Nahodha wa Simba SC Juma Kaseja akiwaongoza wachezaji na viongozi wa Simba kushangilia baada ya kuichapa SC Kiyovu leo
Mashabiki wa Simba wakishangilia ushindi wa timu yao.
Emmanuel Okwi akiipangua beki ya Kiyovu.
Timu ya soka ya Simba SC leo imeibuka kidedea baada ya kuilaza SC Kiyovu ya Rwanda mabao 2-1 katika mchezo wa marudiano wa raundi ya awali ya Kombe la Shirikisho la klabu za Afrika, uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mabao yote mawili ya Simba yamewekwa kimiani na mshambuliaji Felix Sunzu akipokea pasi safi kutoka kwa Emmanuel Okwi. Kwa ushindi huo, Simba wamesonga mbele katika michuano hiyo.
Post a Comment