Home » » Amuunguza wifi yake sehemu za siri

Amuunguza wifi yake sehemu za siri

Written By Koka Albert on Friday, June 8, 2012 | 2:44 AM

KATIKA hali ya kushangaza na kusikitisha,mkazi wa moshi bar Manispaa ya Ilala,amedaiwa kumuunguza  wifi yake( 15) sehemu zake za siri  na kumsababishia maumivu makali.

Hayo yametokea jana Jijini Dar es Salaam, baada ya askari polisi wa kituo cha Stakishari, kupokea taarifa kutoka kwa majirani juu ya unyama huo aliofanyiwa binti huyo.

Polisi hao mara baada ya kupata taarifa hiyo, walifika nyumbani kwa mtuhumiwa lakini iliwachukua zaidi ya saa mbili kufanikiwa  kumtoa ndani mtuhumiwa ambaye alidaiwa kujifungia.

Hata hivyo, hali ilikuwa tete baada ya wakazi na majirani  wa eneo hilo walioguswa na tukio , walipoamua kuvamia nyumba hiyo baada ya kupokea taarifa za uongo kuwa mtuhumiwa hayupo  na kuamua kuwashinikiza polisi wamtoe au wajichukulie sheria mkononi.

Kufuatia mvutano huo, Polisi waliofika kumchukua mtuhumiwa , walizidiwa na kuamua kuondoka  kwa lengo la kwenda kuongeza nguvu kwa kuongeza askari na mabomu ya kurusha ili kuweza kuwatanya wananchi waliokuwa na hasira.

Licha ya kuongeza askari, haikuwa kazi rahisi kuwatawanya mpaka walipoamua kupiga risasi  hewani na kufanikiwa kuwatawanya wakazi hao waliokuwa na hasira sambamba na kumtoa mtuhumiwa aliyekuwa amejificha juu ya dari ya nyumba.

Mtoto aliyefanyiwa unyama huo alisema, Mei 30, alilazimishwa kunywa maji ambayo yamechanganywa na vipande vya glasi huku akiwa anapigwa na waya wa umeme.

Alisema  siku iliyofuata Mei 31, alipigwa na mama huyo na baadaye kuingizwa kipande cha mti  sehemu za haja kubwa ambacho alikaa nacho kwa saa mbili na baadaye mama huyo alimtoa.
“Nilikunywa maji yaliyochanganywa na vipande vya chupa ya bilauli huku nikiwa napigwa ambavyo vinaniletea matatizo ya tumbo ambapo nimepata choo siku moja hadi leo hii sijapata tena ambacho kilikuwa na damu nyingi”alisema

Juni 1, mwaka huu majira ya saa 8 mchana mtoto huyo ndiyo alichomwa moto katika sehemu zake za siri, huku akiwa amefungwa mikono na miguu kwenye dirisha.

Alisema siku hiyo alianza kumpiga kwa saa moja na baadaye alimkamata na kumfunga kamba kwenye miguu na mikono huku akichukua moto na kumuunguza sehemu zake hizo za siri na kumsababishia maumivu makali.

“Nilivuliwa nguo zote na alinifunga kamba huku akichukua moto na kuniweka sehemu zangu zote za  siri ambapo kwa sasa nashindwa kwenda haja kubwa na ndogo.

Jirani Aziza Saidi alisema, Juni 2, mwaka huu walimuona mtoto huyo akielekea dukani huku akiwa amepanua miguu yake ndipo walipomwita na kumuuliza na  aliwajibu kuwa ameunguzwa na moto sehemu zake za mwili.

Alisema walimwita ma kumwangalia sehemu zake na kukuta zimeharibika ndipo walipoamua kutoa taarifa kwa dada yake ili amchukue.

Mtuhumiwa huyo  katika utetezi wake alisema, hawezi kufanya vitendo kwa wifi yake na anajua uchungu wa kuzaa kwa sababu yeye ni mama wa watoto wawili.

Mtoto huyo alipelekwa katika hospitali ya Amana kwa uchunguzi zaidi.
Share this article :

+ comments + 1 comments

Anonymous
June 8, 2012 at 4:03 AM

Jamani huu ni unyama

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger