Home » » CWT yachochea walimu wakimbie vituo vya

CWT yachochea walimu wakimbie vituo vya

Written By Koka Albert on Saturday, March 3, 2012 | 12:16 AM

CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT), kimewachochea walimu wapya walioajiriwa hivi karibuni, warejee makwao iwapo Serikali itaendelea kuwazungusha kuwalipa fedha za kujikimu pamoja na mishahara.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Rais wa (CWT), Gratian Mukoba alisema wamepokea taarifa za malalamiko kutoka halmashauri mbalimbali nchini kwamba walimu walioajiriwa Februari mwaka huu, hadi sasa hawajapata fedha za kujikimu pamoja na mishahara.

“Sioni sababu ya walimu kuendelea kuteseka na kuwa ombaomba wakati wapo kazini. Kama Serikali imeshindwa kuwalipa fedha zao za kujikimu pamoja na mishahara wanatakiwa kurudi nyumbani kwao hadi itakapopata fedha ndipo iwaite tena kazini,” alisema Mukoba.

Mukoba alisema kama hali itaendelea hivyo hadi mwisho wa mwezi huu, CWT kitalazimika kuchukua hatua za kuhakikisha walimu wote wanarudi nyumbani ili kuwaepusha na hali ya kuwatia majaribuni kutokana na kuishi katika mazingira magumu.

“Napenda kuwaambia walimu ambao wataweza kuvumilia hali hii hadi mwisho wa mwezi huu na kuona hakuna mabadiliko, nao wanatakiwa kurudi kwao hadi pale Serikali itakapopata fedha. Hebu fikiria mwalimu hana sehemu ya kulala, chakula nacho shida; halafu ananyimwa fedha zake. Unategemea nini?” Alihoji Mukoba.

Alisema kitendo cha kuwalipa fedha za kujikimu za siku tatu badala ya malipo ya siku saba ni ukiukwaji wa sheria za kazi na unyanyasaji wa watumishi jambo ambalo CWT haitalivumilia.

Mukoba alisema malalamiko mengine ni ya fedha za madai ya walimu ambayo yalihakikiwa na Serikali kati ya Novemba na Desemba lakini ulipaji umegubikwa na utata.

“Kwa kweli unyanyasaji wa walimu umekithiri sana maana hata walimu waliopo kazini kwa muda mrefu, fedha za madai ya zamani yaliyohakikiwa na Serikali bado ulipaji wake ni utata mtupu. Walimu wanazungushwa na kunyimwa fedha hizo lakini kwa sasa tunafikia hatua ya mwisho ya kuchukua,” alisema Mukoba.

Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger