Home » » Harusi ya Britney Spears yapigwa kalenda

Harusi ya Britney Spears yapigwa kalenda

Written By Koka Albert on Saturday, March 3, 2012 | 12:25 AM

LOUISIANA, MAREKANI
NDOA ya mwanamuziki, Britney Spears na mchumba wake, Jason Trawick, imesogezwa mbele baada ya mawakili wa mwanamuziki huyo kumshauri afanye hivyo.

Mawakili wake wamemshauri aachane na masuala ya ndoa, mpaka pale kesi yake dhidi ya meneja wake wa zamani, Sam Lutfi, itakapofikia tamati.

Mwanamuziki huyo amefunguliwa mashtaka na meneja huyo ambaye anadai kuwa hakuridhika baada ya kufukuzwa kazi.

Mahakama imeamua kuwa mali na biashara zote za Spears, zisimamiwe na baba yake mzazi, Jamie Spears, mpaka kesi itakapomalizika.

Kwa maana hiyo, huenda ndoa hiyo isifungwe mpaka mwishoni mwa mwaka kwa kuwa hukumu ya kesi hiyo inatarajiwa kutolewa Septemba mwaka huu.
Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger