Home » » Kwema: Shule ya msingi ilivyoweka historia mpya Shinyanga

Kwema: Shule ya msingi ilivyoweka historia mpya Shinyanga

Written By Koka Albert on Tuesday, March 27, 2012 | 2:22 AM

Na Shija Felician
KWA muda mrefu, mkoa wa Shinyanga umekuwa ukishika mkia katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa darasa la saba.

Kwa mfano, takwimu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, zinaonyesha mkoa huo ulishika nafasi ya mwisho katika miaka ya 2008 na 2009.

Hata hivyo, matokeo ya mtihani wa darasa la saba wa mwaka 2011 ulikuja na sura tofauti hasa baada ya mkoa huo kutoa shule kinara wa mtihani huo na hata wanafunzi bora kitaifa.

Shule iliyoupandisha chati mkoa wa Shinyanga inaitwa Kwema ambayo ni shule ya mchepuo wa Kiingereza iliyopo wilayani Kahama.

Kwa mujibu wa taarifa za matokeo ya mtihani huo zilizotolewa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), shule ya Kwema ilitajwa kuwa ya pili kitaifa kati ya shule 15,510, huku pia ikitoa wanafunzi bora wa kwanza, wa tatu na wa nne kitaifa.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa shule hiyo, Pauline Mathayo, siri kubwa ya kufanya vizuri kwa shule yake ni ari kubwa ya kufundisha waliyo nayo walimu anaosema aghlabu humaliza silabasi muda mrefu kabla ya mitihani ya mwisho,jambo linalowapa fursa ya kuwapa mazoezi ya kutosha  wanafunzi.

 “Tuna walimu  waliobobea na wenye nia ya kujituma katika kuelimisha wanafunzi. Pia wazazi wanashirikiana bega kwa bega  na uongozi kuhakikisha wanafunzi wanapata mahitaji yao ya shule kwa wakati,’’anasema

Tofauti na hali Ilivyo katika shule nyingi hata zile kongwe na maarufu anajivunia kuwa na walimu zaidi ya 70 wanaowafundisha wanafunzi 1600 waliopo shuleni hapo.

Anasema ufaulu mzuri wa shule yake ni faraja kwa mkoa wa Shinyanga, huku akisema mkoa huo sasa umeamka kielimu.

Anaeleza kuwa  tangu shule yake ianze  kufanya mtihani wa darasa la saba mwaka  2002, hakuna mwanafunzi aliyefeli, huku  wote  wakichaguliwa kujiunga na shule za sekondari.
Kauli za wanafunzi

Innocent Nyakabunda ndiye aliyeongoza jahazi la ufaulu wan shule yake kwa kushika nafasi ya kwanza kitaifa.Unapozungumza naye kwa haraka utagundua kuwa mtoto huyu anajiamini na ana upeo mkubwa ndani yake.
Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger