Home » » Jennifer Hudson Kupanda kizimbani

Jennifer Hudson Kupanda kizimbani

Written By Koka Albert on Saturday, March 3, 2012 | 12:30 AM


ILLINOIS, MAREKANI
JENNIFER Hudson atakuwa mmoja kati ya watu watakaotoa ushahidi katika kesi ya mauaji ya mama yake mzazi, kaka yake na mpwa wake waliouawa mwaka 2008.

Jina la mwimbaji huyo limewekwa kwenye orodha ya watu wanaohitajika kutoa ushahidi katika kesi hiyo itakayoanza kusikilizwa Aprili 9.

Katika kesi hiyo mume wa dada yake, William Balfour, anashtakiwa kwa mauaji hayo yaliyotokea, Oktoba 2008 huko Chicago.

Huson anakuwa shahidi wa kwanza baada ya kumtaja mwanamume huyo katika maelezo yake ya awali, huku akisema kuwa aliwahi kumuonya dada yake asikubali kuolewa na mwanamume huyo.
Share this article :

Post a Comment

KARIBU KATIKA WEBSITE YA KIJANJA, KUPATA HABARI MBALIMBALI ZA NDANI NA NJE YA NCHI. PIA UTAPATA MAMBO YA ACADEMIC. KARIBU SANA
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. GetInformedTz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger