Home » » HIVI, UNATAMBUA MATUKIO YANAYOONGOZA KUVUNJA MOYO WAKO IKIWA UTARUHUSU UENDELEE KUYAFANYA?

HIVI, UNATAMBUA MATUKIO YANAYOONGOZA KUVUNJA MOYO WAKO IKIWA UTARUHUSU UENDELEE KUYAFANYA?

Written By Koka Albert on Wednesday, October 17, 2012 | 10:53 PM


Kuna siku niliwahi kukaa 
na kujiuliza,
 ilikuwaje kati ya
 viungo vyote mwilini,
MOYO 
ndiyo uteuliwe kuwakilisha hisia 
zote za binadamu.

Ukiwa katili, mpole, mkarimu, mwizi, au jasiri bado utatumika 
moyo kubeba hizo sifa.
Si kitu cha ajabu kusikia mtu anapewa sifa ya  kuwa na Moyo 
mgumu, moyo mwepesi au moyo wa tamaa. 
Nilipochunguza kwa kusoma vitabu vya kisayansi
 nikagundua kuwa Moyo ndiyo kiungo cha kwanza kuishi 
na cha mwisho kufa 
kwa binadamu,
ndio maana kimepewa nafasi hiyo.
Kutokana na kiungo hiki kubeba matukio mengi muhimu katika maisha yetu ni vyema tukakitunza.

Hivi ni kweli moyo huvunjika?
Kisayansi haiwezekani,
lakini amini usiamini,
 kihisia ni kweli moyo unavunjika.
Na mtu ambaye inasemekana moyo wake umevunjika,
raha ya maisha kwake haipo.
Kuna matukio yanayoongoza kuvunja mioyo ya binadamu,
Hebu tuyaangalie na tuanze kuyakwepa:

1.KURUHUSU WATU WABATILISHE UNAVYOJISIKIA

Kama kuna kitu unajisikia, 
ni kweli ndivyo kilivyo.
Hakuna kingine watu watakachosema 
chenye uwezo wa 
kubadilisha hilo.
Hakuna anayeishi ndani yako 
zaidi ya wewe mwenyewe.
Hakuna anayeweza kuelezea hisia zako
 zaidi ya wewe mwenyewe,
usiruhusu mtu akuhukumu kwa ulilofanya kwa kuwa hajui ulikuwa katika hali gani.
Usiruhusu watu wakuaminishe tofauti na wewe unavyojisikia.

2.KUJUTIA KILA KOSA

Yaani
 kama mpaka leo bado unaendelea
 kujutia kosa ulilofanya muda mrefu uliopita unajivunja moyo wako.
Kumbuka katika kipindi ulichokosea,
 ulifanya kutokana 
na uelewa na uzoefu uliokuwa nao 
muda ule na sio sasa.
Yawezekana kabisa,
 uchanga wa akili 
ndio ulikufanya ufanye vile 
ulivyofanya, 
na ndio maana kama ungepewa nafasi ya leo kufanya maamuzi
 uliofanya miaka iliyopita 
usingefanya  kama vile hata kidogo.
Muda na uzoefu vinatupa nafasi ya kufanikiwa katika yale tunayoyafanyia maamuzi,
kwa hiyo sahau yaliyopita songa mbele.

3.KUWAPOTEZEA WANAOKUPENDA

Unajua 
kuna kipindi unakuwa na watu
 wanakuonyesha upendo halafu wewe unashindwa kuwaonyesha shukrani.
Hii ni sawa na 
kujiandalia bomu ambalo litakuja 
kukulipukia siku ile watakapoondoka kabisa machoni pako.
Na kuna kipindi,
 utatamani angekuwepo karibu yako umueleze unavyojisikia 
au akikusaidia shughuli fulani.
Unatakiwa umuonyeshe shukrani yule anayekufanyia upendo kila muda utakaopata.

4.KURUHUSU MATAMANIO KUKUTAWALA

Kuna kipindi tunafanya uamuzi mbaya,
 sio kwasababu ni wabaya ila 
ni kwasababu 
tumejali zaidi kuwafurahisha wengine 
kuliko fahari yetu.
Unapokubali 
kufanya uamuzi wa tamaa ya kutaka
 uonekane mtu fulani 
ni 
kujitengenezea uasi wa ndani.

5.KUTAKA KUBISHANA KILA HOJA

Kuwa shujaa sio kupigana kila vita 
inayokuja mbele yako,
 au 
si kujibu kila shutuma dhidi yako.
Kama unaona hilo jambo
 litakushushia heshima na utu wako,
 ni heri ukaachana nayo ili yasiweze kuzaa mengine mapya
 na mabaya zaidi.


6.KUHARAKISHA UHUSIANO

Uhusiano 
mzuri ni wa watu ambao kila mmoja
 amempokea mwenzake kwa hali yake 
aliyonayo, 
na kumsaidia atoke 
hapo alipo kwenda katika hali 
iliyobora zaidi ya aliyomkuta nayo.
Usikimbilie
 kuwa katika uhusiano na mtu kwa kuwa, mazingira au 
nafasi imetokea tu.
Tafuta mwenza ambaye atakuhimiza kukua,
asiyeng'ang'ania ufanye 
anachopenda yeye kila wakati,
atakayekuruhusu uchangamane na watu wengine, na atakayekuamini.

7.KUMNG'ANG'ANIA ANAYETAKA KUONDOKA

Ni uchungu sana,
 kumuaga mtu unayetaka abaki,
lakini ni maumivu zaidi kumng'ang'ania anayetaka kuondoka.
Kama unayemuonyesha upendo na,
 hataki kurudisha upendo kwako
 usikae kulazimisha kwani utaendelea kujiumiza tu na
 kuwa mtumwa kwake.
Mtu pekee unayepaswa kuwa naye ni yule anayekuheshimu na anatambua umuhimu wako katika maisha yake.

8.KUKATAA KILA USHAURI 

Si kila
 ushauri utakao pewa 
utakuwa sahihi sawa,
lakini 
si kila ushauri utakuwa mbaya kwako.
Kubali kupokea
 marekebisho kutoka kwa watu
 wengine.
Usijitengenezee mazingira ya kuja kuuvunja moyo wako siku zijazo kwa kujuta.

RAHA YA MAISHA NI KUISHI KWA AMANI NA FURAHA,
KAMA UTAENDELEA KUJIWEKA 
KATIKA MAZINGIRA YA KUJA 
KUUVUNJA MOYO WAKO,
 HAUTAONA LADHA 
YA MAISHA KAMWE.

ANZA LEO KUUTUNZA MOYO WAKO.
Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger