Mh. SALVATORY MACHEMLI Mbunge wa Ukerewe.
MH. HIGHNESS KIWIA MBUNGE WA ILEMELA
Wabunge wawili mmoja wa Jimbo la Ilemela na mmoja wa jimbo la Ukerewe wamepigwa mapanga na mawe usiku wa leo
kuamkia asubuhi na hii inatokana viongozi hao walikuwa huko Mwanza wakati wakitembea usiku walivamiwa na watu wasiojulikana na walipigwa mapanga na kuumizwa sana huku mbunge wa Ilemela akiwa hoi bin taabani yani ameumizwa sana TAARIFA KUTOKA KWA ZITO
"Tupo Hospitali ya Bugando hapa. Ndg. Kiwia, mb anatoa maelezo kwa maafisa wa polisi.
Kuna mmoja wa majeruhi ambaye yupo hapa mwanzoni alisema yeye ni mtu wetu na ameumizwa pia. Imegundulika ni mtu wa UVCCM, Ahmed Mkilindi ambaye ndiye alikuwa anaongoza kikosi kilichowavamia kina Kiwia. Amepata jeraha mkononi (friendly fire?). Mwenyekiti wa CCM mkoa yupo hapa kaja kumwona. Nimewaambia Polisi mtu huyu asitolewe hospitali kinyemela bali atoe maelezo polisi kwanza. Huyu ni mtuhumiwa wa kwanza kabisa.
Hali ya ndg. Kiwia sio nzuri sana. Anatakiwa kufanyiwa ct scan kuona athari aliyopata (maana kapigwa na shoka na mapanga kichwani). Bahati mbaya hapa Bugando kifaa hicho hakifanyi kazi.
Nimezungumza na Katibu wa Bunge na ndani ya muda mfupi ndg. Kiwia atasafirishwa kupelekwa Muhimbili kwa uangalizi zaidi.
Ndg. Machemuli anaendelea vizuri alitoka hospitali jana (alipata huduma ya Kwanza Sekou Toure).
Siasa za Tanzania zinazidi kujidhihirisha kuwa hazina tofauti na nchi nyingine za Kiafrika. Chama cha siasa kuwa na makundi ya wahuni na kupiga watu ni hatari na chama hicho kinakosa 'moral' authority ya kutawala.
Tusubiri uchunguzi zaidi wa Polisi. I am so depressed" BY ZITO ZUBERI KABWE
Kuna mmoja wa majeruhi ambaye yupo hapa mwanzoni alisema yeye ni mtu wetu na ameumizwa pia. Imegundulika ni mtu wa UVCCM, Ahmed Mkilindi ambaye ndiye alikuwa anaongoza kikosi kilichowavamia kina Kiwia. Amepata jeraha mkononi (friendly fire?). Mwenyekiti wa CCM mkoa yupo hapa kaja kumwona. Nimewaambia Polisi mtu huyu asitolewe hospitali kinyemela bali atoe maelezo polisi kwanza. Huyu ni mtuhumiwa wa kwanza kabisa.
Hali ya ndg. Kiwia sio nzuri sana. Anatakiwa kufanyiwa ct scan kuona athari aliyopata (maana kapigwa na shoka na mapanga kichwani). Bahati mbaya hapa Bugando kifaa hicho hakifanyi kazi.
Nimezungumza na Katibu wa Bunge na ndani ya muda mfupi ndg. Kiwia atasafirishwa kupelekwa Muhimbili kwa uangalizi zaidi.
Ndg. Machemuli anaendelea vizuri alitoka hospitali jana (alipata huduma ya Kwanza Sekou Toure).
Siasa za Tanzania zinazidi kujidhihirisha kuwa hazina tofauti na nchi nyingine za Kiafrika. Chama cha siasa kuwa na makundi ya wahuni na kupiga watu ni hatari na chama hicho kinakosa 'moral' authority ya kutawala.
Tusubiri uchunguzi zaidi wa Polisi. I am so depressed" BY ZITO ZUBERI KABWE
Post a Comment