Dk. Joyce Ndalichako
KATIBU Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk. Joyce Ndalichako, kwa mara nyingine ametetea uamuzi wa baraza lake kuwafutia matokeo ya mtihani wa kidato cha IV baadhi ya wanafunzi. Nimesikia kwa umakini utetezi alioutoa.
Kimsingi Dk. Ndalichako ameeleza mambo matatu makubwa kuhalalisha kile alichoita, “kukithiri kwa vitendo vya udanganyifu katika vyumba vya mitihani.”
Kwanza, Dk. Ndalichako amesema baraza lake limelazimika kuchukua hatua hiyo ngumu baada ya baadhi ya walimu na wasimamizi wa mitihani kushiriki katika “uchafuzi wa mitihani.”
Pili, amasema baadhi ya wanafunzi walikutwa na majibu ya mitihani kupitia simu zao za mkononi.
Tatu, amesema wasimamizi walikamata vikaratasi ambavyo wanafunzi walikuwa wanavitumia “kupasiana” majibu.
Lakini kabla ya Necta kubebesha tuhuma wasimamizi wa mitihani sharti ieleze kama katika mtihani huu, ilibadilisha mfumo wake wa kuteua wasimamizi waaminifu kama wanavyofanya siku zote.
Hii ni kwa sababu, wengi wa wasimamizi ni wale wale waliowahi kutaka kutunikiwa tuzo kutokana na kulipatia sifa nzuri ya “usimamizi wenye tija,” baraza lake.
Post a Comment