nyumbani nikitembea mwenyewe. Hivi sasa niko fiti na niko tayari kwa kazi yoyote.”
Uwanja huo ulikuwa umefurika mamia ya wananchi wakiwemo madaktari ambao walikuwa na shauku ya kumwona Dk Ulimboka, lakini wengi hawakufanikiwa kumwona.

Wingi wa watu ulisababisha kutokea kwa msuguano kati ya madaktari na waandishi wa habari. Wakati wanahabari wakitaka kumwuliza maswali Dk Ulimboka, baadhi ya madaktari walikuwa wakimzuia Dk Ulimboka kujibu maswali licha ya mwenyewe kuonekana kuwa tayari kuulizwa.
Baadhi yao walifikia hatua ya kushika kamera za waandishi huku wengine wakisema... “Mwacheni akapumzike bwana, kwa nini mnamsumbua sumbua.”

Baadhi ya madaktari hao walifikia hatua ya kutumia nguvu dhidi ya wapiga picha wa magazeti na televisheni na hivyo kusababisha vurugu na kelele nyingi katika eneo hilo.

Muda wote wakati Dk Ulimboka akielekea kwenye gari akiwa na maua mkononi aliyokadhibiwa baada ya kuwasili uwanjani hapo, madaktari hao walikuwa wakiimba nyimbo za kuhamasishana ukiwamo Wimbo wa Taifa huku wengine wakisema: “Mtakufa nyie, lakini si Dk Ulimboka.”
Baada ya kupanda gari aina ya Nissan Patrol nyeusi, madaktari hao na wanaharakati na wananchi wengine wakiongozwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Ananileya Nkya walilisukuma gari hilo hadi katika lango la kutokea katika uwanja huo.

Wanaharakati
Mbali na Nkya, kulikuwa na idadi kubwa ya wanaharakati wengine wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP, Usu Malya.
Wanaharakati hao walikuwa na mabango yaliyoandikwa,  “Dk Ulimboka karibu nyumbani uliumizwa kikatili ukitetea afya bora kwa Watanzania.”
Bango jingine lilisomeka: “Dk Ulimboka damu yako ilimwagika na kuamsha ari kwa wananchi kudai za afya.”

Jingine, “Dk Ulimboka wewe ni mpigania haki ya afya bora kwa wananchi wote Mungu na Watanzania wote tuko nawe.”
Malya akizungumza uwanjani hapo alisema kupona kwa Dk Ulimboka na kurejea nchini ni uthibitisho kwamba Mungu amesikia sauti za wanyonge.

“Dk Ulimboka alisimamia haki za madaktari na za Watanzania wote akitaka huduma bora zipatikane kwenye hospitali za umma kwa ajili ya Watanzania wote,” alisema.
Mkurugenzi wa Tamwa, Nkya alisema amefurahi kumpokea Dk Ulimboka akiwa hai kwa sababu hali yake ilikuwa mbaya wakati akipelekwa kwa matibabu nje ya nchi.

Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Edwin Chitage alisema kurejea kwa Dk Ulimboka akiwa amepona kunathibitisha kwamba nchi za wenzetu kuna vifaa vya tiba za kisasa na dawa.

“Kurejea kwa Dk Ulimboka ni mapenzi ya Mungu, huu ni uthibitisho kuwa hapa nchini hakuna vifaa tiba na dawa zinazoweza kusaidia wananchi kama ilivyo kwa wenzetu,” alisema Dk Chitage na kuongeza:

“Madaktari tumefarijika na hii imetupa nguvu licha ya vitisho tunavyopata tutaendelea kupigania haki zetu, haya ni mapambano ya muda mrefu, ”alisema.

Dk Chitage alisema kupona na kurejea nchini kwa Dk Ulimboka ni uthibitisho kuwa watu wengi wasio na uwezo wanapoteza maisha kutokana na kukosekana kwa vifaa tiba na dawa hapa nchini... “Madaktari tupo, lakini tatizo ni vifaa na dawa, hiki ndicho tunachopigania ni haki wananchi kupata huduma za afya nchini.”

Katibu Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk Rodrick Kabangila alisema kurejea kwa Dk Ulimboka kutasaidia kuwatambua watu waliohusika katika tukio la kumteka, kumpiga na kumtupa katika Msitu wa Pande.

“Sisi tumefurahi sana, Dk Ulimboka alisimamia haki za madaktari na sekta ya afya kwa ujumla, kurudi kwake kunatupa nguvu ya kuendelea kudai haki za madaktari na wananchi,” alisema.
Dk Ulimboka anarejea nchini huku Serikali na madaktari wakiwa hawajafikia mwafaka kuhusu madai yao.

Madai ya madaktari hao ni hali bora ya mazingira ya utoaji afya nchini, ongezeko la mishahara, posho za kufanya kazi katika mazingira magumu, posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi na posho za kuitwa kazini.

Safari ya Dk Ulimboka kwenda kwenye matibabu nchini Afrika Kusini ilitawaliwa na usiri mkubwa alipoondoka nchini Juni 31 mwaka huu, akisindikizwa na Dk Pascal Lugajo na kaka yake, Dk Hobakile Ulimboka na mke wake,  Dk Judith Mzovela.

Kutekwa
Dk Ulimboka alitekwa na kufanyiwa vitendi vya ukatili wakati akiratibu mgomo wa madaktari uliokuwa ukiendelea na aliokotwa na msamaria mwema akiwa amefungwa mikono na miguu akiwa katika hali mbaya.

Kutokana na tukio hilo, wanaharakati wa haki za binadamu waliituhumu Serikali kuhusika na tukio hilo, huku Serikali ikikana na kuliagiza Jeshi la Polisi kuwasaka waliohusika.
Akisimulia mkasa huo Dk Ulimboka alisema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Juni 27 katika Klabu ya Leaders, Dar es Salaam alikokuwa na daktari mwenzake na mtu mwingine aliyekuwa amemwita hapo (Leaders).

“Mara, katikati ya maongezi tukaona huyo mtu aliyeniita anaongea na simu. Ghafla tukiwa tunasema tuagane, wakaja watu kama watano hivi na bunduki, wakasema wewe na yule bwana mko free (huru), tunakuchukua wewe (Dk. Ulimboka). Sijakaa sawa, nikaona nimeshaburutwa nikaanguka kwenye lami, wakaniinua na kuniingiza kwenye gari nyeusi, lakini ilikuwa haina namba.”
Wakati Dk Ulimboka alipokuwa akiendelea na matibabu Afrika Kusini, Rais Jakaya Kikwete alisema Serikali haihusiki na kilichomtokea daktari huyo kwa kuwa alikuwa kiungo muhimu katika majadiliano baina ya Serikali na madaktari.

Rais Kikwete alisema hayo katika hotuba yake ya mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
“Dk Ulimboka alikuwa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na madaktari. Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam madaktari wanamwamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali,” alisema Rais Kikwete.
Alisema alichofanyiwa Dk Ulimboka kimemsikitisha na kumhuzunisha kwa kuwa ni kitendo cha kinyama na kinyume kabisa na mila na desturi za Tanzania.
Kauli ya Rais Kikwete kuhusu mgomo wa madaktari inafanana na ile iliyokuwa imetolewa awali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisema wanatambua kuwa Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka kuhusu kilichomtokea Dk Ulimboka, lakini ameshangazwa na hisia hizo akisema haoni sababu ya Serikali kufanya hivyo.

Dk Ulimboka alisafirishwa kwenda Afrika Kusini Juni 31, mwaka huu kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi baada ya jopo la madaktari waliokuwa wakimhudumia, kueleza mabadiliko ya hali ya afya yake, yaliyosababisha figo kushindwa kufanya kazi.

Ulinzi nyumbani
Nyumbani kwao, eneo la Ubungo Kibangu kulikuwa na watu kadhaa waliokuwa nje ya nyumba huku ulinzi ukiwa umeimarishwa.
Vijana wasiopungua watatu wakiwa wamevaa kawaida walikuwa wamekaa jirani na lango la kuingilia wakiratibu nyendo za wanaopita na wanaotaka kuingia katika nyumba hiyo iliyopo karibu na Shule ya Msingi Ubungo Kibangu.
“Watu walikuwa wengi hapa lakini wametakiwa kuondoka ili kutoa nafasi kwa dokta kupumzika na hakuna ambaye anaruhusiwa kuingia kwa sasa labda kama ni daktari mwenzao,” alisema kijana mmoja anayeishi jirani.

Awali, mama mmoja ambaye alifahamika kama ndugu wa familia hiyo anayeishi karibu na nyumba ya Dk Ulimboka alipoulizwa nyumbani kwa kiongozi huyo wa madaktari alihoji anatafutwa na nani na hata mwandishi walipojitambulisha alimtaka aondoke na kurejea alikotoka.
“Baba wewe nenda nyumbani kwako tu, usitake kujua zaidi,” alisema mama huyo majibu ambayo yalionekana kufanana na ya majirani wengi wa daktari huyo.
Nyongeza na Joseph Zablon

Malawi kutopigana na Tanzania

Written By Koka Albert on Friday, August 10, 2012 | 11:33 PM

MALAWI imesema imeondoa ndege zake zilizokuwa zikifanya utafiti wa mafuta katika Ziwa Nyasa kwa kuwa haitaki kuingia vitani, badala yake imeamua kupeleka mgogoro huo Mahakama ya Kimataifa.

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Mambo ya Ndani na Uhusiano wa Kimataifa kwa Mambo ya Kiusalama wa Malawi, Uladi Mussa alipokuwa akizungumza na gazeti linalochapishwa nchini humo la Nyasa Times.

“Nawahakikishia wananchi mtaendelea kuishi kwa utulivu. Tupo kwenye mazungumzo na Serikali ya Tanzania, bila shaka mambo yataenda vizuri. Kama hali ikishindikana tutalipeleka suala hili kwenye Mahakama ya Haki ya Kimataifa,” alisema Mussa.

Kauli ya Waziri huyo imekuja wakati baadhi ya wananchi wa Malawi wanaoishi katika Vijiji vya Karonga na Chitipa vilivyopo kando ya Ziwa Nyasa upande wa Malawi wakiwa wameanza kuvihama vijiji hivyo kuhofia usalama wa maisha yao.

Baadhi ya wakazi hao wamekaririwa na Nyasa Times wakisema kuwa wameamua kuchukua hatua hiyo kunusuru maisha kutokana na kuwapo kwa dalili za kutokea vita kati ya Malawi na Tanzania.
Waziri Mussa amesema suala hilo la mgogoro wa mpaka litaamuliwa kwa njia ya amani na hivyo kuwataka wananchi kuendelea na shughuli zao bila wasiwasi.

Waziri huyo aliwahakikishia wananchi hao kuwa Serikali ya Malawi ina ushahidi wa kutosha kuwa ziwa lote la Malawi (Nyasa)ni mali ya Malawi na Tanzania haina nguvu ya kuwasimamisha kuendelea na kazi ya kutafuta mafuta.

“Kimsingi hapa hakuna hoja ya kubishania. Wote tunajua ziwa hili ni mali yetu (Malawi),” alisema.
“Kama malalamiko haya yangekuwa yametolewa na Msumbiji, hapa tungekuwa na hoja ya kubishania, lakini si Tanzania.” alisisitiza.

Alisema ushahidi wao wa mipaka ni wa tangu mwaka 1890 wakati ambako wakoloni wa Uingereza na Ujerumani walitiliana saini juu ya suala hilo.

Aliendelea kueleza kuwa umiliki huo wa ziwa  umeongezewa nguvu na maazimio ya mwaka 1963 ya Wakuu wa uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (OAU) kwamba wanachama wanapaswa kuheshimu mipaka waliyorithi kwa wakoloni.

Kauli za wananchi
Wakati Serikali ya Malawi ikitoa msimamo huo watu kadhaa waliohojiwa wameonyesha hofu ya nchi hizo kuingia katika vita.

Heckley Christopher ambaye ni raia wa Malawi anayefanya biashara eneo la Mbambabay mkoani Ruvuma anasema: " Malawi ni nchi ndogo sana kupigana na Tanzania, ni nchi yenye mikoa minne tu, kukiwa na vita itaangamia mara moja."

Raia mwingine wa Malawi ni Vilion Gordon ambaye alisema Tanzania na Malawi ni marafiki wa siku nyingi, hivyo hawana sababu za kugombania ziwa ambalo lilikuwapo tangu enzi hizo.

"Nashauri wakae chini wapatane, kwa nini tugombane sasa wakati ziwa hilo lilikuwapo tangu enzi hizo?"alisema.

Mtanzania mkazi wa Kijiji Lundo kilichoko Mbambabay mkoani Ruvuma, Zakhia Chengula ameitaka Serikali ya Tanzania kuendelea kuimarisha ulinzi na kukubali kuingia katika mazungumzo na Malawi badala ya kufikiri vita.

"Hapa sisi ni kwetu, vita ikiingia sisi tutakufa tu hakuna pa kukimbilia. Tunaiomba Serikali iimarishe ulinzi eneo hilo na ikae na Malawi kuzungumzia mgogoro huo," alisema.

Mkuu wa Wilaya mpya ya Nyasa, Ernest Kahindi alisema hakuna hofu yoyote kwa wakazi wanaoishi kando ya Ziwa Nyasa upande wa Tanzania.
Amewataka wananchi hao kuendelea na shughuli zao za uzalishaji mali kama kawaida kwani suala hilo sasa linashughukiliwa kitaifa.

"Mwanzoni kulikuwa na hofu kubwa, lakini baada ya Serikali ya Tanzania kutoa tamko la kutaka ndege za Malawi ziondoke na zenyewe kutii amri hiyo, hakuna tatizo lolote," alisema na kuendelea;
"Shughuli katika eneo hili zinaendelea kama kawaida. hakuna mwananchi aliyepigwa risasi wala ndege iliyotunguliwa, mambo yako shwari."
Jeshi laimarisha ulinzi

Katika hatua nyingine Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limeimarisha ulinzi katika mwambao wa Ziwa Nyasa na kupiga marufuku wananchi kukatisha eneo lao la jeshi.

Super Sport kumjaribu Bocco

Written By Koka Albert on Thursday, August 9, 2012 | 5:25 AM

MSHAMBULIAJI wa Azam FC, John Bocco ataondoka wiki ijayo kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa na klabu ya Super Sport ya nchini Afrika Kusini.

"Nimepata taarifa kwamba natakiwa kwenda kufanya majaribio Afrika Kusini, lakini ukweli ni kwamba viongozi wangu bado hawajaniambia," alisema Bocco.

“Nasubiri kuelezwa taarifa za safari hiyo kama kweli ipo kama ambavyo nimekuwa nikisikia kwa watu mbalimbali na vyombo vya habari," alisema Bocco.

Habari kutoka chnazo cha kuaminika ndani ya klabu ya Azam, kimethibitisa taarifa za Bocco kuitwa Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya majaribio.

Bocco, mfungaji wa mabao matatu katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Simba, robo fainali ya Kombe la Kgame zaidi ya wiki mbili zilizopita, alionyesha kiwango cha juu kwenye michuano hiyo.

“Anakwenda kufanya majaribio, hizi ni taarifa za kweli kabisa," alisema mpashaji huyo wa habari.
Aliongeza: "Ni vigumu kuamini nayokueleza, lakini fahamu kwamba (Bocco) ana safari ya kwenda kucheza kwa majaribio nchini Afrika Kusini."

Wakati wa michuano ya Kombe la Kagame, Bocco alifunga mabao matato, na kukamatana nafasi ya tatu ya ufungaji bora.Msimu uliiopita wa Ligi Kuu Bara, Bocco aliibuka kuwa mfungaji bora baada ya kukwamisha wavuni mpira mara 18 na kuwapiku washashambuliaji, Emmanuel Okwi, Kenneth Asamoah na Davies Mwape.

Ndege za Malawi zafungasha virago Ziwa Nyasa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe
SIKU chache baada ya Serikali kuzitaka ndege zinazozunguka Ziwa Nyasa upande wa Tanzania kufanya utafiti wa mafuta kuondoka mara moja, Serikali ya Malawi imetii na kuziondoa kampuni zinazofanya kazi hiyo katika ziwa hilo.

Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yake Jumatatu iliyopita, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe aliitaka Malawi kuziondoa ndege na kampuni zinazofanya utafiti wa mafuta katika eneo hilo kwa kuwa ni mali ya Tanzania.

Mbali na Waziri Membe, viongozi wengine waliozungumzia mgogoro huo na kuitaka Malawi iache uchokozi ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Edward Lowassa.

Wakati Sitta akiwataka Watanzania kuendelea na shughuli zao bila hofu kwa kuwa Serikali iko tayari kwa tishio lolote, Lowassa alisisitiza kuwa Tanzania imejiandaa kiakili na kivifaa kuingia vitani na Malawi kama italazimika kufanya hivyo.

Jana kwa nyakati tofauti, Wakuu wa Wilaya nne zilizo mpakani mwa Tanzania na Malawi za Ileje, Mbozi, Mbeya, Kyela na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro walieleza kuwa mara baada ya kauli hizo, ndege hizo za Malawi ziliondoka na kampuni zilizokuwa zikitafiti mafuta katika Ziwa Nyasa zimeacha.
“Hapa tuko cool (tulivu) kabisa tangu zile ndege zilipoacha kuruka, tofauti na hizo kauli zinazotolewa na viongozi wa Serikali (ya Malawi),” alisema Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Dk Michael Kadeghe na kuongeza:

“Hapa niko kwenye Sherehe za Nanenane na Malawi wana banda lao nimetoka kulitembelea. Hali iko shwari, tunaendelea na uhusiano kama kawaida.”
KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger